RC Kafulila: Rais Samia Suluhu ametoa TZS 2.3Trilioni kwaajili ya Wafanyakazi

MAELEKEZO 8 YA RC KAFULILA KWENYE MEI MOSI SIMIYU, ILIYOFANYIKA KIMKOA WILAYANI MEATU LEO 01|05|2022

1. Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zina sheria zinazolinda haki ya mfanyakazi kwa kiasi kikubwa ndio maana mchakato wa kumfukuza kazi mtumishi ni mgumu sana. Hata hivyo ameonya kuwa dhamira hiyo njema ya Serikali yenye lengo la kulinda haki ya mtumishi inakwaza ufanisi kwani baadhi ya watumishi wenye utendaji usioridhisha wamedumu kutokana na ulinzi huo wa kisheria.

2. Amewapongeza wanawake kuendelea kupiga hatua katika uwajibikaji kwani kati ya watumishi 145 waliopata zawadi ya ufanyakazi bora ,wafanyakazi 46 tu, sawa na asilimia 32% ni wanawake.

3. Pamoja na changamoto zote kwa watumishi lakini kuna mengi serikali imefanya katika kipindi kifupi kusaidia wafanyakazi ikiwemo;
# kutenga zaidi ya trilioni 2.3 kwa ajili ya wafanyakazi wanaolipwa na mfuko wa PSSSF ambao walistaafu kabla ya mwaka 1999. " Huu ni uamuzi wa kimapinduzi kwa watumishi kwani madai haya ni tangu awamu ya 3. Hivyo mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Wafanyakazi wa halmashauri na mkoa Simiyu, ndani ya mwaka1 wamelipwa zaidi ya bilioni 2.1 za malimbikizo ya mishahara ya miaka mingi ambayo ni sawa na 40% ya deni lote.

4. Amewataka wakurugenzi na mamlaka za serikali zilizotoa uhamisho kwa watumishi bila kuwalipa fedha ya uhamisho wajieleze ndani ya siku7 na kuagiza kuwa,hataki kuona mfanyakazi anahamishwa kabla ya kulipwa stahiki zake na kwamba ndani ya wiki siku7 chama cha wafanyakazi kimpatie orodha ya watumishi waliohamishwa kwa utaratibu huo ili achukue hatua dhidi ya waajiri.

5. Amewataka waajiri mkoani Simiyu wa sekta binafsi na Umma kuheshimu sheria za kazi ikiwemo uhuru wa wafanyakazi kuwa wanachama na kushiriki harakati za vyama vya wafanyakazi kwakuwa vipo kisheria na kwamba ametaka vyama vya wafanyakazi ndani ya siku7 kuwasilisha majina ya waajiri wanaotisha na kukiuka sheria za kazi ikiwemo kunyanyaswa watumishi ili achukue hatua stahiki.

6. Amewahakikishia watumishi wote kuwa haki zao zilizo ndani ya mamlaka za serikali kuanzia mkoa kushuka chini atafanyia kazi na watapata. Na kwamba haki za watumishi zilizo nje ya uwezo wake atazifikisha mamlaka husika zifanyiwe kazi kadiri inavyowezekana na kutaka watumishi kuendelea kuwajibika kikamilifu wakati haki zao zinashughulikiwa.

7. Ametaka watumishi watambue nafasi yao katika kujenga uchumi ambao ni msingi wa stahiki zao za kazi ikiwemo nyongeza za mshahara . Amesema karibu bilioni 600 au asilimia 40% ya mapato kila mwezi inatumika kulipa mishahara.Upo uhusiano kati ya ufanisi wa mamlaka za Umma na ufanisi wa sekta binafsi. Na kwamba katika mataifa 13 makubwa zaidi kiuchumi duniani, 25% ya uchumi wao inatokana na ufanisi wa taasisi ambao lazima tujiulize kwa kiasi gani taasisi zetu za umma ni mzigo na kiasi gani zinachochea uchumi. Tukijua hilo tutaona wajibu wetu ambao tukiutekeleza tutaweza kupata mishahara mizuri hata kama tunacholipwa hakifikii asilimia 15% ya makusanyo ya serikali kila mwezi.

