Rastafarians ndio diaspora pekee wanaomwakilisha Mwafrika popote walipo

Quinine Mwitu

JF-Expert Member
Oct 19, 2014
5,266
5,663
Wasalam,

Nimeona leo niwasifie hawa watu jamii ya rastafarian. Ni watu amabao walio wengi wana uzalendo wa kweli wa kulipenda Bara la Afrika na watu wao kwa mapenzi makubwa kabisa.

Ukitaja jamii ambayo huwa wanaichukia biashara ya utumwa mpaka leo, biashara iliyosababidha maumivu makubwa kwa watu wa bara la Afrika, basi huwezi kuacha kuwataja watu jamii ya rastafarian na mtu yoyote aliyeutukuza na kuwatukuza waafrika huwa wanampa kipaumbele kikubwa sana.

Mfano mpaka leo wanamchukulia Marcus Gavey kama Mtume wao kwa kuwa tu alifanya juhudi kubwa za kuwarudisha waamerika weusi kwenye bara lao, Afrika.

Na wanamchukia sana Mwafrika aliyeko ugenini ambaye hataki kutambua Afrika kama chimbuko lake. Wana msemo wao kuwa if you are a black man, wherever you are Africa is home.

Wameingia kwenye Mgogoro wa kudumu na Mapapa wote, point yao wanadai kama papa alikuwa muadilifu na muungwana asingeamuru jeshi la Italy kwenda kuivamia nchi ya Ethiopia. Walio wengi wanaamini kizazi cha Haile Selasie ndio kizazi cha mitume wote kwa kuwa Haille Selasie alikuwa mjukuu wa Mfalme Daudi, kwahiyo wao wanaamini hata Yesu Kristo alikuwa Mweusi ni watu weupe tu wameipotosha Historia na kumfanya yesu kama mzungu lakini si kweli.


Watu kama Akina Suni Ali, Walter Rodney, Martin Luther na waafrika waliofanya vyema miaka hiyo hadi sasa katika kutetea utu wa mtu mweusi bila kujali rangi zao nk, maana huwa wanamsemo wao mmoja wanasema you can have a white face with a black heart and viceversa. Mpaka leo, kwao bado unabaki shujaa wa mtu mweusi haijalishi rangi yako.

Yawezekana wakawa na Mapungufu, ila hili la uzalendo na mapenzi kwa Afrika huwa linanifanya niwakubali sana hawa watu na mtu yoyote atakayehujumu maisha ya mtu mweusi kwao ni msaliti mkubwa ''Babylon''.
 
Marcus Garvey sindie alie sema if all black will back into Africa I will be last of them yani alikuwa hapendi kurudi Darkland kwanini atukuzwe?
 
Marcus Garvey sindie alie sema if all black will back into Africa I will be last of them yani alikuwa hapendi kurudi Darkland kwanini atukuzwe?
sidhani kama marcus aliongea maneno hayo,na pia kumekua na mbinu nyingi za kumchafua Marcus,wapo waliosema hakua mweusi ila alikuwa muhindi,Marcus ndie aliyesimamia mpango mzima wa blacks kurudi Afrika
 
Marasta mbele tu, hawa Wa bongo wote wasaka K za wazungu. Hivi hujiulizi kwanini wengi wao wameoa/wanawapenzi wazungu tu? Km kweli ni wazalendo Wa ki Africa wangekua wanaoa wa Africa
 
Marasta mbele tu, hawa Wa bongo wote wasaka K za wazungu. Hivi hujiulizi kwanini wengi wao wameoa/wanawapenzi wazungu tu? Km kweli ni wazalendo Wa ki Africa wangekua wanaoa wa Africa
kila sehem matapeli wapo,na ndio maana wazungu wanaingia king kwa kua wanajua rasta wa kweli ni mtu wa namna gani,sio muongo,ni mkweli wa roho na nafsi ila ndio hvo wanatapeliwa
 
Marcus Garvey sindie alie sema if all black will back into Africa I will be last of them yani alikuwa hapendi kurudi Darkland kwanini atukuzwe?
hapana huyo alikuwa ni mtu mweusi wa kwanza kuwa na PhD Bwana W.E.Dubois

Marcus Garvey yeye alisema "emancipate your self from mental slavery non but your self can free your mind"

hii ndiyo sababu The king Robert Nesta Marley [HASHTAG]#Bob[/HASHTAG] Marley katika wimbo wake wa mwisho kabla ya umauti aliiweka hiyo nukuu ya Garvey huo wimbo unafahamika kama Redemption song
 
Je wajua kwanini Hatupendi kuitwa rastafarians ilhali tunapenda kujulikana kama rastafaris

jibu ni kuwa hiyo #an inawakilisha system mfano [HASHTAG]#Babylonians[/HASHTAG] na kwakuwa Babylonians ni maadui wakubwa kwetu sababu mfumo wa babeli ni kandamizi ndomaana ili kujitofautisha inakuwa [HASHTAG]#rastafaris[/HASHTAG]


Jah will never give bald headed power never ever raaaaaah!
 
hapana huyo alikuwa ni mtu mweusi wa kwanza kuwa na PhD Bwana W.E.Dubois

Marcus Garvey yeye alisema "emancipate your self from mental slavery non but your self can free your mind"

hii ndiyo sababu The king Robert Nesta Marley [HASHTAG]#Bob[/HASHTAG] Marley katika wimbo wake wa mwisho kabla ya umauti aliiweka hiyo nukuu ya Garvey huo wimbo unafahamika kama Redemption song
Well said...., na pia ni huyo huyo Marcus Garvey akiwa na wenzie kadhaa waliokuwa mstari wa mbele sana (pioneers) wa "THE BACK TO AFRICA MOVEMENT" they had the sense & the feeling to come back and stay in their mother land Africa baada ya maswaibu yote na karaha zote walizopata huko kwa hao jamaa wenye ngozi tofauti na nyeusi.
And moreover sasa hivi wenzetu hawa wenye rangi tofauti na sisi wanajitahidi kupotosha historia kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano kama mtu umesoma kitabu cha Walter Roodney "HOW EUROPE UNDER~DEVELOPED AFRICA" ile original version utagundua kuna tofauti kubwa na hivi Revised Editions vinavyopatikana madukani kwa sana sasa hivi. Wamejaribu sana kunyofoa baadhi ya mambo
 
Je wajua kwanini Hatupendi kuitwa rastafarians ilhali tunapenda kujulikana kama rastafaris

jibu ni kuwa hiyo #an inawakilisha system mfano [HASHTAG]#Babylonians[/HASHTAG] na kwakuwa Babylonians ni maadui wakubwa kwetu sababu mfumo wa babeli ni kandamizi ndomaana ili kujitofautisha inakuwa [HASHTAG]#rastafaris[/HASHTAG]


Jah will never give bald headed power never ever raaaaaah!
nimepata elimu mkuu
 
Cha kusikitisha ni kuwa walio haribu ile project ni baadhi blacks people walioshirikiana na FBI meli zikanunuliwa kwa garama kubwa huku zikiwa ni chakavu na viwango hafifu siri za Back to Africa movement zikavujishwa na baadhi ya watu weusi waliokubali kuwa vibaraka kwa nguruwe weupe wenye vipara mwishowe Garvey anafungwa miaka nafikiri mitano jela all in all Garvey anasimama kwa kielelezo cha John The Babtist hiyo ndiyo sababu tunamwita prophet kwakuwa twautambua mchango wake katika athira za mtu mweusi
 
Well said...., na pia ni huyo huyo Marcus Garvey akiwa na wenzie kadhaa waliokuwa mstari wa mbele sana (pioneers) wa "THE BACK TO AFRICA MOVEMENT" they had the sense & the feeling to come back and stay in their mother land Africa baada ya maswaibu yote na karaha zote walizopata huko kwa hao jamaa wenye ngozi tofauti na nyeusi.
And moreover sasa hivi wenzetu hawa wenye rangi tofauti na sisi wanajitahidi kupotosha historia kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano kama mtu umesoma kitabu cha Walter Roodney "HOW EUROPE UNDER~DEVELOPED AFRICA" ile original version utagundua kuna tofauti kubwa na hivi Revised Editions vinavyopatikana madukani kwa sana sasa hivi. Wamejaribu sana kunyofoa baadhi ya mambo
 

Attachments

  • HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA.pdf
    1 MB · Views: 31
  • before-the-mayflower-1-3.pdf
    2.2 MB · Views: 64
ukisoma hivyo9 vitabu utagundua jinsi gani hawa jamaa ni mabingwa wa kupotosha histo9ria,viwil vimekataa ni vikubwa sana,ni Destruction of black civilization na They came before columbus
 
ukisoma hivyo9 vitabu utagundua jinsi gani hawa jamaa ni mabingwa wa kupotosha histo9ria,viwil vimekataa ni vikubwa sana,ni Destruction of black civilization na They came before columbus
Thanx mkuu infact kuna kama mchezo flani hivi wanafanya hawataki generation ya sasa ijue ukweli wa mambo & thats why ukisoma e~books based on history kuna ladha flani utakosa
 
Thanx mkuu infact kuna kama mchezo flani hivi wanafanya hawataki generation ya sasa ijue ukweli wa mambo & thats why ukisoma e~books based on history kuna ladha flani utakosa
ni kweli mkuu hilo sikatai kabisa,editing nyingi
 
Thanx mkuu infact kuna kama mchezo flani hivi wanafanya hawataki generation ya sasa ijue ukweli wa mambo & thats why ukisoma e~books based on history kuna ladha flani utakosa
ila hakuna kitabu nilichokisoma na kufarijika kama they came before columbus,yaani tunakosea kuamini kua slave trade ndio chanzo pekee cha mtu mweusi kufika Amerika,aisee waafrika walianza kuitembea hii dunia hata kabla ya wazungu,na pia hata wao walimilik watumwa tena wa rangi zote,Mansa Musa tajiri mkubwa afrika anayetikisa mpaka leo utajiri wake ,alikuwa akienda kuhiji maka soko la madini ninaporomoka kabisa kwa wingi wa dhahabu aliyoenda nayo,kuna mengi sana ya mtu mweusi ya kufurahishs na kuuzunisha
 
Back
Top Bottom