Rasmi nimeamua kuachana na betting. Kubet ni kutafuta umasikini na ufukara

Betting is easier carabao inapoanza. Uefa na Europa zinapoanza.

Mwanzoni mwa ligi.

Also usikimbilie kuziba pengo la hasara. Ukijiona unalose dawa siyo kubet na kubet kucover hii hasara.

Anyway, hua nabet ili kujua kama timu niliyoifuatilia for some time itaact vile nimetarajia so hua naweka amounts comedy.
 
Kweli mkuu betting hapana, ninaroho ngumu lakini nimesarenda
Hahaha umefuata nilichofanya. Mimi nilikuwa nabet japo haikuwa kazi ila stake zangu zilikuwa zimeshiba kuanzia 50,000 na kuendelea mpaka lak kadhaa huko. Kuna siku nilipigwa kipigo kitakatifu ilikuwa mwaka juzi, nikataka rudisha nilichopigwa nikapewa tena. Nikaapa kuwa sitobet tena na toka siku hiyo mwaka juzi sijawahi kubet tena.
 
Hizo hela za betting ungeamua kununua vitu vya geto, ungekuwa mbali sana.
Kamari haiwezi kukutoa kimaisha. Vijana wengi mnadanganyana sana vijiweni.
Fanya kazi na Mungu ataibariki kazi ya mikono yako
Kabisa ndugu betting ni disaster
 
Hahaha umefuata nilichofanya. Mimi nilikuwa nabet japo haikuwa kazi ila stake zangu zilikuwa zimeshiba kuanzia 50,000 na kuendelea mpakalak kadhaa huko. Kuna siku nilipigwa kipigokitakatibu ilikuwa mwaka juzi, nikatakarudisha nilichopigwa nakapewa tena. Nikaapa kuwa sitobet tena na toka siku hiyo mwaka juzi sijawahi kubet tena.
Jambo la maana bora kutumia kidogo ulichonacho kuliko kutamani vikubwa ,visivyowezekana
 
Kwanza niseme tu mimi ni kati ya watu, waliokuwa wakiamini betting kwa asilimia 100, nilikuwa na imani betting ndio kitu itanitoa kimaisha, kuhusu betting ulikuwa huniambii kitu, kuna ile kauli watu huwa wanasema beti kama starehe, Lakini mimi nimekuwa nikiifanya kama kazi ya kujiingizia kipato.

Nilikuwa mstari wa mbele kutoa Matusi, kejeli husda na masimango kwa wale wote, waliokuwa wakionesha kupinga ama kuleta hoja kinzani kuhusiana na gambling/betting.

Katika kipindi kifupi takribani mwaka mmoja baada ya kumaliza masomo ndio nilianza kuifanya betting kama kazi.

Lakini kwa huo muda mfupi, imeniletea hasara kubwa kubwa kubwa ambayo sitokuja kuisahau, yaani zile pesa ambazo nimepoteza ningesema badala ya kutuma kwenye betting company, niziweke kwenye kibubu now ningeweza kufungua biashara kubwa sana.

Baada ya vipigo kuzidi, huwa kuna msemo wanasema sikiliza wataalamu inaonekana strategies unazotumia sio salama, Hao wanaojiita watalamu watakwambia usiweke timu nyingi weka timu chache ,"tafuta odds mbili halafu tia laki," Aloo huo msemo ndio umenifukia kabisa hadi sasa naandika hapa sina hata mia mbovu.

Jana kuna mkeka niliucopy kutoka kwa jamaa mtata sana humu Jamiiforums nikaweka pesa ya nauli ambayo leo nilikuwa naelekea Dar es Salaam, kwa mazingira ya kutatanisha sana pesa yote nimeliwa, mpaka muda huu nimejilaza hapa nasingizia naumwa.

Kwenye betting sio kwamba watu hawashindi wanashinda ila kunautofauti mkubwa sana kati kuliwa na kushinda so ukiifanya kwa muda mrefu ukaja piga mahesabu baada ya mwaka utajikuta na hasara kubwa Hadi utaogopa kama sio kulia.

Betting imefanya nashindwa hata kununua nguo mpya hadi zile nilizomaliza nazo masomo zimeanza kupauka sio kwamba hela sipati hapana zote zinaishia kwenye mikeka, yaani getto unaweza kuta nimenunua sukari robo, mchele kilo mbili halafu kwenye simu nimebet 50000 na yote inaliwa.

Mwaka jana nilikuwa nasimamia mashamba ya jamaa fulani sasa nilikuwa nikipokea hata pesa za kupalilia, na mimi boss wa vibarua najitengea ekari yangu moja ya palizi maana nimepita JKT halafu 60000 naweka mfukoni kisha wale vibarua badala ya kuwalipa 60000 nawalipa 40000 kwa ekari, tutalima weee nikimaliza pesa yote naenda kuliwa kwenye betting.

Usiku wa leo nimekaa nikafanya projection nikiendelea hivi baada ya miaka 5 ijayo nitakuwa mmoja kati ya watu masikini zaidi Tanzania, At 20s vijana wengi hutumia kujenga future zao mimi natumia kubomoa, Betting imeniletea uvivu, muda wote sina furaha, nilikuwa napenda kusoma, kuongeza ujuzi, kutafuta kazi, kuwekeza, kuchangamana na watu, kufanya kazi, mdau wa michezo, mapenzi but now nimekuwa kama mtu aliepigwa bomu.

Bado sijachelewa, nina muda wa kutosha kusahihisha makosa niliyoyafanya, sihitaji tena kuwa mtumwa, nimekubali kusahau yaliyopita na kufungua ukurasa mpya, sioni kama ni tatizo kuanza moja, ninaamini tatizo ni kuendelea kukumbatia adui na adui wangu anaehujumu uchumi wangu ni betting.
Nmekusukiliza kwa umakini mkubwa sana ndgu.kwanza pole sana. mkuu kuna watu wana kunja mpaka 4m kila week kupitia betting. kuna watu wameecha kazi kabisa wao wana bet tu. tatizo hawaji kutoa shuhuda humu

kwenye betting kuna masoko zaid ya 170. kwenye hayo wewe endelea kujitafuta uone soko litakalo ku favour wew. Hauwez kufikia kutengeneza pesa nzuri ya mfululizo kama hujajuwa soko lipi kwako ni sahihi. Mimi nna maika 2 ya kuliwa. Nmefail chuo sababu ya stress za betting (sio kudiscow). kwa nilivo kuona umesoma uchumi au statistics kwa kupita comments zako humu

kuwa mvumilivu na mtulivu tu.kuna pesa nyingi sana ipo humo kwenye betting nadhan hujajuwa soko lako unaloliweza.mimi juzi nmepoteza 2.5m. kijinga tu hyo ni faida niliyotengeneza


zingatia yafuatayo
i) nidhamu
ii) kutokuwa na tamaa
iii)kumbuka ukipata faida kufanya kitu au miradi inayo onekana.mfano umepata milion 5 nunua boda boda fasta zianze kufanya kazi.siku uki drop zina kuinua
iv)kuwa na limit ya kubet na malengo
v) betting inahitaji uwekeze pesa sio ikupe pesa.ni investment ka investments nyingine.pale huend kuchota pesa pale unawekeza

NB
kila la kheri mkuu.gamble what you afford to loose
 
Mnaoiponda betting hamna lolote, ni wivu tu! Watu tunaweka mikeka tunaliwa sanaaa, lakini sometime tunamdaka mhindi vile vile, imagine stake ya 20k inakuletea 10m hata upigwe vipi lazma wewe ni winner tu! Huwez fananisha betting na tatu mzuka au biko. Madrid kafungwa unaona kabsaa! Siyo zile za kuzungusha gurudumu
 
Man Ungelijua Kila Kazi Inachangamoto Zake Na Kila Biashara Haikosi Hasara Usingekuwa Na Maneno Mengi. Kwa Ufupi Ulifanya Kitu Usichokijua, Betting Haimtaki Mtu Mwenye Kichwa Cha Kufugia Nywele
Acha Kudanganya Watu.... Betting Uwezekano was Kupoteza Ni Mkubwa Sana kuliko kupata... Jifanye Mjanja Tena Wewe Ni Suala la Muda Tuu utakuja Kajinyonga Endelea Kuendekeza Kamari... Usijisifu eti Ni Mjanja Hakuna Mtu Mwenye Akili atawekeza Akili yake Kwenye Kamari... Wengi wetu Ni Wahanga Tumeshaona Madhara ya Huu Upumbavu .....
 
Acha Kudanganya Watu.... Betting Uwezekano was Kupoteza Ni Mkubwa Sana kuliko kupata... Jifanye Mjanja Tena Wewe Ni Suala la Muda Tuu utakuja Kajinyonga Endelea Kuendekeza Kamari... Usijisifu eti Ni Mjanja Hakuna Mtu Mwenye Akili atawekeza Akili yake Kwenye Kamari... Wengi wetu Ni Wahanga Tumeshaona Madhara ya Huu Upumbavu .....
Mkuu umeongea kwa uchungu sana inaonekana umesulubiwa sana kama mimi.
 
Mkuu tatizo unabet kimaskini unaweka 500 ili ushinde million unaona inawezkana? Hio ni bht sana asee. Mimi niliweka 500k nikala 6m na usheee lakin ningeweka 500 hapo ningeshinda 6000 unaona utofauti hapo nmepata faida ya 5.5m. Ukibet ukaweke pesa ndogo lazma uweke tim nyingi ili dau liwe kubwa lakin ukiweka timu chache dau kubwa unakua na probability kubwa ya kushinda.
500k!!!. Kuna mawili
1. Wewe ni papaa mwenye fweza zakutosha
2. Una roho ngumu sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom