GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,545
- 108,873
Nadhani hii si mara yangu ya Kwanza kuja humu JamiiForums na kukusifia kuwa Wewe ni mchapakazi mzuri na mpambanaji wa Kimaendeleo hasa katika huu Mkoa wako wa Dar es Salaam tofauti na watangulizi wako wengi tu ila kuna Kasoro zako ambazo bado naziona zipo na hujaziacha kitu ambacho mara nyingi zinakushusha japo Watu wako wa karibu wanakuficha ila wakikaa wao kwa wao wanakucheka na hata kukudhihaki.
Kasoro yangu kubwa ya kuzaliwa ni ya kupenda kusema ukweli tena kwa Mtu ambaye namheshimu, nampenda na namtakia mafanikio mema bila chembe yoyote ile ya Unafiki au Kupepesa macho au Kutikisa masikio na Kumung'unya maneno nikiwa nategemea kwamba ninavyomsema basi atabadilika na hatimaye kuja kuwa bora zaidi Kiuwajibikaji.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ( RC ) Paul C. Makonda ukifanyia Kazi ' mapungufu ' yako haya makubwa nakuhakikishia huko mbele utakuja kuwa ' bonge ' la Kiongozi na si ajabu hata hawa ' wanaokubeza ' leo wao ndiyo wakawa sehemu ya Watu watakaokuwa wanakupigia ' chapuo ' na Kukuunga mkono.
Mkuu wa Mkoa Makonda una......
Nawasilisha.
Kasoro yangu kubwa ya kuzaliwa ni ya kupenda kusema ukweli tena kwa Mtu ambaye namheshimu, nampenda na namtakia mafanikio mema bila chembe yoyote ile ya Unafiki au Kupepesa macho au Kutikisa masikio na Kumung'unya maneno nikiwa nategemea kwamba ninavyomsema basi atabadilika na hatimaye kuja kuwa bora zaidi Kiuwajibikaji.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ( RC ) Paul C. Makonda ukifanyia Kazi ' mapungufu ' yako haya makubwa nakuhakikishia huko mbele utakuja kuwa ' bonge ' la Kiongozi na si ajabu hata hawa ' wanaokubeza ' leo wao ndiyo wakawa sehemu ya Watu watakaokuwa wanakupigia ' chapuo ' na Kukuunga mkono.
Mkuu wa Mkoa Makonda una......
- Tabia ya Kukurupuka sana katika mipango yako
- Unapenda kutaka upewe Sifa kuliko kufanya Vitu vya Kiuhalisia na vyenye Tija kwa wengi
- Tabia kila unapoongea na hadhira / umma ' body language ' yako huwa 100% imejaa dharau na ujivuni kitu ambacho kwa Kiongozi wa Watu si kizuri
- Tabia ya Kulazimisha ukubwa hata pasipotakiwa Kuulazimisha
- Tabia ya Kuanzisha Kampeni kadha wa kadha lakini zisizo na mwisho mzuri na wenye ufanisi
- Tabia ya kupenda sana Kushindana na ' Critics ' wako kitu ambacho mara nyingi kinakuharibia na unajikuta unakosea mno katika mipango yako
- Tabia ya kupenda sana kuwa juu ya hata waliokuzidi ' Kiitifaki ' kitu ambacho hakitakusaidia mno na jitahidi ujifunze Kujinyenyekeza kwa hao wakubwa wako wa ' Kiitifaki ' ili waweze kukupa ushirikiano mkubwa kwani wengi wao wanakulalamikia japo ukikutana nao wanakuchekea kwakuwa tu wanajua Wewe una ' influence ' fulani ' mahala ' fulani.
Nawasilisha.