magnifico
JF-Expert Member
- Jan 14, 2013
- 7,373
- 13,041
”Simba walinifuata, nitafute kadi ya njano,
wanipe IST mpya”, hayo ni maneno ya mlinda
mlango wa klabu ya Yanga, Ramadhan Kabwili
ambapo amesema kuwa uongozi wa Klabu ya
Simba umewahi kumlaghai ukimtaka atafute
kadi ili asiweze kucheza katika mchezo wa
watani wa jadi na kimuahidi akifanya hivyo
kumpatia garia iana ya IST.
Mlinda mlango huyo amesema hayo wakati
akifanya mahojiano na EATV Radio katika
kipindi cha Kipenga Extra mapema leo
Jumatatu ya tarehe 27, 2020.
“Simba waliwahi kunifuata kipindi tupo na
kocha Zahera, nilikuwa na kadi 2 za njano na
kwenye mchezo wa Yanga na JKT Tanzania,
walitaka nitafute kadi ya njano makusudi ili
wanipe gari ya IST mpya na nikose mchezo
ujao wa watani” – Ramadhan Kabwili.
Amesema kuwa tukio hilo lilitokea kipindi
ambacho Zahera akiwa kocha wa klabu hiyo ya
Yanga.
Amesema kuwa siku hiyo Yanga ilikuwa
inaelekea kucheza na JKT Tanzania na yeye
alikuwa na kadi mbili za njano, hivyo Simba
walimfuata na kumuambia kuwa atafute kadi
moja ya njano ili akose mchezo uliokuwa
unafuatia wa watani wa jadi huku wakimuahidi
kumpa IST mpya, wakiamini kuwa angekaa
Klaus Kindoki golini wangemfunga kirahisi.
Katika mchezo huo dhidi ya JKT Tanzania,
Yanga ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 ambapo
Ramadhan Kabwili ndiye alikuwa golikipa wa
Yanga siku hiyo.
Aidha Kabwili amesema kuwa kwa sasa ahitaji
meneja yoyote atakayemtafutia timu ya
Tanzania akitamani meneja ambaye atamtafutia
timu Ulaya, “mimi nataka meneja ambaye
atanipeleka kucheza soka la Ulaya, sitaki
meneja wa kunichezesha hapa nchini kwa
sababu kama ni hapa nchini sasa hivi nipo
katika klabu kubwa Tanzania na inashinda
mataji”.
Pia Rejea..
Source : Dar24
wanipe IST mpya”, hayo ni maneno ya mlinda
mlango wa klabu ya Yanga, Ramadhan Kabwili
ambapo amesema kuwa uongozi wa Klabu ya
Simba umewahi kumlaghai ukimtaka atafute
kadi ili asiweze kucheza katika mchezo wa
watani wa jadi na kimuahidi akifanya hivyo
kumpatia garia iana ya IST.
Mlinda mlango huyo amesema hayo wakati
akifanya mahojiano na EATV Radio katika
kipindi cha Kipenga Extra mapema leo
Jumatatu ya tarehe 27, 2020.
“Simba waliwahi kunifuata kipindi tupo na
kocha Zahera, nilikuwa na kadi 2 za njano na
kwenye mchezo wa Yanga na JKT Tanzania,
walitaka nitafute kadi ya njano makusudi ili
wanipe gari ya IST mpya na nikose mchezo
ujao wa watani” – Ramadhan Kabwili.
Amesema kuwa tukio hilo lilitokea kipindi
ambacho Zahera akiwa kocha wa klabu hiyo ya
Yanga.
Amesema kuwa siku hiyo Yanga ilikuwa
inaelekea kucheza na JKT Tanzania na yeye
alikuwa na kadi mbili za njano, hivyo Simba
walimfuata na kumuambia kuwa atafute kadi
moja ya njano ili akose mchezo uliokuwa
unafuatia wa watani wa jadi huku wakimuahidi
kumpa IST mpya, wakiamini kuwa angekaa
Klaus Kindoki golini wangemfunga kirahisi.
Katika mchezo huo dhidi ya JKT Tanzania,
Yanga ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 ambapo
Ramadhan Kabwili ndiye alikuwa golikipa wa
Yanga siku hiyo.
Aidha Kabwili amesema kuwa kwa sasa ahitaji
meneja yoyote atakayemtafutia timu ya
Tanzania akitamani meneja ambaye atamtafutia
timu Ulaya, “mimi nataka meneja ambaye
atanipeleka kucheza soka la Ulaya, sitaki
meneja wa kunichezesha hapa nchini kwa
sababu kama ni hapa nchini sasa hivi nipo
katika klabu kubwa Tanzania na inashinda
mataji”.
Pia Rejea..
Ulimboka adakwa kwa kutaka kumhonga Kado
Waandishi Wetu, Dar na Morogoro MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba, Ulimboka Mwakingwe amekamatwa na polisi mkoani Morogoro akihusishwa na njama za kuhujumu mchezo wa Ligi Kuu baina ya Simba na Mtibwa uliopangwa kufanyika leo kwenye Uwanja wa Jamhuri.Mshambuliaji huyo aliyetemwa na mabingwa...
www.jamiiforums.com
Source : Dar24