Rc, Dc na Polisi vitisho katika karne hii siyo suluhu ya migogoro.

Naytsory

JF-Expert Member
Nov 3, 2011
2,192
791
Kuwatisha walimu, kuwaagiza maafisa elimu na Dc kwenda kufundisha ni kupoteza muda wa kutatua tatizo. Suluhu ya mgogoro wa walimu ni serikali ikubali kukaa na walimu ili kukubaliana kwa kile kinachowezekana na siyo vitisho kama wanavyofanya sasa. Wilaya moja ina Dc na afisa elimu wangapi? Je shule, madarasa na masomo yako mangapi, je Dc au afisa elimu atamudu? Au ni kupoteza muda tu. Kama hawa ndiyo viongozi tulio nao kazi tunayo. Maana yawezekana hapo ndiyo uwezo wao wa kufikiri unapoishia. Pole kwa watanzania.
 
ni bora kukaa na wanafunzi wa milembe! kuliko kukaa na viongozi wa chama cha mabwepande!
 
Hivi hii serikali ya CCM imekwisha fanya mahakama kama shock absorber yake! Maana kila inapokabiliwa na hoja nzito za kujibu au kutoa maamuzi magumu inakimbilia mahakamani ili hoja isijadiliwe au uamuzi ucheleweshwe kwa kisingizio cha kuingilia uhuru wa mahakama!
 
Viongozi hawa lazima wafanye utafiti kabla ya kutoa kauli kwa umma, kwani Watanzania wa leo wana uwezo wa kuchambua mambo na kutambua uongo na ukweli. Dc/afisa elimu moja kwa shule, madarasa na masomo zaidi ya 100?
 
Kuwatisha walimu, kuwaagiza maafisa elimu na Dc kwenda kufundisha ni kupoteza muda wa kutatua tatizo. Suluhu ya mgogoro wa walimu ni serikali ikubali kukaa na walimu ili kukubaliana kwa kile kinachowezekana na siyo vitisho kama wanavyofanya sasa. Wilaya moja ina Dc na afisa elimu wangapi? Je shule, madarasa na masomo yako mangapi, je Dc au afisa elimu atamudu? Au ni kupoteza muda tu. Kama hawa ndiyo viongozi tulio nao kazi tunayo. Maana yawezekana hapo ndiyo uwezo wao wa kufikiri unapoishia. Pole kwa watanzania.

Kwani wale madaktari waliosema watawaleta kutoka nje wameletwa? Sasa hivi maDc na maafisa elimu nao wawe waalimu? Kweli viongozi wetu wana utapia mlo wa fikra chanya!!!
 
Penye mgogoro wa kikazi soln ni kukaa na kujadiliana si vitisho au kutafuta shortcuts eti sijui maafisa elimu waende wafundishe hawatoshi na wengine hata wamesha sahahu kufundisha!
 
Waacheni waalimu wapambane na Polisi.
"WALIOMBA KAZI, WAKAPATA KAZI, WASIONE KAZI KUFANYA KAZI, WAKIONA KAZI KUFANYA KAZI, WAACHE KAZI WAONE KAZI"
 
Hata Mahakama yenyewe tumeshapoteza imani nayo, kwani imekubaliwa kutumiwa na Serikali. Kwanza Majaji na baadhi ya Mahakimu wanateuliwa na Mtu mmoja, what do you expect? Urais wa Kifalme Sio?
 
Back
Top Bottom