Ras simba kushtakiwa

jogi

JF-Expert Member
Sep 25, 2010
25,558
25,320
Ni kwa kutokuwa mzalendo hasa alipokuja bwana "tothorn" kumsalimia Yohana kwenye makazi yake.
Huyu bwana (ras simba) ana kanuni yake moja hivi ikitumika humuwezesha mtu "kutema yai balaa"

Sasa huyu bwana alipojua kuwa kuna ugeni upo njiani yeye kazima simu na si nyumbani wala kazini kwake alikoonekana!!!

Mzungu si katia timu!!
Watu mule ndani wakamkaribisha kiubishiubishi tu!

Wakati huo wote watu wanamtafuta Ras Simba au angalau ile kanuni yake ya plas ngapi siju plas ngapi tena!!

Si wamemkosa na kanuni pia wameikosa!

Mkuu kapewa taarifa akajitoma kwenye mazungumzo kichwa kichwa!!! Huku na huku tukaanza kuona tabasam kwa mkulu.

Hatimaye zikafuata Ok. Ok. Yes yes ofkozi nyingiiiii kila mzungu alipoporomosha Lugha yenye kanuni.
Ikaonekana kama wameelewana vile!!!!

"Tontoni" kaingia kwenye galfu striim yake (kama ileee mramba alimnunuliaga presidenti wetu wakati uleee) akasepa.

Sababu ya Ras simba kushtakiwa inajengwa kwenye msingi wa hoja hii.

Mkulu akiwa na bashasha akawaambia wananchi wake "jamaa wamepiga magoti, vidume wamelegea!!, fullu shangwe au sio?

Taarifa rasmi si ikatolewa kwa lugha isiyo na kanuni (ukilinganisha na ile ya ras) kuwa Tonton amekubali kumlipa kila mtanzaniya Noah kwa rangi aitakayo!!!!!

Tonton ile anatua mahom kwao anaulizwa (maana na kule wapo wanaoijua lugha hii isiyo na kanuni) eti nasikia umewaambia utawalipa hela zao wanazokudai?
Jamaa likajibu kwa kujiamini kabisa
No! We have agreed to..... ..

Kimbembe ni kwenye magazeti sasa!!!!
Magazeti ya kwetu kuna yalifanikiwa kupata kanuni ya ras yakajikuta yameandika kuwa jamaa wamekubali kukaa kwenye meza ya mazungumzo.

Mengine yanasisitiza tuchague rangi za Noah mapema ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza ikiwa tutachelewa.
Kwamba TONTON analipa fasta!!!!

Ras simba bado anasakwa kwa udi na uvumba afikishwe mahakama ya manzese kwa kuzima simu na kuhatarisha upatikanaji wa Noah kwa kila mwananchi

Wito umetolewa popote akionekana taarifa itolewe redkross.
 
Mmmh mkuu ni yule yule Ras Simba mzee wa kugandamizia N+K+S???
Yaah!
Ndio huyo huyo!!
Huyu jamaa sio mzalendo kabisa, rais wetu kapigwa chenga kwa kizungu na Noah zinayeyuka hivi hivi!!
 
Yaah!
Ndio huyo huyo!!
Huyu jamaa sio mzalendo kabisa, rais wetu kapigwa chenga kwa kizungu na Noah zinayeyuka hivi hivi!!

Sasa hapo Ras Simba anahusika vipi??!!Kwani alimfundisha mkulu??
 
Utoto mtupu ...yani kweli Umemka Asubuhi Umeandika Ujinga wote huo.
Watoto wako wanajua Ww ni Kilaza no.1 wa Taifa.
 
Utoto mtupu ...yani kweli Umemka Asubuhi Umeandika Ujinga wote huo.
Watoto wako wanajua Ww ni Kilaza no.1 wa Taifa.
Si umuulize aliyeelewa kuwa kuna noah zinakuja kumbe kaambiwa tukae tuzungumze??
 
hahaaa jogi wewe sio mzima!!

asante kwa kuniongezea uhai asubuhi hii! Ras Simba atakuwa kafichama pale biashara complex kwenye ile VIP class
Haya naomba Noah yangu, iwe nyeusi tafadhali!
 
hahaaa jogi wewe sio mzima!!

asante kwa kuniongezea uhai asubuhi hii! Ras Simba atakuwa kafichama pale biashara complex kwenye ile VIP class
Haya naomba Noah yangu, iwe nyeusi tafadhali!
:D:D Ni shida!!
 
  • Thanks
Reactions: bht
Jamani japo hii habari ilinipitia mbali nami pia ningependa kuhakikishiwa kadi yangu ya Noah itakuwa salama.
 
Unaweza kukuta hii ni akaunti ya katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo, maana hapajawahi kutokea katibu mkuu wa chama kilaza kama huyu.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom