Rayvanny aonesha uelekeo wa mapenzi yake baada ya kumalizana na Fayhma

Rosh Hashannah

JF-Expert Member
Sep 13, 2017
3,415
2,042
Staa wa ngoma ‘Mbeleko’ Rayvanny aliyeko Marekani kikazi, baada ya kurushiana maneno yaliyoashiria kuwa amekosana kimahusiano na mama wa mtoto wake, ‘Fayhma’ sasa ameonesha kuelekeza mapenzi mazito kwa kinachoweza kubaki kama kumbukumbu isiyobadilika kama hawatamaliza tofauti zao kwa suluhu ya wawili hao kurudiana.

Akiwa mjini Washington, Rayvanny kupitia ukurasa wake wa Instagram alipost picha ya mwanae, Jaydany sambamba na maneno yayoambatana kwenye picha hiyo yaliyozungumza kuutamani ukaribu wake na mtoto wake huyo. Bila shaka mapenzi ya mzazi na mtoto yamechangia kumsukuma Rayvanny aoneshe hisia hizo.

Katika hilo la wawili hao kutokauwa katika hali nzuri ya kimahusiano, inahesabika kuwa ni miezi isiyopungua miezi 7 tangu wawili hao walipokaribisha mtoto wao huyo wa kwanza kwakuwa taarifa za wawili hao kupata mtoto zilisambaa tarehe 19 mwezi Aprili mwaka huu.
 
Sijaelewa asee
d024a072573e7a1e774f5fc7f0bdd078.jpg

16cfbd58b08185061081951fcbd25b83.jpg
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom