VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Endelea na kejeli zako kwa watu. Endelea na kiburi chako cha kauli na matendo. Endelea na kusema chochote tena vyovyote. Endelea kujiamini hadi kupitiliza. Endelea kuona kuwa unaweza kusema au kufanya lolote na usiguswe. Lakini, CHUNGA SANA mwanangu!
Ita watu wa hovyo na wa ajabu, lakini si Dr. Shika. Umesikika ukimtaja kwa kejeli, dharau na kutojali madhara ya kufanya hivyo. Kwasasa unajadiliwa mahali ambapo hadi utamaliza u-RC wako hautapakanyaga. Unajadiliwa kwa kumzungumzia huyo Dr. Shika.
Ni ajabu 'kuharibu' mnada wa TRA na mambo kutulia hivi. Tafakari sana. Unajua kwasasa yuko wapi? Unajua anafanya nini? Unajua ana thamani gani kwa nchi hii na dunia kwa ujumla? Unajua kwanini kwasasa hasikiki tena? Nakwambia tena mwanangu, CHUNGA SANA!
Ulimi huponza kichwa. Hapo kwa Dr. Shika utaingia choo cha kike....utapotea mazima!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Geita, Tanzania)
Ita watu wa hovyo na wa ajabu, lakini si Dr. Shika. Umesikika ukimtaja kwa kejeli, dharau na kutojali madhara ya kufanya hivyo. Kwasasa unajadiliwa mahali ambapo hadi utamaliza u-RC wako hautapakanyaga. Unajadiliwa kwa kumzungumzia huyo Dr. Shika.
Ni ajabu 'kuharibu' mnada wa TRA na mambo kutulia hivi. Tafakari sana. Unajua kwasasa yuko wapi? Unajua anafanya nini? Unajua ana thamani gani kwa nchi hii na dunia kwa ujumla? Unajua kwanini kwasasa hasikiki tena? Nakwambia tena mwanangu, CHUNGA SANA!
Ulimi huponza kichwa. Hapo kwa Dr. Shika utaingia choo cha kike....utapotea mazima!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Geita, Tanzania)