WAFANYABIASHARA MOSHI WAMSHANGAA RC MGWIRA KUMLAUMU RAIS MAGUFULI
Wafanyabiashara wa manispaa ya Moshi waliokuwa na kikao na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mgwira wameonesha kushangazwa na Kitendo cha Mkuu huyo kumlaumu hadharani Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Juma Raibu kuwa huwa anamshtaki kwa Rais Magufuli juu ya mambo mbalimbali.
Wafanyabiashara hao wametoa maoni yao kupitia Nungwi Fm kwa (sharti la kutotaka majina yao yaandikwe) baada ya kutoka kwenye Kikao cha kamati ya ulinzi na usalama cha Mkoa huo,akiongea kwaniaba ya wenzake Mfanyabiashara wa Kwanza alisema "Sisi tulikuja kuona namna gani kero yetu inatatuliwa kwa njia za amani lakini cha kustaajabisha ni kitendo cha RC kumshambulia Meya mbele yetu katika mambo yao ya siri akijua wazi sisi ni raia hatupaswi kusikia mambo yao,tunachoitaji kuona ni mshikamano ili Wafanyabiashara tupate ahueni kwenye maisha yetu" mwisho wa kunukuu
Pia Mfanyabishara mwingine alisema "Meya na RC wote ni watumishi wetu tunategemea wafanye kazi kwa muunganiko sio malumbano haya,Meya amefanya mazuri mengi nahata hili letu amelibeba sana, Kumgombeza na kumfukoe mbele yetu sio Sahihi ,wangesubiri tuondoke wafanye wao kwa wao,hili limetujengea picha mbay vichwani mwetu ,Tunaloomba ni watusikilize Jambo letu hili"
Source : Nungwi Online Fm
Wafanyabiashara wa manispaa ya Moshi waliokuwa na kikao na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mgwira wameonesha kushangazwa na Kitendo cha Mkuu huyo kumlaumu hadharani Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Juma Raibu kuwa huwa anamshtaki kwa Rais Magufuli juu ya mambo mbalimbali.
Wafanyabiashara hao wametoa maoni yao kupitia Nungwi Fm kwa (sharti la kutotaka majina yao yaandikwe) baada ya kutoka kwenye Kikao cha kamati ya ulinzi na usalama cha Mkoa huo,akiongea kwaniaba ya wenzake Mfanyabiashara wa Kwanza alisema "Sisi tulikuja kuona namna gani kero yetu inatatuliwa kwa njia za amani lakini cha kustaajabisha ni kitendo cha RC kumshambulia Meya mbele yetu katika mambo yao ya siri akijua wazi sisi ni raia hatupaswi kusikia mambo yao,tunachoitaji kuona ni mshikamano ili Wafanyabiashara tupate ahueni kwenye maisha yetu" mwisho wa kunukuu
Pia Mfanyabishara mwingine alisema "Meya na RC wote ni watumishi wetu tunategemea wafanye kazi kwa muunganiko sio malumbano haya,Meya amefanya mazuri mengi nahata hili letu amelibeba sana, Kumgombeza na kumfukoe mbele yetu sio Sahihi ,wangesubiri tuondoke wafanye wao kwa wao,hili limetujengea picha mbay vichwani mwetu ,Tunaloomba ni watusikilize Jambo letu hili"
Source : Nungwi Online Fm