johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,840
- 141,765
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesema Waziri Mkuu, Majaliwa anaanza ziara ya siku mbili mkoani Mbeya.
Akiwa mkoani Mbeya Mhe. Majaliwa atafungua Jengo la Mama na Mtoto jijini Mbeya, atafungua hospitali iliyoahidiwa na Rais Magufuli wakati wa kampeni wilayani Rungwe na atafungua kituo cha pamoja cha forodha (One Stop Center) wilayani Kyela.
Aidha, Chalamila amemshukuru sana Rais Magufuli kwa kutimiza ahadi yake ya kujenga hospitali Wilayani Rungwe yenye thamani ya Tsh. 481 milioni.
Chanzo: Channel Ten
Maendeleo hayana vyama!
Akiwa mkoani Mbeya Mhe. Majaliwa atafungua Jengo la Mama na Mtoto jijini Mbeya, atafungua hospitali iliyoahidiwa na Rais Magufuli wakati wa kampeni wilayani Rungwe na atafungua kituo cha pamoja cha forodha (One Stop Center) wilayani Kyela.
Aidha, Chalamila amemshukuru sana Rais Magufuli kwa kutimiza ahadi yake ya kujenga hospitali Wilayani Rungwe yenye thamani ya Tsh. 481 milioni.
Chanzo: Channel Ten
Maendeleo hayana vyama!