Uchaguzi 2020 RC Chalamila: Nilikuwa nahesabu masaa tu kwa walioni-beep. Kwenye hizi chaguzi mtu asidhani 'atani-beep' alafu niache 'kumpigia'

Matangazo ya vituo yataanza kurushwa kidogo kidgo kila siku kadri vituo vinapomaliza kuhesabu. baada ya hapo kunakuwa na majumuisho. so itategemea kasi ya kuhesabu
Hapana. Hakuna kidogo kidogo katika kuhesabu. Nchi nzima kura zinahesabiwa wakati huo huo mmoja, na pote watakuwa wamekamilisha kuhesabu ikifikia saa mbili usiku hivi. Ni kura chache. Hakuna kituo kinachohesabu zaidi ya kura 500. Kuchelewa kupo katika kujumuisha, maana vituo ni vingi na viko mbalimbali kiasi cha kuhitaji muda kupata taarifa na kuzihakiki.
 
Sheria inasema uyu mkuu wa mkoa haruhusiwi ktk vituo vya kupigia kura, afanye tu kiherehere chake aone mahakama ikitengua matokeo dhidi ya ccm, tnamjua ye ni kada wa ccm
Huo mtego madc na marc wengi watauingia kwa sababu wengi wanafikiri kwa kutumia matumbo yao kisa ukada.
 
Atuambie wale vijana 150 atakaowavisha nguo za chadema na kuwapa kadi ili walete vurugu kwa kuwalipa mpango wake umebuma.
 
23 October 2020
Mbeya, Tanzania




RC Albert Chalamila asema jana niliwaona watu ofisi ya Mkurugenzi lakini nilikuwa nawahesabia masaa akina mama wale kabla ya kushughulikiwa kwa hatua kali ambazo wasingesahau.

Kuhusu kusimamia mchakato wa uchaguzi RC Albert Chalamila amesema uongozi wa mkoa umejipanga kuhakikisha uchaguzi wa 2020 unakuwa wa Haki na Huru.

Amewatoa wasiwasi wananchi wa mkoa wa Mbeya na jijini la Mbeya ipo shwari kabisa katika mitaa, kata, Halmashauri na wapiga kura wajitokeze kwa wingi kutimiza haki yao ya kikatiba amemalizia mkuu wa mkoa wa Mbeya Albert Chalamila alipokuwa anaongea wa vyombo vya habari.


Haijui Mbeya huyu!!! Atakumbia Mbeya huyu akileta ujinga wake. Malafyale hawajawaigi kuniangusha
 
Haijui Mbeya huyu!!! Atakumbia Mbeya huyu akileta ujinga wake. Malafyale hawajawaigi kuniangusha
Siyo awamu hii. Hata wakati Rais Magufuli anapanga kwenda Mbeya ulisema utopolo huo huo lakini Rais akaenda akapata mapokezi ambayo hayajawahi tokea! Kwahiyo wewe ni wakupuuzwa tu na hadithi zako.
 
Huyu ni mpuuzi na mpumbafu sana. Anatufanya sisi sote ni wajinga Kama yalivyo ma ccm. Hivi huyu hakumbuki aliyemteua alishawahi kutamani ashuke malaika azime mitandao??
 
Back
Top Bottom