RC Makonda avamia Clouds na kuwatisha SHILAWADU

Habari kama hizi za kichochezi na za uzushi ndizo zinazotuponza wanaJf mbona tuliokuepo mjengoni mda huo hatujasikia lolote na hakuna chochote kilichotokea.

Au umetumwa?
Clouds ni taasisi kubwa inayoongozwa kwa misingi na taratibu zake haiwezekani mtu from no where aje tu aingie mpaka peoduction bila kufata utaratibu!

Acha uzushi watanzania puuzeni hizi taarifa si za kweli!!.

Unauhakika habari sio za kweli na za kichochezi? "Evil succeeds when good men do nothing" - Edmund Burke. cha msingi fuatilia kujiridhisha. Nyakati hizi mitandao ndio source ya uongo na ukweli vile vile hasa ule ambao ni vigumu kuupata kwa "mainstream media"
 
Ndio maana akakimbilia Redio Uhuru ambayo sijui kama ina msikilizaji..kwa vitendo kama hivi ndio unagundua kwamba Bashite alipata sifuri
 
Mkuu hapana unakosea hii ni Armed Robbery ya wazi acha kutetea kumbuka maelezo ni kwamba wameshinikiza kupewa hiyo dvd kwa nguvu huku wakiwaonesha smg kwa mujibu wa mtoa mada inakuwaje kutishia pekee
 
=====
Msomaji, vema pia ukasoma hapa > Mwanamama kupitia Uhuru FM, adai kuzalishwa na Askofu Gwajima na kutelekezwa!
=====

Makonda hua anafika office za clouds mara kwa mara. Siku zingine anashinda hapo mpaka jioni. Siku ya Alhamis Makonda alifika office za Clouds Cha ajabu siku hiyo alikaa mpaka usiku akawa anamtafuta soudy Brown na Qwisser wa SHILAWADU muda huo walikuwa bado hawajafika kazini basi akawa anazungukazunguka tu ofisi hii anatokea ile kama mfanyakazi wa Clouds.

Kwenye Mida ya Saa kumi hivi akakutana na kina Soudy pamoja na prodyuza wa kipindi wakawa wanaongea kwa uficho hivi na usiri tukajua tu ni mambo ya kawaida ya kuhitaji uprivate lakini siku ile ulikuwa unatia mashaka sana.

Kumbe Makonda alikuja na Story ya mwanamke mmoja ambaye yeye Makonda alisema huyo mwanamke amezaa na mchungaji Gwajima na ametelekeza akawa anataka arekodiwe na ubuyu uruke kwenye kipindi cha SHILAWADU.

Basi wakakubalia kwa kuwa ni habari itabidi huyo mwanamke arekodiwe na kipindi kiruke siku ya jana lakini kawaida ya Kipindi cha SHILAWADU ubuyu ukipatikana lazima kila mtu apewe Natural Justice ya kusikilizwa pande zote mbili sababu huwa ndiyo kawaida ya kipindi.

Makonda siku hiyo hiyo ya Alhamisi akamwambia Soudy ajiandae then huyo mwanamke mnayemuona kwenye video na mtoto aliletwa na wasaidizi wa Makonda ahojiwe na Soudy Brown tayari kwa kurushwa kwa kipindi.

Siku ya Ijumaa ambayo ilikuwa ni jana SHILAWADU wakamtafuta Gwajima kwa upande wake kama anaifahamu hiyo ishu na je mwanamke huyo aliyetajwa ni kweli kwasababu tunaelewa ugomvi uliopo kati ya Makonda na Gwajima isijekuwa SHILAWADU wanatumika kuwafitinisha watu vibaya!

kwa bahati mbaya Gwajima hakupatikana jana ijumaa kwa ajili ya kurekodiwa na kufanyiwa mahojiano.

SHILAWADU wakatumia busara mpaka apatikane Gwajima scene ya Dada mwenye mtoto ziende kwa pamoja na ya mchungaji Gwajima kama kawaida ya POVU inavyokuwaga.

Jana usiku sasa kumbe Makonda alikuwa anafuatilia kipindi cha SHILAWADU aone kama kile kipande kitaruka hewani wapi ndiyo akaamua kuja Clouds na magari mawili yeye mwenyewe Makonda na Watu kama nane hivi wakiwa na Bunduki aina ya SMG geti la kawaida mlinzi alifungua geti kwasababu amezoeleka Mh anakujaga mjengoni wakafunguliwa kisha wakaingia ndani.

Walipofika reception wakazuiwa kuingia ndani sababu hatuna utaratibu wa kuruhusu wageni baada ya saa Nne usiku kuingia ndani ya Ofisi kama siyo mfanyakazi wa CLOUDS.

Alipoona wanazuiwa wakatoa bunduki zao mlinzi akashurutishwa afungue mlango kwa nguvu sababu walimtishia na Silaha mlimzi akafungua mlango wakaenda naye hadi studio kipindi kilikuwa kinaendelea hewani.

Makonda akawatoa nje Soudy na Mwenzake Qwisser akawauliza kwanini video aliyowaletea haijachezwa wakaelezea utaratibu jinsi utaratibu ulivyokuwa Qwisser wakati anajielezea akapigwa mtama akaanguka chini wakavamia mitambo ya transmission kwenye traycaster wakitaka kile kipande kirushwe hewani prodyuza wa kipindi akamuambia Makonda kwanini anavunja utaratibu na kutumia nguvu na ameshapewa utaratibu akapigwa na kitako cha Bunduki mgongoni akaanguka chini bahati mbaya kipindi kilikuwa kimefika mwisho.

Wakamshurutisha Prodyuza wa SHILAWADU anaitwa Chriss awape kile kipande wakaondoka naye wakati wanaondoka Ruge alikuja na Polisi akaingia lakini tayari walikuwa wameondoka ofisini wamechukua hicho kipande cha Video ya huyo mwanamke.

Hizo video zilichukuliwa kwa nguvu na Makonda na hao watu waliokuwa na Silaha inasemekana Makonda ana timu yake wanazisambaza kwa kasi na hatujui lengo lake ni nini.

Hata mkihitaji footage za Camera zipo jinsi tukio lilivyokuwa usiku wa jana.

====
Kutoka kwa wadau wa Clouds Media

Tunaomba mtuwekee cctv footage ya tukio. Hapo inabidi huyo Makonda akamatwe na aeleze hiyo private militia yake yenye SMG ni akina nani na je wana permit gani?
Tuache kucheka au kutetea mambo kama haya!
 
Mkuu hapana unakosea hii ni Armed Robbery ya wazi acha kutetea kumbuka maelezo ni kwamba wameshinikiza kupewa hiyo dvd kwa nguvu huku wakiwaonesha smg kwa mujibu wa mtoa mada inakuwaje kutishia pekee
Sawa lkn hakuna risasi iliyopigwa. Ila unyang'anyi wa kutumia nguvu upo pia
 
Back
Top Bottom