Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Pamoja na matarajio yetu kuwa Prof. Lipumba umaana wake kwenye siasa za humu ndani unaelekea ukingoni lakini kwa vile CUF itafanya vizuri na kuongeza viti vya ubunge na hakuna chama kitakachokuwa na wabunge wengi Dr. Slaa atamvuta shati Prof. Lipumba na kumpa wadhifa wa Mshauri wa Siasa na Uchumi Ikulu kazi ambayo hata hivyo profesa ana uzoefu nayo tangia siku za Bw. Mwinyi alipokuwa ni Raisi.
Kwa kufanya hivyo CUF na Chadema wataingia makubaliano ya kuunda serikali ya umoja chini ya kaka yetu mpendwa Dr. Slaa.
CCM nao hawatatupwa kwani dada yetu mpendwa Prof. Anna Tibaijuka atakuwa Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke katika historia ya nchi yetu.
Hili kidogo linashangaza kwa sababu CCM na ngebe zote za kuwajali na kuwaenzi wanawake za miaka takribani 50 zilikuwa ni changa la machoni ili kunasa kura za akina mama kwani hata uwaziri mkuu CCM imekuwa ikiwawekea ngumu akina mama!!!!!!!!!!!!
Huu utakuwa mwanzo wa ukombozi wa nchi yetu........
MUNGU IBARIKI TANZANIA .........MUNGU IBARIKI AFRIKA..................
Kwa kufanya hivyo CUF na Chadema wataingia makubaliano ya kuunda serikali ya umoja chini ya kaka yetu mpendwa Dr. Slaa.
CCM nao hawatatupwa kwani dada yetu mpendwa Prof. Anna Tibaijuka atakuwa Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke katika historia ya nchi yetu.
Hili kidogo linashangaza kwa sababu CCM na ngebe zote za kuwajali na kuwaenzi wanawake za miaka takribani 50 zilikuwa ni changa la machoni ili kunasa kura za akina mama kwani hata uwaziri mkuu CCM imekuwa ikiwawekea ngumu akina mama!!!!!!!!!!!!
Huu utakuwa mwanzo wa ukombozi wa nchi yetu........
MUNGU IBARIKI TANZANIA .........MUNGU IBARIKI AFRIKA..................