Rasmi: Ukimfumania mara 490 ruksa kutoa talaka

clion dismas

Senior Member
Aug 6, 2017
185
170
Wanabodi

Kumekuwa na ongezeko la hali ya juu ya kutalikiana au kutoa talaka kwa wanandoa eidha kwa kujua au kutokujua madhara yake baadaye.

talaka.jpg


Kwa ufupi kabisa, MUNGU ANACHUKIZWA SANA NA WANANDOA KUTALIKIANA AU KUACHANA.

images.jpeg



Hebu tuone mungu anasema nini:-

Mwanzo 2:24
"Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja."

Malaki 2:15-16
"...Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema BWANA, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema BWANA wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana."

Mathayo 19:5-7
"...akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe."

HIVI, KWELI WAWILI HAO WALIOKUA MWILI MMOJA BAADA YA KUUNGANISHWA, NI NANI AWEZAYE KUWATENGANISHA? HAYUPO, NARUDIA, HAYUPO HAPA CHINI YA JUA WALA JUU YA JUA ISIPOKUA UMAUTI TUU. KWA WALE WALIOSOMA KEMIA WATAELEWA, KUNA NJIA NYINGI ZA KUTENGANISH VITU LAKINI NJIA YA KUTENGANISHA MTU NA PUMZI YAKE NI IPI KAMA SIYO KIFO TUU?

Sasaje, ni nini kilichopelekea hadi MUSA kuruhusu watu kutalikiana??
( NI UGUMU WA MIOYO YAO)

Mungu anapowaambia mafarisayo ni "ugumu wa mioyo yao anamaanisha hawakuwa wamempokea yesu kama mwokozi wa maisha yao na sheria kuu ya upendo haikuwa mioyoni mwao na kiashiria kikubwa kilikuwa ni hiki:-

Galatia 5:19-22
"Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Marko 10:2-12 na mathayo 5:31-32

"Akaondoka huko akafika mipakani mwa Uyahudi, na ng’ambo ya Yordani; makutano mengi wakakutanika tena wakamwendea; akawafundisha tena kama alivyozoea. Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamwuliza, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe? Huku wakimjaribu. Naye akajibu, akawaambia, Musa aliwaamuru nini? Wakasema, Musa alitoa ruhusa kuandika hati ya talaka na kumwacha. Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe. Hata nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo. Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake; na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini."

Mathayo5:31-32( MUNGU AMAANISHA NINI HAPA? ISIPOKUWA UASHERATI?)

31Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; 32lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

Ikumbukwe, hakuna amri kubwa wala amri ndogo katika amri za Mungu. Mungu anaposema isipokuwa uasherati.

Je, uasherati ni nini? NKJV INASEMA " SEXUAL IMMORALITY". Kifupi ni pale unapofanya ngono na mtu ambaye hamjafungamanishwa naye, yaweza kuwa kiroho au kimwili.

Lakini, bwana asema, ijapo kua dhambi zako ni nyekundu kama damu nitazifanya nyeupe kama theluji. Pia bwana Mungu asema tusamehe ili tusamehewe pia sisi makosa yetu. Je, kuna mtu msafi awezaye kumnyooshea kidole mwenzake? Kabla ya kujisema wewe ni msafi, jilinganishe na Mungu ndio ujue usafi ulionao.

Mwisho wa siku, bwana asema katika mathayo 18:22

" Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini."

Yaani, ikimshika anafanya ngono na mtu tifauti na wewe mme/mke wa halali akaomba samahani na akajutia kosa lake huna budi kumsamehe, akifanya hivyo tena jioni ma akakiri kwamba kafanya na akajuta huna budi kumsamehe. Yaani hata kwa siku afanye zaidi ya mara 5 na kila muda akakuomba msamaha hina budi kumsamehe. Ikumbukwe, pale unapomsamehe, unasahau. Kwaiyo akikosea tena unaanza kuhesabu upya mpaka zifike mara 490 basi mtaliki.

Ila kwasababu ya mahonjwa mengi, tizingatie afya na taratibu zote zitakazofanya tusipatwe maradhi.

"HII NDIYO GHARAMA YA UKRISTO, SAMEHE ILI MUNGU AKUSAMEHE NA URITHI UFALME WAKE".

Zaidi
Shetani akiwatawala mkashindwa kuishi pamoja, mkiachana basi kila mmoja abaki vivyo hivyo bila kuoa au kuolewa kwa maana akifanya hivyo yeye ufanya UZINZI na wazinzi mwisho wao ni "moto wa jehenam".

Rejea

Biblia:union version
:king jamez version
Mahubiri ya dodoma: uzoefu wa nguvu ya mungu( somo la kaya na familia na mama Urio) kupitia Morning star radio, hope channel tv, star tv na rock fm mbeya. Kila siku kuanzia saa 12 jioni hadi saa 2 usiku viwanja vya dodoma kati.

Barikiwa.
 
Hahaha! Uo si mpango wa Mungu ndugu. Vijana wengi wanaingia ndoani bila ya kuwa na sababu za msingi, so inabidi watu wakomae kiakili na kiimani kabla ya kuingia huko.
siku hizi hakuna hio unakuta baba zima kama marehemu mengi halikukomaa akiri likaoa stahiki yetu vijanauje kusema vijana hawajakomaa akiri nakataa hii main point KAMA UNAHISI UNAWEZA KUFUGA MTU(mwanamke) OA KWISHA
 
Mke wa ujanani ni yupi?
Wanabodi

Kumekuwa na ongezeko la hali ya juu ya kutalikiana au kutoa talaka kwa wanandoa eidha kwa kujua au kutokujua madhara yake baadaye.

View attachment 1099121

Kwa ufupi kabisa, MUNGU ANACHUKIZWA SANA NA WANANDOA KUTALIKIANA AU KUACHANA.

View attachment 1099116


Hebu tuone mungu anasema nini:-

Mwanzo 2:24
"Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja."

Malaki 2:15-16
"...Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema BWANA, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema BWANA wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana."

Mathayo 19:5-7
"...akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe."

HIVI, KWELI WAWILI HAO WALIOKUA MWILI MMOJA BAADA YA KUUNGANISHWA, NI NANI AWEZAYE KUWATENGANISHA? HAYUPO, NARUDIA, HAYUPO HAPA CHINI YA JUA WALA JUU YA JUA ISIPOKUA UMAUTI TUU. KWA WALE WALIOSOMA KEMIA WATAELEWA, KUNA NJIA NYINGI ZA KUTENGANISH VITU LAKINI NJIA YA KUTENGANISHA MTU NA PUMZI YAKE NI IPI KAMA SIYO KIFO TUU?

Sasaje, ni nini kilichopelekea hadi MUSA kuruhusu watu kutalikiana??
( NI UGUMU WA MIOYO YAO)

Mungu anapowaambia mafarisayo ni "ugumu wa mioyo yao anamaanisha hawakuwa wamempokea yesu kama mwokozi wa maisha yao na sheria kuu ya upendo haikuwa mioyoni mwao na kiashiria kikubwa kilikuwa ni hiki:-

Galatia 5:19-22
"Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Marko 10:2-12 na mathayo 5:31-32

"Akaondoka huko akafika mipakani mwa Uyahudi, na ng’ambo ya Yordani; makutano mengi wakakutanika tena wakamwendea; akawafundisha tena kama alivyozoea. Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamwuliza, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe? Huku wakimjaribu. Naye akajibu, akawaambia, Musa aliwaamuru nini? Wakasema, Musa alitoa ruhusa kuandika hati ya talaka na kumwacha. Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe. Hata nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo. Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake; na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini."

Mathayo5:31-32( MUNGU AMAANISHA NINI HAPA? ISIPOKUWA UASHERATI?)

31Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; 32lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

Ikumbukwe, hakuna amri kubwa wala amri ndogo katika amri za Mungu. Mungu anaposema isipokuwa uasherati.

Je, uasherati ni nini? NKJV INASEMA " SEXUAL IMMORALITY". Kifupi ni pale unapofanya ngono na mtu ambaye hamjafungamanishwa naye, yaweza kuwa kiroho au kimwili.

Lakini, bwana asema, ijapo kua dhambi zako ni nyekundu kama damu nitazifanya nyeupe kama theluji. Pia bwana Mungu asema tusamehe ili tusamehewe pia sisi makosa yetu. Je, kuna mtu msafi awezaye kumnyooshea kidole mwenzake? Kabla ya kujisema wewe ni msafi, jilinganishe na Mungu ndio ujue usafi ulionao.

Mwisho wa siku, bwana asema katika mathayo 18:22

" Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini."

Yaani, ikimshika anafanya ngono na mtu tifauti na wewe mme/mke wa halali akaomba samahani na akajutia kosa lake huna budi kumsamehe, akifanya hivyo tena jioni ma akakiri kwamba kafanya na akajuta huna budi kumsamehe. Yaani hata kwa siku afanye zaidi ya mara 5 na kila muda akakuomba msamaha hina budi kumsamehe. Ikumbukwe, pale unapomsamehe, unasahau. Kwaiyo akikosea tena unaanza kuhesabu upya mpaka zifike mara 490 basi mtaliki.

Ila kwasababu ya mahonjwa mengi, tizingatie afya na taratibu zote zitakazofanya tusipatwe maradhi.

"HII NDIYO GHARAMA YA UKRISTO, SAMEHE ILI MUNGU AKUSAMEHE NA URITHI UFALME WAKE".

Zaidi
Shetani akiwatawala mkashindwa kuishi pamoja, mkiachana basi kila mmoja abaki vivyo hivyo bila kuoa au kuolewa kwa maana akifanya hivyo yeye ufanya UZINZI na wazinzi mwisho wao ni "moto wa jehenam".

Rejea

Biblia:union version
:king jamez version
Mahubiri ya dodoma: uzoefu wa nguvu ya mungu( somo la kaya na familia na mama Urio) kupitia Morning star radio, hope channel tv, star tv na rock fm mbeya. Kila siku kuanzia saa 12 jioni hadi saa 2 usiku viwanja vya dodoma kati.

Barikiwa.
 
Umeelezea vizuri sana but jitahidi kwenye uandishi usichanganye Yesu na yesu, Mungu na mungu. Mungu anachukia kuachana
 
Labda kama umemfunga application ya android papuch tracker kwenye.Kwa wanaume kamilika hatutoi talaka ila tuna mpunish na gifts za nguvu then yule fala wake ana shika ukuta akiwa anaona.Tlaka sio suluhisho ni kuwapa uwanja wasasambuane.
 
siku hizi hakuna hio unakuta baba zima kama marehemu mengi halikukomaa akiri likaoa stahiki yetu vijanauje kusema vijana hawajakomaa akiri nakataa hii main point KAMA UNAHISI UNAWEZA KUFUGA MTU(mwanamke) OA KWISHA

Aseeee! Hapa ndio siku 3 mmechokana na kila mtu anatafuta njia yake. Huu ndio ugumu wa mioyo. Tumpe nafasi Mungu jamani. Wana wa kike bila kua na akili timamu ya uongozi wa Mungu, tutaingilia mlango wa "exit".
 
Mara zote hizo..yupo peke ake duniani?

Hadi umempenda na kumuweka ndani ni matarajio ya wanajamii wote kwamba yule ndiye ulimuona ni msichana kati ya wasichana, mrembo kati ya warembo na wengine wote muda ule walionekana kama wanaume. Yaani hamkuwa na itofauti wa jinsi pamoja nao.
 
Mke wa ujanani ni yupi?

Ni yule ambaye ulivutiwa naye angali bado anachanua, bado chipukizi na bado anasababisha hulali bila kumjulia hali na muda mwingine alisababisha hadi ukakosana hadi na jamaa zako. Huyu ndiye tunaamini mmeona nae nayeye anakutosheleza. Yeye ndiye sega lako la asali. Mpenzi uliyempenda na kumuweka ndani.
 
Uasherati ni sababu pekee ya kuvunja ndoa. Na ukumbuke mke na mume si ndugu. Hivyo mara moja tu (uasherati) unatosha kuvunja ndoa.

Kama kweli ingekua hivi na Mungu angelifanya sawasawa na neno lake sidhani kama hata wewe ndugu ungekua hai. Mshahara wa dhambi ni mauti, je, umetenda dhambi ngapi hadi sasa na bado ungali hai? Kama ni kweli hadi sasa hujafa basi kubali ya kwamba ni neema ya Mungu inakungoja uiendee toba.

Basi nawe huna budi kumsamehe yeyote yule anayekukosea maadam amekiri amekosea. Ninakuhakikishia, unapomtaliki mtu kwasababu ya uasherati wewe binafsi unajiongezea nafasi kubwa ya kuishia jehanam. Utawapa talaka wangapi? Uliyefungamanishwa nae ni huyohuyo. Kuna mambo mengi sana kwenye ndoa, kila siku ni darasa jipya. Jifunze uvumilivu mpaka itakapoona saba mara sabini umeitimiza.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom