sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,026
Upande wa kwanza Zanzibar ni nchi iliyoungana na Tanganyika ikapatikana Tanzania, katika huu muungano Zanzibar inabidi iwe na raisi au makamu wa raisi wa Tanzania, Pia Wazanzibari katika huu muungano wapo Mawaziri, mabalozi, wakuu wa taasisi, wabunge, Idara za ulinzi, waajiriwa, n.k.
Lakini kwa upande mwengine Zanzibar ina serikali yake ambayo haiingiliani na Tanganyika, Kwa mfano kwenye Ajira za serikali ya Zanzibar inabidi muombaji awe mzanzibari, Wana rais wao Mzanzibari, Wana katiba yao, Wana mahakamu wa raisi Mzanzibari, wama bunge lao la wazanzibari, Wana taasisi zao za mpira, umeme, mapato, n.k. Huku Mtanganyika hakumuhusu.
Sasa kama eneo linalooneshwa kwenye ramani ni upande wa Tanganyika pekeyake utasemaje ni ramani ya Tanzania?