Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,813
- 4,545
Picha: Mkuu wa Mkoa wa Iringa Queen Sendiga
MKUU wa Mkoa wa Iringa, Queen Sendiga amempa wiki mbili DED Mufindi, Netho Ndilito kupeleka maji katika vyoo vipya vya Shule ya Msingi Ifwagi. Pia ameagiza kufungwa kwa vyoo chakavu katika shule hiyo na badala yake wanafunzi 400 watumie vipya.
Hatua hii imekuja baada ya Nipashe kuripoti changamoto ya upungufu wa vyoo katika shule hiyo hali iliyopelekea wanafunzi wengine kujisaidia vichakani.
PIA SOMA:
- Iringa: Wanafunzi 400 wa Shule ya Msingi hatarini kuhara kutokana na changamoto ya choo kukosa maji