Akitoa elekezo la nane Mhe. Kafulila amesema;

8.Wafanyakazi wa Tanzania wanalindwa na sheria za ajira na utumishi kazini kuliko mataifa mengi duniani ndiyo maana mchakato ya kumfukuza mfanyakazi ni mgumu sana kulinganisha na mataifa mengi. Hili linasaidia sana kulinda haki za ajira kwa wafanyakazi ingawa kwa upande wa pili linatoa mwanya kwa wafanyakazi wasio na utendaji wa kuridhisha kuendelea kuwa mzigo kwa serikali na hata kwenye kodi ya wananchi. Suala hili sijaona likizungumzwa kwa sauti kubwa na vyama vya wafanyakazi lakini ni tatizo kubwa kwani wafanyakazi wazembe wanakwaza wananchi na ni hasara kwa serikali.

Mkoa wa Simiyu una vyama vya Wafanyakazi 5 kati ya vyama vya Wafanyakazi 13 vilivyoandikishwa na TUCTA. Vyama hivyo ni TALGWU,TUGHE, TUICO, CWT na TAMICO.Mwisho.
Huyu naye msomi lakini anajifanya anafel padogo tu.Asahihishe kauli yake siyo rais ametoa hela.Kwani katoa mfukoni mwake.Yeye na rais mabosi wao ni sisi.Na huu mrejesho wa kodi zetu wananchi.
 
Hizi kauli zinachangia "mfumko wabei" mtaani mambo ya mishahara iwe siri... Mboni hatusikiagi mshahara wa Mayele wa Yanga.. Au Kagere was ssc
 
Sukuma gangus(singular) katika ubora wake
😂😂😂😂
Wana hasira kiasi kwamba hata Raisi akisema malaria inaletwa na mbu watabisha! Shida yao hapo si hiyo, 'fedha imeletolewa na raisi' bali huyo raisi ndo shida yao. Kwa vile hawana cha kumfanya basi ndo wanazidi kufura!!
 
Hivi kwaninini neno "serikali" limeachwa na yanatumia majina ya watu? Au serikali haipo tena? Ni aibu na fedheha sana!
Katika hotuba ya Mama siku ya may day alitumia maneno "Serikali yenu" mara kwa mara. Lakini kwasababu bado hawajatoka kwenye akili ya Jiwe kuabudu na kusifu ili kupata vyeo. Basi tutasubiri sana, watu kuacha hiyo tabia ya ajabu. Maana ndiyo iliyo wapandisha watu vyeo, kupewa pesa barabarani na hata kupelekewa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, enzi zile.
 
MAELEKEZO 8 YA RC KAFULILA KWENYE MEI MOSI SIMIYU, ILIYOFANYIKA KIMKOA WILAYANI MEATU LEO 01|05|2022

1. Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zina sheria zinazolinda haki ya mfanyakazi kwa kiasi kikubwa ndio maana mchakato wa kumfukuza kazi mtumishi ni mgumu sana. Hata hivyo ameonya kuwa dhamira hiyo njema ya Serikali yenye lengo la kulinda haki ya mtumishi inakwaza ufanisi kwani baadhi ya watumishi wenye utendaji usioridhisha wamedumu kutokana na ulinzi huo wa kisheria.

2. Amewapongeza wanawake kuendelea kupiga hatua katika uwajibikaji kwani kati ya watumishi 145 waliopata zawadi ya ufanyakazi bora ,wafanyakazi 46 tu, sawa na asilimia 32% ni wanawake.

3. Pamoja na changamoto zote kwa watumishi lakini kuna mengi serikali imefanya katika kipindi kifupi kusaidia wafanyakazi ikiwemo;
# kutenga zaidi ya trilioni 2.3 kwa ajili ya wafanyakazi wanaolipwa na mfuko wa PSSSF ambao walistaafu kabla ya mwaka 1999. " Huu ni uamuzi wa kimapinduzi kwa watumishi kwani madai haya ni tangu awamu ya 3. Hivyo mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Wafanyakazi wa halmashauri na mkoa Simiyu, ndani ya mwaka1 wamelipwa zaidi ya bilioni 2.1 za malimbikizo ya mishahara ya miaka mingi ambayo ni sawa na 40% ya deni lote.

4. Amewataka wakurugenzi na mamlaka za serikali zilizotoa uhamisho kwa watumishi bila kuwalipa fedha ya uhamisho wajieleze ndani ya siku7 na kuagiza kuwa,hataki kuona mfanyakazi anahamishwa kabla ya kulipwa stahiki zake na kwamba ndani ya wiki siku7 chama cha wafanyakazi kimpatie orodha ya watumishi waliohamishwa kwa utaratibu huo ili achukue hatua dhidi ya waajiri.

5. Amewataka waajiri mkoani Simiyu wa sekta binafsi na Umma kuheshimu sheria za kazi ikiwemo uhuru wa wafanyakazi kuwa wanachama na kushiriki harakati za vyama vya wafanyakazi kwakuwa vipo kisheria na kwamba ametaka vyama vya wafanyakazi ndani ya siku7 kuwasilisha majina ya waajiri wanaotisha na kukiuka sheria za kazi ikiwemo kunyanyaswa watumishi ili achukue hatua stahiki.

6. Amewahakikishia watumishi wote kuwa haki zao zilizo ndani ya mamlaka za serikali kuanzia mkoa kushuka chini atafanyia kazi na watapata. Na kwamba haki za watumishi zilizo nje ya uwezo wake atazifikisha mamlaka husika zifanyiwe kazi kadiri inavyowezekana na kutaka watumishi kuendelea kuwajibika kikamilifu wakati haki zao zinashughulikiwa.

7. Ametaka watumishi watambue nafasi yao katika kujenga uchumi ambao ni msingi wa stahiki zao za kazi ikiwemo nyongeza za mshahara . Amesema karibu bilioni 600 au asilimia 40% ya mapato kila mwezi inatumika kulipa mishahara.Upo uhusiano kati ya ufanisi wa mamlaka za Umma na ufanisi wa sekta binafsi. Na kwamba katika mataifa 13 makubwa zaidi kiuchumi duniani, 25% ya uchumi wao inatokana na ufanisi wa taasisi ambao lazima tujiulize kwa kiasi gani taasisi zetu za umma ni mzigo na kiasi gani zinachochea uchumi. Tukijua hilo tutaona wajibu wetu ambao tukiutekeleza tutaweza kupata mishahara mizuri hata kama tunacholipwa hakifikii asilimia 15% ya makusanyo ya serikali kila mwezi.

Akitoa elekezo la nane Mhe. Kafulila amesema;

8. Wafanyakazi wa Tanzania wanalindwa na sheria za ajira na utumishi kazini kuliko mataifa mengi duniani ndiyo maana mchakato ya kumfukuza mfanyakazi ni mgumu sana kulinganisha na mataifa mengi. Hili linasaidia sana kulinda haki za ajira kwa wafanyakazi ingawa kwa upande wa pili linatoa mwanya kwa wafanyakazi wasio na utendaji wa kuridhisha kuendelea kuwa mzigo kwa serikali na hata kwenye kodi ya wananchi. Suala hili sijaona likizungumzwa kwa sauti kubwa na vyama vya wafanyakazi lakini ni tatizo kubwa kwani wafanyakazi wazembe wanakwaza wananchi na ni hasara kwa serikali.

Mkoa wa Simiyu una vyama vya Wafanyakazi 5 kati ya vyama vya Wafanyakazi 13 vilivyoandikishwa na TUCTA. Vyama hivyo ni TALGWU,TUGHE, TUICO, CWT na TAMICO.Mwisho.
Kaziiendelee kufanyika, Simiyu tuko vizuri Sana,
 
Back
Top Bottom