RAV4 KWA 3,650USD( Gari kwa Mtanzania wa kawaida)

punguzo

Member
Jul 9, 2011
51
6
Wakuu, bado ni mpya kama ionekanavyo kwenye Pics,
Details zake,

TOYOTARAV4 1997

· Year:1997
· Displacement (cc):2000
· Steering Wheel:RHD
· Transmission (Gear):AT
· Fuel:Petrol
· Color:Wine
· Door: 3

Bei : 3,650USD

TAFADHALI KAMA UTAHITAJI NI PM.
 
Ingia BE FoRWarD uone bei ilivyo chini CIF...ni za 1998.

kaka, ukienda kwenye hiyo link yako, utagundua gharama za kututua na kutuma ni 3000usd, na wao wanastock za zamani ndo maana sasa wanafanya sales, pia hujui hali ya gari lenyewe, ila hii mimi nimetoka kuinunua na najua condition yake ninzuri sana kama uionavyo kwenye picha!
 
Gari yenye umri wa miaka zaidi ya 14 bei haiwezi ikalingana na gari ya miaka mitano..Mileage itakuwa juu sana...Kwa ufupi bei ni kubwa mno kulingana na umri wa gari.
 
... hivi "Mtanzania wa kawaida" ndio mtu wa namna gani?

Ana kipato cha angalau kiasi gani kwa mwezi? ... maana siku hizi tunasikia sana watu wanasema eti kwa Mtanzania wa kawaida! ... sasa mimi bado sijajua ni vigezo gani vinavyotumika
 
Najua, Watanzania wengi ni wazuri wa kulialia, kulalamika na kutafuta visababu vidodo vidogo ili wapunguziwe bei au wauziwe kwa bei ya chini sana( Mwisho wanaishia kununua vitu fake).

Pia imekuwa kama hulka yetu kudharau biashara za wenzetu, kuzikandia, kuponda, kusengenya na kuzidharirisha. Tumekuwa na tabia ya kushusha hadhi na bei ya bidhaa/biashara za wenzetu huku tukijifanya tunajua mazingira na mzunguko wa biashara hiyo wakati hatujui. Tunasahau ya kuwa tunaharibu biashara za watu mwingine (hii husababisha biashara nyingi kufa).

Kwa kifupi, Bei ya bidhaa hutokana na mazingira yanayoizunguka biashara hiyo, ubora na hadhi ya bidhaa, upatikanaji, ukubwa wa biashara/ kampuni, usafirishaji, umuhimu wa bidhaa, kodi, malengo ya muuzaji na mambo mengine mengi.

Kuhusu bei za magari yatokayo Japan, Siku za mwanzo watu wengi walikuwa wanaship magari ya wizi hivyo ilifanya kushusha bei halisi ya magari.

Pia kunawafanya biashara wengi( Hasa wakubwa) ambao wanakwepa kodi au wanatumia exemption fake, hawa wanasababisha kushuka kwa bei halisi ya magari , pia wanachangia kushuka kwa pato la serikali kwa kukwepa kodi.

Kutokana na kuyumba kwa uchumi wa dunia, Wajapan wengi walikosa kazi za kuajiliwa na kuamua kujiajiri katika sekta Magari used. Ikumbukwe ya kuwa Wajapan wengi wanauwezo wa kupata magari ya bure (Dumping cars) au magari ya bei nafuu yenye migogoro au yaliyopata ajari kwa bei ya chini kabisa hivyo kuwafanya wawe kwenye nafasi nzuri ya kuuza kwa bei ya chini.

Siku za nyuma, ambapo magari yalikuwa bei rahisi kuna baadhi ya makampuni makubwa ya kijapan yalinunua magari mengi na kuyaweka kwenye stock. Haya makampuni kwa sasa wanayauza haya magari kwa bei ya chini mno, ndo maana magari ya miaka ya nyuma ni bei rahisi sana kulinganisha na magari ya miaka ya hivi karibuni.

Kuna magari yaliyo athirika na mafuriko ya tsunami, active radiator, Nuclear, haya huuzwa kwa bei ya chini Mno na madhara yake kiafya ni makubwa mno ( KANSA NI ZA KUFIKIA). Pia injini zake ndo kama zinavyo waharibikia kila siku.

Kuna magari yanaitwa accedental/broken cars haya ni magari yaliyopata ajari, damped, damaged, yenye matatizo ya injini, na matatizo mengine mbalimbali na kuwa solved. Haya magari bei yake ni nafuu sana. Ukweli ni kwamba ongezeko la haya magari, limesababisha ongezeko la kushamili kwa biashara ya spare parts. Wabongo wengi wamenunua Magari haya na hata kabla ya mwaka mmoja kuisha wanajikuta wameingia katika biashara ya manunuzi ya spare parts. wanakwepa bei halisi ya magari au wanakwepa tofauti ya USD 1,000/ lakini ukichambua gharama za kufix hilo gari miaka miwili baada ya kulinunua utakuta ni sawa na gharama za kununua magari mawili kwa bei inayokubarika. Na ndio maana magari mengi bongo baada ya miaka miwili mitatu utayakuta juu ya mawe.

