Rasimu ya Mswada wa Sheria ya Kuandika Katiba Mpya - The Proposed Constitutional Review Act

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
Baada ya kupigia kelele rasimu ya kwanza Serikali iliondoa mswada na kwenda kuufanyia marekebisho mbalimbali. Je kilio cha Watanzania kimesikika na hoja tulizozitoa wakati ule zimezingatiwa? Binafsi sijapata muda wa kusoma - ndio nimepata tu mswada huu - lakini natumaini wengijne watapitia na kutoa maoni yao kama ni mswada unaofaa kusimamia uandishi wa Katiba yetu mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015. Jipatie nakala yako.

Mswada uliokataliwa Aprili 2011: BONYEZA HAPA

Mswada Mpya wa Oktoba 2011: BONYEZA HAPA
 
Baada ya kupigia kelele rasimu ya kwanza Serikali iliondoa mswada na kwenda kuufanyia marekebisho mbalimbali. Je kilio cha Watanzania kimesikika na hoja tulizozitoa wakati ule zimezingatiwa? Binafsi sijapata muda wa kusoma - ndio nimepata tu mswada huu - lakini natumaini wengijne watapitia na kutoa maoni yao kama ni mswada unaofaa kusimamia uandishi wa Katiba yetu mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015. Jipatie nakala yako.
Inapatikana wapi Mkuu MJJ? Naitafuta sana
 
mi nasubiri wanasheria wa CDM na wale wa Legal human rights wausomee then waje wanifafanulie -- unajua naweza kusoma na usielewe yaliyomo yanamaana gani kisheria, lugha zenyewe wanatumia na za kimahakama mahakama. na sina uhakika kama huu wa sasa wameandika kiswahili walau na sisi tulioishia form four tukaokota mawili matatu.
 
Naona kulikuwa na shida kwenye attachment ya hapa. Ila angalia post ya awali nimeweka link ya miswada yote miwili - ule uliokataliwa mwanzoni na huu wa sasa. Na kwa vile umendikwa kwa lugha nyepesi tu ya Kiingereza unahitaji uelewa tu nadhani wa pili upo kwa Kiswahili pia.
 
Baada ya kupigia kelele rasimu ya kwanza Serikali iliondoa mswada na kwenda kuufanyia marekebisho mbalimbali. Je kilio cha Watanzania kimesikika na hoja tulizozitoa wakati ule zimezingatiwa? Binafsi sijapata muda wa kusoma - ndio nimepata tu mswada huu - lakini natumaini wengijne watapitia na kutoa maoni yao kama ni mswada unaofaa kusimamia uandishi wa Katiba yetu mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015. Jipatie nakala yako.

Mwanakijiji,

Mimi personally huu mswada nimeusoma na kuuelewa. Serikali is really being clever. Wameuma na kupuliza. How? kwanza Constitution Commissioners watateuliwa na rais kwa kushauriana na rais wa Zanzibar. Hapa nadhani ndo penye tatizo kwa sababu Rais anajua fika kwamba anaweza kuteua team yoyote anayoona ita-bend kwenye matakwa ya chama na serikali. Hapo naona hajatutendea haki watanzania. Ushauri wangu: Hii tume ya kurekebisha katiba ingeundwa na watu mbali mbali. Hata kama rais atateua wajumbe, lakini vile vile sheria imuamuru kushauriana na makundi mbali mbali especially vyama vya upinzani. Kwa sababu composition ya tume ndo kila kitu.

Pili, sheria inampa mamlaka rais ya kuteua Constitutent Assembly (baraza la katiba). Hapa serikali imetupiga changa la macho kwa nini? Kwa sababu, sheria inasema kwamba wabunge wote (bara na visiwani) watakuwa wajumbe wa hii Constituent Assembly-automatically!. Hapa ni dhahiri kwamba hili bunge la katiba litakuwa dominated na wabunge wa CCM. Fair enough kwa watanzania, sheria inatoa nafasi 116 kwa 'wadau mbali mbali' kutoka makundi kama dini, NGOs, vyama vya siasa nk. kuingia kwenye Constituent Assembly (baraza la katiba). Sasa hapa tunadanganywa kwa sababu kiukweli ni kwamba watanzania wa kawaida ambao ndo hii katiba inaandikwa kwa niaba yetu tutakuwa na wawakilishi 116 tuu! (maana wabunge watawakilisha maslahi ya vyama vyao-as experience has shown). Halafu vile vile, sijui wametumia vigezo gani kuamua kwamba kuwe na wajumbe 116. Hapa panahitaji majibu.

To be fair, serikali imeweka 'referendum' kama nafasi ya wananchi kupiga kura ya kuikubali au kuikataa katiba mpya. This is a very good component and I applaud my government. Lakini kiukweli, uwakilishi wetu sisi wananchi kwenye utengenezaji wa hii katiba ni mdogo sana. Na kama mswaada utapitishwa kama ulivyo basi ni dhahiri, katiba ita-reflect matakwa ya CCM. Maana to be fair to the opposition, ni wachache sana kuweza kuweka maslahi na mategemo ya wengi mbele.

Ushauri wangu: Huu mswada, una mapungufu ambayo kama yangefanyiwa kazi ingetusaidia kuwa na katiba nzuri inayoendana na matakwa na maoni ya wananchi walio wengi. Otherwise, wale wote ambao hawakubaliani na huu mswada nafasi yao ya pekee ni kuipinga katiba wakati wa referendum. Kitu ambacho kwangu mimi naona kingetafutiwa ufumbuzi kwa kuhakikisha kwamba kuanzia mwanzo mchakato wa katiba unawashirikisha wengi.

Maoni yangu ni hayo,

Masanja
 
Solution ni wananchi tu kuingia barabarani. Hivi serikali haijajifunza tu mpaka sasa hata baada ya Gaddaffi kuzikwa jangwani?
 
Asante MM kwa taarifa, sio kuzoea dezo lakini tukiweka link hapa jamvini itarahisisha upatikanaji wake zaidi.
 
I long held a feeling that ccm would stupidly play delay tactic to this. Then and ONLY then, probably they'll kindle the revolutionary spark so long abused by vain slogan of amani & utulivu in the midst of unaparalled poverty and much social, political and economic injustice so imposed on wananchi.

Plz can I have the rasimu and of coz the subsequent actual New Katiba very soon?
 
Kama watu wanaona kuwa mambo muhimu hayamo kwenye mswada huu ni wa kuukataa tu. Ni bora watu wasubiri chama ambacho kitakuja kuandika katiba mpya kwa misingi ya uwazi, usawa, demokrasia na utu wa Watanzania kuliko kuburuzwa kwa sababu watu wanataka Katiba Mpya. Tusiburuzwe kwani tutakachoandika ndio urithi wetu kwa kizazi kijacho.
 
JK yuko Australia............. Nimejisemea tu jamani......... Anyway, will catch you later on this!
 
mzee mm hu mswada hau fai kabisa hata kwa kale ka knowledge kangu ka business law ni ngeandika mswada wa kukidhi haja
wasiwasi wangu isije kua mwana wa mfalme na washirika wake ndo wameandika maana huyu mwana mfalme ana taaluma ya sheria
 
Hapo kwenye composition ya Constituent Assembly Article 20 (2) a-e ndio tatizo! Bunge hili hili au lingine? Na hapo kwenye (e) Hao wajumbe 116 kutoka vyama vya siasa, NGOS, FBO's n.k isije ikawa tunawekewa mamluki tu! Ukizingatia mshauri wa Rais kwenye hili ni Makamu Mwenye kiti wa CCM Zanzibar pamoja na AG (Werema aliyesema hakuna haja ya katiba)
 
Tunapata shida sana wale tunaotumia simu kubrowse na pdf haifunguki kwa simu nyingine. MM, naomba uipaste ili tuweze kuisoma kwa simu.
 
Kama watu wanaona kuwa mambo muhimu hayamo kwenye mswada huu ni wa kuukataa tu. Ni bora watu wasubiri chama ambacho kitakuja kuandika katiba mpya kwa misingi ya uwazi, usawa, demokrasia na utu wa Watanzania kuliko kuburuzwa kwa sababu watu wanataka Katiba Mpya. Tusiburuzwe kwani tutakachoandika ndio urithi wetu kwa kizazi kijacho.
Tukiendelea kusubiri chaguzi za katiba hii hii, ushindi utakuwa chama kile kile. Kina Kambona, Babu, Kasanga Tumbo, etc, walisubiri, siku zao zikaisha wakapita, na hawa walioipo wakisubiri, basi nao wataendelea kusubiri mpaka nao siku zao zitapita na wanaokuja nao watasubiri na kusubiri na kusubiri mpaka nao siku zao zitapita!.

Haya na Tusubiri maana subira yavuta kheri!.
 
Asante Mkuu MKJJ,

Mambo ya CCM na serikali yake huwa yananichisha hata kuyaongelea. Ukweli ni kuwa huu mswaada haufai.
 
Muswaada wa Kiingereza tuliukataa!

Ulitoka wa Kiswahili, usiturudishe nyuma.

Huu wa Kiingereza uondoe humu tafadhali.
 
Back
Top Bottom