Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
WanaJF,
Kila kiongozi anatakiwa ajaze form maalumu ya kutaja mali zake kwa mujibu wa sheria ya Maadili ya Umma.
Taarifa zilizothibitishwa ni kwamba mara zote viongozi hao wanapojaza form hizo hakuna hata mmoja anayejaza kwamba anadaiwa na Bodi ya Mikopo!!
Kiongozi anatakiwa ndani ya muda maalumu awe ametaja mali zake na madeni pamoja na kutoa akaunti namba zake za benki! Lakini ni dhahiri kwamba viongozi wamekuwa wakijaza uongo form hizo na tume ya maadili haifuatilii kwa karibu kuthibitisha taarifa zinazotolewa na viongozi kuhusu mali zao!
Kutokana na hali hiyo ndio sababu hata mikopo iliyotolewa kisheria kwa viongozi mbalimbali kwa ajili ya elimu ya juu hairudishwi! Viongozi hawahesabu kama hilo ni deni ambalo linastahili kulipwa!!
Huu ni udanganyifu kama sio uzembe wa viongozi!
Viongozi wote walioshindwa kutaja deni hilo wawajibike kwa kuwaomba radhi wananchi na wajaze upya form za maadili na kuikabidhi tume!
Nawasilisha!
Kila kiongozi anatakiwa ajaze form maalumu ya kutaja mali zake kwa mujibu wa sheria ya Maadili ya Umma.
Taarifa zilizothibitishwa ni kwamba mara zote viongozi hao wanapojaza form hizo hakuna hata mmoja anayejaza kwamba anadaiwa na Bodi ya Mikopo!!
Kiongozi anatakiwa ndani ya muda maalumu awe ametaja mali zake na madeni pamoja na kutoa akaunti namba zake za benki! Lakini ni dhahiri kwamba viongozi wamekuwa wakijaza uongo form hizo na tume ya maadili haifuatilii kwa karibu kuthibitisha taarifa zinazotolewa na viongozi kuhusu mali zao!
Kutokana na hali hiyo ndio sababu hata mikopo iliyotolewa kisheria kwa viongozi mbalimbali kwa ajili ya elimu ya juu hairudishwi! Viongozi hawahesabu kama hilo ni deni ambalo linastahili kulipwa!!
Huu ni udanganyifu kama sio uzembe wa viongozi!
Viongozi wote walioshindwa kutaja deni hilo wawajibike kwa kuwaomba radhi wananchi na wajaze upya form za maadili na kuikabidhi tume!
Nawasilisha!