Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,887
- 143,983
Kama ambavyo mpaka leo hii haujatekeleza uanzishwaji wa wakala wa meli nchini kama ulivyoshauriwa na kamati mojawapo ya makinikia, ndivyo ambavyo mpaka leo hii haujatekeleza wala kuanzisha mchakato wa uanzishwaji wa taasisi hii ambayo itahusika na management ya majanga mbalimbali nchini.
Licha ya Bunge kupitisha sheria ya Disaster Management Act tarehe 26/03/2015,si wewe wala mtangulizi wako ambae ameanzisha hii taasisi.
Hii Agency ingekuwa ni chombo muhimu sana katika kusimami na kuzuia majanga mbalimbali, kuishauri serikali na pia ingeshirikiana na wakuu wa taasisi kama Mamlaka ya Hali ya Hewa,TCRA, Mamla ya Chakula na Dawa, Hifadhi ya Taifa ya chakula,kikosi cha zimamoto,n.k pamoja na wizara mbalimbali katika utendaji wake wa kazi.
Nashangaa hata baada ya hii ajali kutokea, jambo hili halipewi uzito licha ya umuhimu wa taasisi hii katika kushughulikia na kudhibiti majanga mbalimbali hapa nchini na ikiwemo kutoa ushauri kwa serikali kuhusiana na maswala mazima ya majanga.
Ni ajabu hata wapinzani nao wako kimya kabisa kuhusu uanzishwaji wa hii taasisi hata baada ya kutokea kwa hii ajali.
Wabongo hatujielewi kabisa!
Licha ya Bunge kupitisha sheria ya Disaster Management Act tarehe 26/03/2015,si wewe wala mtangulizi wako ambae ameanzisha hii taasisi.
Hii Agency ingekuwa ni chombo muhimu sana katika kusimami na kuzuia majanga mbalimbali, kuishauri serikali na pia ingeshirikiana na wakuu wa taasisi kama Mamlaka ya Hali ya Hewa,TCRA, Mamla ya Chakula na Dawa, Hifadhi ya Taifa ya chakula,kikosi cha zimamoto,n.k pamoja na wizara mbalimbali katika utendaji wake wa kazi.
Nashangaa hata baada ya hii ajali kutokea, jambo hili halipewi uzito licha ya umuhimu wa taasisi hii katika kushughulikia na kudhibiti majanga mbalimbali hapa nchini na ikiwemo kutoa ushauri kwa serikali kuhusiana na maswala mazima ya majanga.
Ni ajabu hata wapinzani nao wako kimya kabisa kuhusu uanzishwaji wa hii taasisi hata baada ya kutokea kwa hii ajali.
Wabongo hatujielewi kabisa!