Ramli za Shafih Dauda kwenye usajili wa Yanga unaondelea

Program Manager

JF-Expert Member
Aug 6, 2018
2,513
3,437
Namnukuu
Tukiacha ushabiki, kwa sasa Simba ina kikosi imara ndani ya uwanja na nje ya uwanja. Yanga hawana kikosi imara ndani ya uwanja wala nje ya uwanja.

Yanga kutaka kushindana na Simba kwa sasa ni uongo! Kwa mtazamo wangu, usajili wanaofanya Yanga sio kwa ajili ya kushindana na Simba kwa maana ya kuchukua ubingwa.

Yanga bado haijafanya vibaya kwa msimu ulioisha, imeshika nafasi ya pili kwenye ligi, imeishia nusu fainali kwenye Kombe la TFF huku ikiwa imetolewa na Bingwa wa ligi na amekuwa bingwa wa Kombe la TFF.

Yanga ipo kwenye process ya kujenga timu labda ili wapiganie nafasi ya kwenda kushiriki kombe la Shirikisho lakini sio kupigania ubingwa wa ligi.

Wachezaji ambao Yanga imewasajili hadi sasa bado watahitaji muda, sio mwezi mmoja au mitatu, huenda ikawa msimu mzima waweze kuelewa tamaduni za mifumo ya uchezaji wa Yanga. Hawezi kuipa Yanga kile inachotaka kwa haraka.

Wachezaji wote wamefanya vizuri kwenye vilabu walivyotoka, wanapokuja Yanga usitegemee viwango vyao vitakuwa vilevile kama kwenye vilabu walikotoka.

Yanga ni tofauti na Kagera Sugar, Mbao na Polisi, Yanga kuna presha ya mashabiki, watu wanataka ushindi asubuhi, mchana na jioni. Kwa hiyo itabidi wachezaji hao wapate muda.

Sitashangaa wachezaji ambao wanasajiliwa sasa hivi 80% wakaja kuachwa baada ya msimu ujao.
Mwisho wa kumnukuu
 
Yupo sahihi.. hata hawa wanaoachwa kina sibomana.. walifanya vizuri sana walipotoka..
 
MCHA MBUZI Dauda anaendelea kwa kusema
Ili uweze kushindana na Simba unahitaji wachezaji wa aina ya Chama, Miquissone, Fraga, Kapombe, Manula, Mkude.

Unazungumzia Simba ambayo Nyoni, Miraji, Ndemla, wote hao wapo nje! Nimi naona timu ya kuipa Yanga ubingwa au kushindana na Simba, ipo ndani ya Simba.

Yanga ilibidi waibomoe Simba, kuna wachezaji ambao wapo Simba wanaweza kwenda Yanga halafu wapambane na Simba kwa sababu watataka kuthibitisha wao ni bora lakini Simba hawapati nafasi.

Mimi nategemea viongozi wa Yanga watoke wawaambie mashabiki kwamba wanajenga timu kitu ambacho ndio ukweli. Yanga bado haijatengemaa kupigania ubingwa sasa kuwaambia wanasajili timu ya kushinda ubingwa msimu ujao watakuwa hawawatendei haki mashabiki wao.
 
Namnukuu
Tukiacha ushabiki, kwa sasa Simba ina kikosi imara ndani ya uwanja na nje ya uwanja. Yanga hawana kikosi imara ndani ya uwanja wala nje ya uwanja.

Yanga kutaka kushindana na Simba kwa sasa ni uongo! Kwa mtazamo wangu, usajili wanaofanya Yanga sio kwa ajili ya kushindana na Simba kwa maana ya kuchukua ubingwa.

Yanga bado haijafanya vibaya kwa msimu ulioisha, imeshika nafasi ya pili kwenye ligi, imeishia nusu fainali kwenye Kombe la TFF huku ikiwa imetolewa na Bingwa wa ligi na amekuwa bingwa wa Kombe la TFF.

Yanga ipo kwenye process ya kujenga timu labda ili wapiganie nafasi ya kwenda kushiriki kombe la Shirikisho lakini sio kupigania ubingwa wa ligi.

Wachezaji ambao Yanga imewasajili hadi sasa bado watahitaji muda, sio mwezi mmoja au mitatu, huenda ikawa msimu mzima waweze kuelewa tamaduni za mifumo ya uchezaji wa Yanga. Hawezi kuipa Yanga kile inachotaka kwa haraka.

Wachezaji wote wamefanya vizuri kwenye vilabu walivyotoka, wanapokuja Yanga usitegemee viwango vyao vitakuwa vilevile kama kwenye vilabu walikotoka.

Yanga ni tofauti na Kagera Sugar, Mbao na Polisi, Yanga kuna presha ya mashabiki, watu wanataka ushindi asubuhi, mchana na jioni. Kwa hiyo itabidi wachezaji hao wapate muda.

Sitashangaa wachezaji ambao wanasajiliwa sasa hivi 80% wakaja kuachwa baada ya msimu ujao.
Mwisho wa kumnukuu
Shafii anawahi kugombea uongozi club ya Simba. Nadhani ilikuwa ujumbe wa kamati ya utendaji.
Kila asemalo liangaliwe kwa jicho hilo.
 
Shafii anawahi kugombea uongozi club ya Simba. Nadhani ilikuwa ujumbe wa kamati ya utendaji.
Kila asemalo liangaliwe kwa jicho hilo.
Kuna muda aligombana sana na manara kutokana na husda zake mpaka wakamchoka
 
Huu uchambuzi ni sawa na mwanahama wa ccm na shabiki wa magufuli aichambue Chadema na wagombea wake,

unaategemea nini kitatokea katika huo uchambuzi!!!!!
 
Kisinda anayesubiriwa na manyani fc keshasaini moroco huku ofa ya sure boy ikikataliwa baada ya kupeleka milioni 29 badala ya 45 wanayotaka yanga
 
Utopolo wana akili ndogo sana,unawezaje kumuacha Jafar Mohamed ukambakisha Juma Mahadhi ambaye ajacheza misimu miwili?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom