Ericus Kimasha
JF-Expert Member
- Oct 27, 2006
- 488
- 470
Napenda kuweka sawa Taarifa ya awali juu ya Taarifa ya msiba na ratiba ya mazishi ya Dokta Kyaruzi kama ilivyoletwa hapa Jamvini awali na Ndg. Pasco wa JF
Mazishi ya Dr. Vedasto Kyaruzi aliyefariki tarehe 20/05/2012 saa 1:20 Jioni katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera, yatafanyika Jumamosi, tarehe 26/05/2012 saa tisa alasiri Missenye-Nyabianga, Kyaka katika shamba lake.
Mazishi haya yatanguliwa na misa ya kuaga mwili hapo kesho Ijumaa, tarehe 25/05/2012 kuanzia saa saba (7:00) mchana. Misa hii itafanyika nyumbani kwa Marehemu Kashai-Matopeni. Baada ya misa safari ya kuelekea Kyaka kwa maziko itaanza. Mwili wa marehemu utalala shambani kwa marehemu Missenye-Nyabianga
Umma unakaribishwa kujiunga na familia kwa sala, hali na mali katika kipindi hiki kizito.
Bwana alitoa, na Bwana ametwaa. Jina la Bwana na lihimidiwe.
Kwa Taarifa zaidi wasiliana na:
Fredy Nshunju
M/Kiti Kamati ya Habari
Na. ya Simu: 0767404113
Evarista Rugeiyamu
Katibu-Kamati ya Habari
Na. ya Simu: 0784888091