Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,476
- 215,295
Hakuna asiyeufahamu umahiri wa Rashid Matumla katika ndondi , huyu ni kati ya mabondia wachache sana walioliletea Taifa hili heshima kubwa sana .
Lakini kama ilivyo ada , katika kila jema kuna upande wa pili wa mabaya , Baada ya kupata umaarufu ule , Rashidi akaamua kuzaa watoto wasio na idadi , mithili ya kufyatua matofali kwenye mashine ya umeme .
Ana watoto zaidi ya 10 , ambao ameshindwa kuwatunza na wamegeuka WAKABAJI , ( Mkazi yeyote wa keko anaweza kuthibitisha )
Ukabaji ninaoumanisha hapa ni ile tabia ya vijana vibaka na mateja maeneo ya uswahilini , kuamua kuvizia na kuwakaba na kupora mali za wananchi , hadharani na gizani , kwa maana nyingine ni kwamba Rashid Matumla ameleta kundi la wakabaji kwenye mitaa ileile aliyokuwa akisifiwa kwa ushujaa wake , jambo linaloleta aibu kwake mwenyewe na kwa wote waliomsaidia kuwa bingwa .
Wito kwa wanamichezo wa Tanzania kuweni makini sana na umaarufu wa kupita , angalieni mbele zaidi , msije dhalilika kama Rashid
Lakini kama ilivyo ada , katika kila jema kuna upande wa pili wa mabaya , Baada ya kupata umaarufu ule , Rashidi akaamua kuzaa watoto wasio na idadi , mithili ya kufyatua matofali kwenye mashine ya umeme .
Ana watoto zaidi ya 10 , ambao ameshindwa kuwatunza na wamegeuka WAKABAJI , ( Mkazi yeyote wa keko anaweza kuthibitisha )
Ukabaji ninaoumanisha hapa ni ile tabia ya vijana vibaka na mateja maeneo ya uswahilini , kuamua kuvizia na kuwakaba na kupora mali za wananchi , hadharani na gizani , kwa maana nyingine ni kwamba Rashid Matumla ameleta kundi la wakabaji kwenye mitaa ileile aliyokuwa akisifiwa kwa ushujaa wake , jambo linaloleta aibu kwake mwenyewe na kwa wote waliomsaidia kuwa bingwa .
Wito kwa wanamichezo wa Tanzania kuweni makini sana na umaarufu wa kupita , angalieni mbele zaidi , msije dhalilika kama Rashid