RAZA: Magamba bado yapo CCM!

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Wednesday, 21 September 2011 20:19

Kizitto Noya

KADA wa CCM, Mohamed Raza, amehoji mantiki ya dhana ya 'kujivua gamba' kama baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi hawataki kuwajibika, wala chama kuwawajibisha.Akizungumza Dar es Salaam jana, Raza alisema ana shaka na umakini wa CCM kusimamia mambo yake, huku akihoji sababu zinazowafanya watuhumiwa wa ufisadi wang'ang'anie kuwapo ndani ya chama hicho tawala.

"Kuna maswali ya kujiuliza hapa, hivi kiburi hiki hawa wenzetu (watuhumiwa) wamekitoa wapi au ndiyo ile tabia ya mambo ya kujuana na kubebana kwa viongozi?" alihoji Raza na kuongeza:

“Tunaamini chama hakimwonei mtu kwa rangi wala kabila, kwa sababu hakuna mtu maarufu kuliko chama. Hivi kama kila unakopita watu wanakung'ong'a, kwa nini usijiondoe? Kuna watu leo wanashindwa kupita Manzese, Mbagala hata Kariakoo kwa aibu, kwa nini wasitoke?"

Alisema tuhuma za ufisadi zinazowakabili watuhumiwa hao, zinatosha kuwafanya wawajibike kama kweli wanakitakia mema chama, vinginevyo wanakifanya chama na Serikali yake vipoteze umaarufu kwa wananchi.
Raza ambaye hakuwataja kwa majina watuhumiwa hao wanaotakiwa kujivua gamba, alikigeukia chama chake cha CCM na kwamba, iwapo watendaji hawataacha unafiki, nchi itayumba.

"Hivi kweli CCM tunahitaji kusubiri wapinzani watuletee majina ya mafisadi? Hawajulikani au tunawalinda?" alihoji Raza ambaye alieleza kuwa urafiki na kujuana, ni mambo yanayokivuruga chama hicho.

Aliendelea: "Mabilioni ya fedha yanaibiwa, lakini sisi tunaishia kuunda tume kama siyo kujuana ni nini. Kulikuwa na haja gani ya kuunda tume kwa ajili ya kuchunguza wizi wa EPA ambao uko wazi na watuhumiwa wapo?

"Zimeshaundwa tume nyingi tu hapa. Hata kwenye chama kuna kamati ya Mwinyi ambayo majibu yake bado ni kitendawili...tabia hii ya kuunda tume halafu matokeo yake hayatangazwi haina msingi wowote zaidi ya kujuana.
"Kuna tume ya kuchunguza jinsi fedha za EPA zilivyoibwa, tume ya kuchunguza mikataba ya madini, lakini mpaka leo bado tunasubiri wapinzani wakatuibie matokeo yake waje kututangazia."

Katika hatua nyingine, Raza alizungumzia mchakato wa katiba mpya, akisema Wazanzibari wanataka kuwe na Miswada miwili; Muswada wa Wazanzibari na Muswada wa Watanganyika.

"Kumekuwa na mambo mengi watendaji wetu hawawi wakweli. Tunaupenda Muungano, lakini tunataka Watanganyika wasitulazimishe kwa kuwa hatukulazimishana kuungana. Katika umoja huu, tuheshimiane, tuvumiliane na tujadiliane," alisema Raza na kuongeza:

“Tusikubali kwenda kujadili Katiba mpya kama hakutakuwa na miswada miwili, vinginevyo Zanzibar itakwisha...The world is talking about peoples power (dunia inazungumzia nguvu ya umma), kama viongozi hawataki, wakae pembeni, wawaache wananchi wajadili masuala yao."

Raza alisema anaamini Katiba itakayopatikana baada ya kuwasilishwa miswada miwili bungeni, itakidhi matakwa ya wananchi wa Tanzania kuliko katiba itakayopatikana baada ya muswada wake kuwasilishwa na Serikali ya Muungano, ambayo kimsingi ni Serikali ya Tanganyika.

"Kuna kasoro nyingi kwenye katiba ya sasa, ambayo kama hatutakuwa makini kuzirekebisha kupitia mchakato sahihi wa mabadiliko ya katiba, zitaendelea kuwapo na kuwatafuna Watanzania na vizazi vyao,” alisema.