Anyway, kuna mazingira mengi yanayofanya magari ya japan kuwa bei chini na juu, unatakiwa kuwa makini, na kunamambo mengi sana yakujadili katika biashara hii, kuliko mtu kukurupuka na kuanza kushambulia biashara za watu hasa wajasiriamali wadogo wadogo.

Lakini pia mwisho wa yote, wewe kama Mtanzania unayependa maendeleo na usiokwisha kuilaumu serikali ya CCM au unayetaka Chadema ilete mabadiliko, Unatakiwa kununua magari/ bidhaa kutoka kwenye makampuni ya watanzania wazalendo wenzako na sio kusujudu makampuni ya kigeni. Ukweli ni kwamba ukinunua magari kwenye kampuni ya kijapan utakuwa umesaidia kukuza uchumi wa taifa la japan, na kuwaongezaa ajira na kipato, na ukinunua kutoka kwenye kampuni la mzalendo mwezako utakuwa umesaidia kuongeza ajira na kipato kwa vijana wetu, umesaidia kuongeza pato la serikali kwa kupata kodi, utakuwa umesaidia maendeleo ya nchi na jamii yetu kwa sababu wamiliki wengi wa haya makampuni hutuma remmitances nyumbani, ambazo zinasaidia familia, zinajenga majumba, zinalipia karo na huduma za afya, pia wamiliki wengi wa haya makambuni wanatabia ya kuwekeza katika shughuri balimbali za kijamii na kimaendeleo.


Nina mengi sana ya kusema ila kwa sasa aksanteni !
 
kaka, ukienda kwenye hiyo link yako, utagundua gharama za kututua na kutuma ni 3000usd, na wao wanastock za zamani ndo maana sasa wanafanya sales, pia hujui hali ya gari lenyewe, ila hii mimi nimetoka kuinunua na najua condition yake ninzuri sana kama uionavyo kwenye picha!

Mtu atajuaje conditipn ya gari kwa kuangalia picha mkuu?,linaweza kuwa na mwonekano mzuri wa nje lakini kumbe halitembei.
 
Aah kumbe mlimuudhi huyu mfanya biashara ndio akaenda kuanzisha uzi maalum wa kuponda wabongo, nb mtanzania wa kawaida kipato chake ni chini ya dollar 2 hadi 1 kwa siku,mimi ni mfano sahihi,je niwekeze kiasi gani kila siku ili niweze kununua gari yako?please have a little mercy kwa mtanzania wa kawaida,mtanzania wa kawaida anafanya shopping ya breakfast mlimani city?
 
Mtanzania halisi halipi bei kwa Dollar.... hicho kigari cha kupidisha migongo watu nani anataka? kawauzie Mombasa
 
Kwa huo mwaka wa gari bei hiyo ni kubwa mno?? 1997?? Acha kabisa bei kubwa sana hiyo.........
 
Najua, Watanzania wengi ni wazuri wa kulialia, kulalamika na kutafuta visababu vidodo vidogo ili wapunguziwe bei au wauziwe kwa bei ya chini sana( Mwisho wanaishia kununua vitu fake).

Unatakiwa kununua magari/ bidhaa kutoka kwenye makampuni ya watanzania wazalendo wenzako na sio kusujudu makampuni ya kigeni. Ukweli ni kwamba ukinunua magari kwenye kampuni ya kijapan utakuwa umesaidia kukuza uchumi wa taifa la japan, na kuwaongezaa ajira na kipato, na ukinunua kutoka kwenye kampuni la mzalendo mwezako utakuwa umesaidia kuongeza ajira na kipato kwa vijana wetu, umesaidia kuongeza pato la serikali kwa kupata kodi, utakuwa umesaidia maendeleo ya nchi na jamii yetu kwa sababu wamiliki wengi wa haya makampuni hutuma remmitances nyumbani, ambazo zinasaidia familia, zinajenga majumba, zinalipia karo na huduma za afya, pia wamiliki wengi wa haya makambuni wanatabia ya kuwekeza katika shughuri balimbali za kijamii na kimaendeleo.

Nina mengi sana ya kusema ila kwa sasa aksanteni !

Mwisho wa hadithi ni ile ile ulio anza nayo, "kulalamika lalamika, kulialia na kutafuta vijisababu..." kwa maana hakuna gari linalitengenezwa Tanzania linalotumiwa na watanzania kibiashara au kibinafsi, mwisho wa siku pesa inarudi Japani! Kununua kwa wabongo ni kujiongezea gharama ya bure!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom