RC Kafulila awanyoosha wachina wa CHICCO, ni wale waliotaka kutupiga TZS 15BL kwenye ujenzi wa barabara ya Mwigumbi-Maswa kilometa 57 kwa TZS 75BL

Mwanahabari wa Taifa

JF-Expert Member
May 27, 2020
1,450
799
IMG-20220714-WA0186.jpg



Kampuni ya kichina ya CHICCO yatekeleza agizo la RC Kafulila, tayari imekamilisha marudio ya barabara yenye urefu wa kilometa 10 zenye thamani ya tzs15bl.

==
Kampuni ya Kichina ya CHICCO inayotekeleza ujenzi wa Barabara ya Mwigumbi - Maswa yenye urefu wa kilomita57, ilianza ujenzi tangu mwaka 2018 kwa thamani ya zaidi ya shilingi za kitanzania billion 75. Wachina hawa walikwaa kisiki baada ya kutakiwa kurudia ujenzi wa vipande vya barabara vinavyofikia kilometa 10 kutokana na kujenga chini ya kiwango kilichowekwa.

Agizo hilo la kutakiwa kurudia ujenzi lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe David Kafulila Juni 5, 2021 ikiwa ni wiki moja tu baada ya kuripoti mkoani Simiyu kama Mkuu wa Mkoa mpya. Leo ikiwa ni mwaka mmoja sasa tangu agizo hilo, RC Kafulila akihojiwa na kituo cha EATV amekiri kuridhishwa na kazi iliyofanywa na kwamba ujenzi upo zaidi ya asilimia 96% kwa viwango vinavyokubalika.

"Nakumbuka ilikuwa ni wiki ya kwanza baada ya kuripoti kama RC, hii barabara niliona wakati nakuja kuripoti Simiyu. Nilifanya ziara na Bodi ya Barabara na kuelekeza marudio ya barabara na kumwelekeza mkandarasi kurudia. Nilimsisitiza barabara yake haitapokewa na Mhe. Rais ikiwa chini ya kiwango" alisema Kafulila na kuongeza kuwa, "mbali ya kurudia barabara, pia mshauri mwelekezi(consultant) alibadilishwa. Sasa watu wote wakipita wanafurahi kuona serikali sasa itapokea barabara imara sawa na thamani ya fedha zao wanazozitoa kupitia kodi na tozo mbalimbali."

"Huu ni ujumbe wangu kwa wakandarasi wote mkoani Simiyu, hakuna mradi utakaopokelewa ukiwa chini ya kiwango. Kwasasa nina amani hata Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan akipita kukagua nina amani kwamba fedha iliyoletwa ndani ya mkoa wetu kwajili ya barabara na hata miradi mingine, thamani ya pesa(value for money) inaonekana. Wakandarasi wababaishaji hawana nafasi, nimeshavunja na nitaendelea kuvunja mikataba na kila mbabaishaji aliyepata mradi kwa bahati mbaya Simiyu," alisisitiza zaidi.

"Serikali inalaza mabilioni ya fedha barabaran ndio maana lazma kuhakikisha tunabanana. Yaani gharama kilomita 1 ya lami ni takribani 1.5 bn., pesa ambazo zinatosha kukamilisha majengo ya kituo cha afya. Sasa upewe mabilioni yote hayo na bado ukabidhi barabara ambayo baada ya mwaka tu imeharibika na kuhitaji mabilioni mengine ya ukarabati? Huu ni ushenzi ambao hauwezi kupewa nafasi ndani ya awamu ya sita, na kwa upande wetu tutatimiza kipande chetu Simiyu, " alimalizia.

#SISITUKO TAYARI KUHESABIWA TAREHE 23/08/2022,WEWE JEE?!
 
Mkurugenzi wa TANROADS alikuwa wapi
Waziri wa ujenzi naye alikuwa wapi
Team ya ufundi ya TANROADS inafanya nini mpaka RC abaini makosa yote hayo tena ya kitaalamu
Mkurugenzi wa TANROADS alikuwa wapi
Waziri wa ujenzi naye alikuwa wapi
Team ya ufundi ya TANROADS inafanya nini mpaka RC abaini makosa yote hayo tena ya kitaalamu
Hahahahaaaa..hao jamaa zetu wa Tanroads, ni vitambi na kunenepeana tu, hata huwezi ona shingo zao..... kaazi iendelee.
 
Hili ni jambo jema sana kafanya mh kafulila, viongozi wote waige mfano huu, tusikubali kulaliwa kwa vipande vidogo vya fedha,kongole kwake Kafulila.

Kwa huku DSM kwasasa barabara za lami wanajitahidi sana kujenga kwa viwango,hilo napongeza tanroads na tarura, ila ningeomba wakuu wetu wa wilaya na RC kwa barabara za changarawe/vifusi kuna uhuni mwingi sana unafanyika, na upigaji hivyo hazidumu hata kwa mvua moja tu, eneo hili lisimamiwe sana,tena kwa kuanzia bajeti hii.

Tukague aina ya vifusi pamoja na idadi kama boq inavyosema kabla mkandarasi hajasambaza.Mimi naamini barabara ikiwekwa kifusi sahihi na kwa utoshelezo sahihi itadumu na kupitika vipindi vyote vya mvua,na kupunguza maumivu na hasara kwa wananchi.Ijumaa karim
 
Mkurugenzi wa TANROADS alikuwa wapi

Waziri wa ujenzi naye alikuwa wapi

Team ya ufundi ya TANROADS inafanya nini mpaka RC abaini makosa yote hayo tena ya kitaalamu
Ndio nilichoshangaa na mimi. Mkuu wa Mkoa na barabara wapi?
 
Acheni utani, Mkandarasi ameingia mkataba na TANROADS kuiwakilisha Wizara ya Ujenzi, barabara inaanzia Shinyanga hadi Simiyu, na Kipande kilichorudiwa kinaanzia Shinyanga, kwa mazingira hayo TANROADS imefanya kazi kubwa sana kumrudisha mkandarasi site(Sina hakika kama Mkuu wa Mkoa mmoja ambaye yupo TAMISEMI awe na nguvu zaidi ya wizara ya Ujenzi ambayo ndio boss wa TANROADS aliye ingia mkataba na Mkandarasi). Taarifa ambazo zipo ni kuwa Mhandasi mshauri ameshafungiwa na TANROADS kutofanya kazi hapa nchini. Team nyingine ya wahandisi wanafanya tafiti ili kubaini makosa.
 
Tumbili acha kujipa promo ridhika na ulichopewa.

Kafulila anafanya kazi na naona kuanzia kwenye U RAS ilimuimarisha sana maana anacheza namba zote mkoani na anajua apite njia ipi kufika apongezwe maana anafuatilia mambo
 
Acheni utani, Mkandarasi ameingia mkataba na TANROADS kuiwakilisha Wizara ya Ujenzi, barabara inaanzia Shinyanga hadi Simiyu, na Kipande kilichorudiwa kinaanzia Shinyanga, kwa mazingira hayo TANROADS imefanya kazi kubwa sana kumrudisha mkandarasi site(Sina hakika kama Mkuu wa Mkoa mmoja ambaye yupo TAMISEMI awe na nguvu zaidi ya wizara ya Ujenzi ambayo ndio boss wa TANROADS aliye ingia mkataba na Mkandarasi). Taarifa ambazo zipo ni kuwa Mhandasi mshauri ameshafungiwa na TANROADS kutofanya kazi hapa nchini. Team nyingine ya wahandisi wanafanya tafiti ili kubaini makosa.
Mh
 
Back
Top Bottom