 
Nimefura hishwa sana na maneno yake' ila namwongezea jingine kuwa RA anatumika Igunga hvyo swala la kujivua gamba ni geresha tu! Kuhusu muungano na katiba yupo sahihi 100%
 
Yes katoa viji-point ila ukiangalia kwa jicho la karibu kuna mambo mawili hivi:-

(i) Magamba waliong'ang'ania: inanipa mashaka kwa yeye kuongelea hilo baada ya Rostam kujiuzulu na sio kabla yake na hata maelezo yake yanajaribu kum-exclude RA. Kuna hoja fulani iliyojificha au inayojaribu kujengwa hapa.

(ii) Muungano: kama kawaida ya wazanzibari hawaachi kulalamika juu ya muungano. (Raza) anataka kuwepo miswada miwili ya mchakato wa katiba mpya eti mmoja kwa ajili ya Zanzibar na mwingine wa upande wa pili kwa ajili ya kitu kilekile - KATIBA. Mbinu nyingine ya siri ya kuuvunja muungano kabla hata wananchi wenyewe hawajaamua kufanya hivyo.
 
[h=3]Magamba bado yapo CCM-Raza[/h]

Na Mwandishi Wetu

MFANYABIASHARA maarufu wa Zanzibar, Bw. Mohamed Raza amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kuwashinikiza makada na baadhi ya viongozi wake
wenye tuhuma mbalimbali za ufisadi kujiondoa ili kufanikisha falsafa ya kujivua gamba.

Pia mfanyabiashara huyo ameonya kuwa endepo hatua hiyo iliyoanzishwa na Halmashauri Kuu wa Taifa ya chama hicho haitatekelezwa kwa ukamilifu hali hiyo itakiumiza chama hicho.

Bw. Raza aliyewahi kuwa Mshauri wa Rais wa Zanziibar wa masuala ya michezo, alisema hayo jana alipotembelea ofisi za gazeti hili na kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu chama hicho, serikali na hatima ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

"Kuhusu kujivua gamba, viongozi tuwe wakweli. Kila anayetuhumiwa kwa ufisadi ajiondoe, hapa hakuna nafasi ya mahakama," alisema.

Alipoulizwa ni akina nani wanaotakiwa kujiondoa, Bw. Raza alisema: "Wako wengi ndani ya chama na wanajijua, maana wanatajwa kila siku na magazeti wanayasoma. Wajiondoe au waondolewe, huo ndio ustaraabu," alisema.

Alisema watuhumiwa hao wanatakiwa kutambua kuwa wao si maarufu kuliko chama. "Umaarufu ni wa chama sio wa mtu. Ndani ya chama hakuna bwana, wakiache chama kiendelee."

Kuhusu tume za rais

Bw. Raza aligusia wingi wa tume zinazoundwa na marais wa muungano na wa Zanzibar akidokeza kuwa matokeo yake hayafanyiwi kazi licha ya kutumia zaidi ya sh bilioni 10 za walipa kodi tangu uhuru.

Kutokana na hali hiyo, Bw. Raza alipendekeza katika kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika ripoti za tume hizo ziwekwe wazi ili wananchi wazisome na kujua kilichomo.

"Imekuwa kiongozi anaunda tume, inaleta taarifa, akifungua anakuta yumo ndugu wake, yumo jamaa yake, yumo swaiba wake anaamua kuachana nayo na kuifungia. Watumishi wamekuwa si waaminifu, urafiki wao, undugu wao na uswahiba wao unaididimiza nchi," alisema.

Kauli ya Muungano

Akizungumzia muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Bw. Raza alisema wakati mjadala wa Katiba Mpya unaendelea, Wazanzibar waruhusiwe kwenda kama nchi kupeleka hoja zao sambamba na zile za Serikali ya Muungano ili kumaliza kile alichosema ni kero za zaidi ya miaka 40.

"Tusilazimishane, tuheshimiane na kama watendaji waliopewa kazi hii wameshindwa wajiuzulu," alisema Bw. Raza huku akiomba Rais Jakaya Kikwete amteue kuwa mbunge kwa mwezi mmoja (bila mshahara wala posho) ili aongoze Wazanzibari wakati wa mjadala wa katiba mpya kwa maslahi ya nchi yake.

Alisema kipindi hiki cha mjadala wa katiba ni muhimu kwa Zanzibar kuhakikisha kero za muungano zinamalizwa vinginevyo fursa hiyo ikipotea hawataipata tena.
 
duuh big up Raza,huwa na mkubali kwa kuwa huwa anaeleza hisia zake kwa uwazi!ni miongon mwa wafanyabiashara wachache wanaoweza kuikosoa CCM hadharani
 
Back
Top Bottom