RC Kunenge: Tumewakamata watuhumiwa 314 wa uhamihaji haramu Mabwepande

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,806
11,968
VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA DAR ES SALAAM VYAKAMATA WATUHUMIWA 314 WA UHAMIAJI HARAMU, RC KUNENGE ATOA ONYO KALI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge amesema Katika operesheni ya pamoja iliyofanywa na Vyombo vya ulinzi na usalama Kata ya Mabwepande January 24 na 25 imefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 314 wa uhamihaji haramu ambapo baada ya kuhojiwa watuhumiwa 84 walibainika kuwa ni wahamiaji haramu.

RC Kunenge amesema Katika watuhumiwa hao 79 wanatokea Burundi, Malawi 02, DRC Kongo 02 na mmoja kutoka Msumbiji ambapo amebainisha watuhumiwa hao wote watafikishwa mahakamani kwa kosa la kuishi nchini kinyume na sheria.

Aidha RC Kunenge amesema watuhumiwa wengine 33 bado wanaendelea kuchunguzwa uraia wao huku wengine 197 waliobaki waliachiliwa baada ya kubainika kutokuwa na dosari Katika uraia wao.

Hata hivyo RC Kunenge amebainisha kuwa Katika uchunguzi ukiofanyika baadhi ya watuhumiwa walibainika kuwa na viashiria vya kujihusisha na uhalifu wa Wizi, Unyang'anyi, Uporaji wa ardhi na kuuza kwa utapeli pamoja na kuzuia wamiliki halali wa ardhi kuingia Katika maeneo yao Jambo linalozua migogoro ya ardhi.

Sanjari na hayo RC Kunenge amesisitiza kuwa utaratibu huo unafanyika kwa kuzingatia sheria na haki za binadamu na watahakikisha hakuna yoyote atakaeonewa ambapo pia ametoa wito kwa wakazi wa eneo husika kuendelea kushirikiana na Vyombo vya ulinzi na usalama Katika kuwafichua wahalifu.
IMG-20210128-WA0018.jpg
IMG-20210128-WA0017.jpg
IMG-20210128-WA0014.jpg
 
Mbopo huko mbona nasikia wamajezana.

Kuna jamaa alisema aliponea kupigwa shaba baada ya kudanganywa kuna kiwanja kinauzwa, kufika anaenda kupeleka hela akarushiwa risasi.

Akawasha gari akakimbia. Uhalifu msitu wa Pande ni mkubwa
 
Mbona huko Masaki na Oysterbay Wanyasa wamejaa huko wake kwa waume wakifamya kazi za ndani kwenye majumba ya raia wa kigeni ?
Wanyasa watu wazuri hawana shida

Ulishasikia mnyasa jambazi?

Hiyo mi nchi mingine imejaa mijambazi
 
Serekali ilitakiwa ibadirishe mfumo wa hawa wahamiaji kuwafunga miaka halafu unawarudisha cjui Kama inaleta maana
 
Wanyasa wengi sana wapo wapo tu. Kuna mmoja nilimtafuna mwishoni mwa mwaka jana nilikuwa na wasiwasi kuwa sio mbongo lkn akawa anakataa. Kuna muda alisema nimuunganishie whatsapp, wakati ananitajia namba akanitajia kwa kiingereza mwanzo mwisho kitu ambacho wabongo huwa hatufanyi.
Nikamwambia hakika sasa nimeng'amua ya kuwa wewe u mnyasa wa Malawi.
 
Wanyasa wengi sana wapo wapo tu. Kuna mmoja nilimtafuna mwishoni mwa mwaka jana nilikuwa na wasiwasi kuwa sio mbongo lkn akawa anakataa. Kuna muda alisema nimuunganishie whatsapp, wakati ananitajia namba akanitajia kwa kiingereza mwanzo mwisho kitu ambacho wabongo huwa hatufanyi.
Nikamwambia hakika sasa nimeng'amua ya kuwa wewe u mnyasa wa Malawi.
Mbona sijaiona hii story kule kwenye Uzi pendwa wetu wa Kimasikhara??

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA DAR ES SALAAM VYAKAMATA WATUHUMIWA 314 WA UHAMIAJI HARAMU, RC KUNENGE ATOA ONYO KALI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge amesema Katika operesheni ya pamoja iliyofanywa na Vyombo vya ulinzi na usalama Kata ya Mabwepande January 24 na 25 imefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 314 wa uhamihaji haramu ambapo baada ya kuhojiwa watuhumiwa 84 walibainika kuwa ni wahamiaji haramu.

RC Kunenge amesema Katika watuhumiwa hao 79 wanatokea Burundi, Malawi 02, DRC Kongo 02 na mmoja kutoka Msumbiji ambapo amebainisha watuhumiwa hao wote watafikishwa mahakamani kwa kosa la kuishi nchini kinyume na sheria.

Aidha RC Kunenge amesema watuhumiwa wengine 33 bado wanaendelea kuchunguzwa uraia wao huku wengine 197 waliobaki waliachiliwa baada ya kubainika kutokuwa na dosari Katika uraia wao.

Hata hivyo RC Kunenge amebainisha kuwa Katika uchunguzi ukiofanyika baadhi ya watuhumiwa walibainika kuwa na viashiria vya kujihusisha na uhalifu wa Wizi, Unyang'anyi, Uporaji wa ardhi na kuuza kwa utapeli pamoja na kuzuia wamiliki halali wa ardhi kuingia Katika maeneo yao Jambo linalozua migogoro ya ardhi.

Sanjari na hayo RC Kunenge amesisitiza kuwa utaratibu huo unafanyika kwa kuzingatia sheria na haki za binadamu na watahakikisha hakuna yoyote atakaeonewa ambapo pia ametoa wito kwa wakazi wa eneo husika kuendelea kushirikiana na Vyombo vya ulinzi na usalama Katika kuwafichua wahalifu.
View attachment 1688047View attachment 1688048View attachment 1688049
Safi sana RC, safisha jiji
 
Mbona huko Masaki na Oysterbay Wanyasa wamejaa huko wake kwa waume wakifamya kazi za ndani kwenye majumba ya raia wa kigeni ?
Siyo majumba ya kigeni tu, infact ya wazawa ndio wako wengi, mbezi beach, mikocheni na msasani wako bwelele, mpaka sinza...
 
Back
Top Bottom