RC wa dar Merck Sadiq anaingilia mchakato wa mahakama kuhusu mgomo wa madaktari

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Jamani hili tamko la vitisho kutoka kwa RC wa Dar Merck Sadiqi limekaa sawa? Ametangaza kwamba serikali itawachukulia hatua madaktari wote watakogundulika wanafanya mikutano ndani ya maeneo ya hospitali za serikali kwa lengo la kushawishi mgomo. Ametoa vitisho hivyo kwa kusema kuwa mahakama imeshautangaza mgomo kuwa ni batili.

Bila shaka RC huyo ana lengo la kutumia hatua za jinai (criminal action) dhidi ya hao wataokiuka 'hukumu' ya mahakama. Hii nadhani si sahihi kwani 'hukumu' iliyopata serikali kutoka High Court (labour Division) ilitokana na ombi la madai (civil suit) na hii haihusiani na mambo ya jinai (criminal).

Mimi naona RC Sadiq anakiuka utaratibu kwa kutoa vitishio visivyokuwa vya kufuata sheria, typical of CCM govt.

Nasema hivi kwa sababu hatua yoyote dhidi ya madaktari watakaokiuka 'hukumu' hiyo ya High Court lazima itoke High Court yenyewe kwanza, na siyo kutoka kwa vyombo vya serikali. RC huyu Anaingilia court process.

Najua serikali iko tayari kutumia nguvu za dola inazomiliki kutisha watu, kwa njia za kuburuza tu huku inakiuka sheria.

Isitoshe, huyu RC wa Dsma kapewe na nani kuzungumzia masuala ya huo mgomo Tanzania nzima? hayo mambo ni ya Waziru husika au Katibu wake Mkuu.

Nawasilisha kwa majadiliano.
 
Jamani hili tamko la vitisho kutoka kwa RC wa Dar Merck Sadiqi limekaa sawa? Ametangaza kwamba serikali itawachukulia hatua madaktari wote watakogundulika wanafanya mikutano ndani ya maeneo ya hospitali za serikali kwa lengo la kushawishi mgomo. Ametoa vitisho hivyo kwa kusema kuwa mahakama imeshautangaza mgomo kuwa ni batili.

Bila shaka RC huyo ana lengo la kutumia hatua za jinai (criminal action) dhidi ya hao wataokiuka 'hukumu' ya mahakama. Hii nadhani si sahihi kwani 'hukumu' iliyopata serikali kutoka High Court (labour Division) ilitokana na ombi la madai (civil suit) na hii haihusiani na mambo ya jinai (criminal).

Mimi naona RC Sadiq anakiuka utaratibu kwa kutoa vitishio visivyokuwa vya kufuata sheria, typical of CCM govt.

Nasema hivi kwa sababu hatua yoyote dhidi ya madaktari watakaokiuka 'hukumu' hiyo ya High Court lazima itoke High Court yenyewe kwanza, na siyo kutoka kwa vyombo vya serikali. RC huyu Anaingilia court process.

Najua serikali iko tayari kutumia nguvu za dola inazomiliki kutisha watu, kwa njia za kuburuza tu huku inakiuka sheria.

Isitoshe, huyu RC wa Dsma kapewe na nani kuzungumzia masuala ya huo mgomo Tanzania nzima? hayo mambo ni ya Waziru husika au Katibu wake Mkuu.

Nawasilisha kwa majadiliano.

You could be damned right! RC asiingize masuala ya jinai katika zuala hili la madai. Nitashangaa akituma polisi kukamata madaktari watakaokiuka na kuwafungulia mashitaka ya jinai pasipo na amri ya mahakama.

Lakini kwa kuwa serikali hii ni almost ya kidikteta I am afraidthat can happen!

Tusubiri.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom