Rasmi Ethiopia waanza kufua umeme kutoka Mto Nile, Nchi jirani zakasirika

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
1645434946897.png

Ethiopia, leo Jumapili inatarajiwa kufua umeme kutoka kwenye Bwawa la The Grand Ethiopian Renaissance linalokabiliwa na utata lililoko katika Mto Nile.

Bwawa hilo limekuwa chanzo kikuu cha mzozo wa kikanda tangu kuanza kwa ujenzi wake muongo mmoja uliopita. Mataifa jirani ya Ethiopia, Misri na Sudan, yanasema bwawa hilo ni kitisho kwao kutokana na utegemezi wao wa Mto Nile huku Ethiopia ikisema mradi huo ni muhimu kwa ajili ya usambazaji wa umeme na maendeleo.

Bwawa hilo lililogharimu dola bilioni 4.2 linalotarajiwa kuwa mradi mkubwa zaidi wa umeme unalozalishwa kwa nguvu za maji barani Afrika, hatimaye litazalisha zaidi ya megawati elfu 5 za umeme.

Mradi huo utaongeza maradufu uzalishaji wa sasa wa umeme nchini Ethiopia. Mataifa hayo matatu jirani yamefanya duru kadhaa za mazungumzo kuhusu jinsi bwawa hilo linavyopaswa kufanya kazi lakini kufikia sasa, hakujakuwa na dalili ya muafaka.
 
Huku bongo watu wameshabadilisha upepo ili tu wapige 10%, bongo miyeyusho saana, hakuna kiongozi aliyekuwepo pale kwa ajili ya taifa, ni kwa ajili ya kwake.
Yeye 1st.
 
Hapa ndo utaona tofauti ya Vision vs Mission.

Wenzetu wana vision ya vp wanataka kizazi chao cha sasa na kijacho kiwe.

Sisi tuna Mission ya vp sisi na marafiki zetu tunaweza kupiga na kujineemesha binafsi,familia zetu na marafiki zetu.
 
Hapa ndo utaona tofauti ya Vision vs Mission...
Wenzetu wana vision ya vp wanataka kizazi chao cha sasa na kijacho kiwe...
Sisi tuna Mission ya vp sisi na marafiki zetu tunaweza kupiga na kujineemesha binafsi,familia zetu na marafiki zetu.

Sisi siasa zimetawala kwanza kabla ya maendeleo
 
Safi sana, wamenganga sana despite criticism zote za kukatishwa tamaa...
 
... safi sana Ethiopia! Wao wanataka ninyi msitumie rasilimali inayoanzia kwenu ili wao na vizazi vyao wakaifaidi huku wakiwacheka na kuwadharau ninyi ni maskini! Thinking ya kipumbavu kabisa. Tumieni ikiipungua au ikiisha huko inakoenda, nature will decide accordingly.
 
Ethiopia kuanza rasmi kuzalisha umeme kupitia Bwawa Nahdha leo Jumapili

Zoezi la kuzalisha umeme kutoka kwenye Bwawa la al Nahdha limepangwa kuanza rasmi leo Jumapili nchini Ethiopia licha ya bwawa hilo kuendelea kulalamikiwa na nchi mbili za Sudan na Misri.

Bwawa hilo ambalo linajulikana pia kwa jina la Renaissance (GERD) ni mradi mkubwa zaidi wa kuzalisha umeme barani Afrika. Ujenzi wa bwawa hilo kwa kutumia maji ya Mto Nile umezusha mgogoro na mzozo mkubwa baina ya Ethiopia na nchi mbili za Misri na Sudan kwa miaka mingi sasa. Juhudi za kieneo na kimataifa zimeshindwa kutatua mgogoro huo licha ya kujitahidi sana kuutatua tangu mwaka 2011.

Taaarifa ya serikali ya Ethiopia iliyotolewa jana imesema: Kesho (leo Jumapili) bwawa letu litaanza kuzalisha rasmi umeme.

Afisa mwingine wa serikali ya Ethiopia alipoulizwa kuhusu usahihi wa taarifa hiyo naye amethibitisha ukweli wake.

Maafisa wote hao wawili hawakutaka kutajwa majina yao kwani tangazo hilo halijatolewa rasmi na pande husika na wala wao si wasemaji wa mamlaka zilizokabidhiwa jukumu hilo.

Huku ikiwa ni sehemu ya juhudi za kieneo za kutatua mgogoro wa bwawa hilo, mwezi Agosti mwaka jana 2021, Rais Abdelmadjid Tebboune wa Algeria alitangaza kuwa nchi yake imebuni mpango mpya wa kutatua wa mgogoro wa Bwawa la Renaissance baina ya nchi tatu za Ethiopia, Misri na Sudan. Hata hivyo mpango huo nao haukufanikiwa kutatua mgogoro huo.

Ujenzi na ujazaji maji kwenye bwawa hilo uliofanywa na Ethiopia unahesabiwa kuwa ni changamoto kubwa ya kiuchumi, kijamii na kimazingira kwa Misri na Sudan.
 
Ethiopia yaanza kuzalisha umeme kwenye Bwawa la GERD la Mto Nile
274450496_4676154469162496_1514762234283621782_n.jpg


Bwawa lenye utata la Ethiopia kwenye Mto Blue Nile limeanza kuzalisha umeme kwa mara ya kwanza Jumapili. Televisheni ya serikali ya Ethiopia imesema bwawa hilo lenye thamani ya Dola za Kimarekani bilioni 4.2, limekuwa chanzo cha mzozo kati ya Ethiopia, Misri na Sudan tangu ujenzi wake ulipoanza mwaka wa 2011.

Sudan na Misri zinahofia mradi huo unaweza kupunguza mgao wao wa maji ya Mto Nile, lakini Ethiopia inasisitiza kuwa bwawa hilo ni muhimu kwa maendeleo yake. Bwawa linaloitwa Grand Ethiopian Renaissance Dam (GERD) ambalo kwa sasa ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 83.9, ni mradi mkubwa zaidi wa umeme wa maji barani Afrika, na linatarajiwa kuzalisha zaidi ya megawati 5,000 za umeme, na litakapokamilika litaongeza pato la taifa la umeme maradufu.

Kwenye hafla ya ufunguzi iliyooneshwa jana kwenye televisheni, Waziri mkuu wa Ethiopia Bw. Abiy Ahmed alizuru kituo hicho, na baadaye alisema kupitia mitandao ya kijamii kuwa hii ni habari njema kwa Bara la Afrika na nchi za chini wanazopenda kushirikiana nao.
 
Ni sawa kwa sababu bwawa wamejenga kwenye ardhi yao. Ni zaidi ya megawati 5,000 zaidi ya mara mbili ya bwawa la Nyerere.
 
Halafu kuna visomi uchwara vikawa vinakejeli uamuzi wa busara wa Hayati Dr John Joseph Magufuli kuhuisha mpango wa kujenga bwawa la kufufua umeme kule Rufiji
Nakumbuka mmoja wa wasomi aliyepinga ule mradi ni bwana Zitto ambaye ni rafiki mkubwa sana wa Pep Gadiola; Pep kila siku analeta visababu vya ajabu ajabu ili tu bwawa lisiendelee.
 
Hapa ndo utaona tofauti ya Vision vs Mission.

Wenzetu wana vision ya vp wanataka kizazi chao cha sasa na kijacho kiwe.

Sisi tuna Mission ya vp sisi na marafiki zetu tunaweza kupiga na kujineemesha binafsi,familia zetu na marafiki zetu.
Ujenzi wa bwawa la Ethiopia ulianza mwaka 2011 kwahiyo ni zaidi ya miaka 10 ndio umekamilika. Bwawa la Bongo limeanza kujengwa mwaka 2018,huu NI mwaka wa 4 harafu wewe unataka Likamilike. Bwawa letu litaanza kufua umeme mwaka 2025 kwenye Kampeni za CCM. Baada ya Hapo litafungwa kwa mda ili kupisha mgawo wa Umeme nao utambe.
 
Back
Top Bottom