Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Akizungumza baada ya kuzinduliwa uongozi mpya wa baraza la vijana wa kiislaam wa baraza kuu la waislamu mkoa wa Dsm bakwata, alisema mkoa una fursa nyingi za kiuchumi ambazo vijana wakijipanga vizuri, wanaweza kuibua miradi mbalimbali na kwamba Serikali ya mkoa iko tayari kuwasaidia.
"Kuna fedha zaidi ya shilingi bilioni 20 zilizotolewa na Rais John Magufuli kwa ajili ya mitaa ya jiji la Dar es salaam "alisema
Aidha Makonda amesema, kumekuwa na tabia ya kubeza jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano, lakini akawataka wananchi kutokatishwa tamaa na kuaahidi kuwa changamoto zote zilizopo zinaendelea kupatiwa ufumbuzi zikiwemo za ulinzi na usalama.
Mufti wa Tanzania sheikh abubakar zubairy bin Ally amelitaka baraza hilo la vijana kuzingatia katiba pamoja na majukumu yao na kuwaasa kutokuwa na fikra za kufanya mapinduzi ya viongozi wa bakwata au wa misikiti huku Kamishna mstaafu wa kanda maalum ya Dsm, CP Suleimani Kova akiwashauri vijana kujikita katika mambo ya uzalishaji mali pamoja na kuzingatia sheria katika utekelezaji wa majukumu yao.
Source: Channel Ten