Rais wetu siku zote nakushauri "Acha uvivu":- kwa hili la ma-Dkt umeharibu kabisa

Danniair

JF-Expert Member
Feb 18, 2011
360
66
Rais wangu mpendwa, waliokushauri kulihutubia taifa kwa gia ya kuzungumza na wazee wamekudanganya. Suala la Ma- dkt si suala la wewe kwenda kuhutubia wahuni wanaoshangilia kwa kuwaita kuwa ni wazee. Pale ulikuwa ukijimwaga na wana CCm na si wazee wa Dar. Kuzungumza na wazee si kuwaambia hayo uliyokuwa unasema! kumbuka ni wazee hao hao wanao lilia huduma ya afya kwani serikali yako imewatupa kabisa. je uliona wale wazee wa kule shinyanga wenye ukoma ambao nyumba zao zimekwisha anguka na sasa wanalala nje? Tungekuona bingwa wa kuwabeza madaktari kama ungekwenda kule makaoni pao na kuongea nao juu ya ma-dkt wetu.

Unajua kuwa Mhimbili haina mazingira mazuri ya kufanyia kazi pamoja na kwamba inaingiza mamilioni kwa usiku tu? Tazama sakafu zake, chakula cha wagonjwa,kitchen utensils, Vitendea kazi kama CT-Scanners, n.k kila siku vibovu. Who is liable for that if not the top most leaders/CEOs? Ebu anza na kuwawajibisha tuone kama TANESCO pia watakuwa wanachezea uchumi wa nchi kwa kukata umeme kama wapendavyo na bila maelezo.
 
angekua anaongea na watu wenye uwezo wa kupambanua mambo sio hao njaa kali ambao kazi yao ni kushangalia na watu wenye udini tu
 
Ndugu watanzania wezangu hebu tujifunze kuelewa na kuthamini kile tunachokisikia ndugu mtoa mada kwanza yapaswa uelewe lengo la mkutano ule lengo la kwanza Mh Rais aliamua kutueleza uma wa watanzania chanzo cha mgogoro ule na hatua zilizowahi kuchukuliwa jee wewe kwa nafasi yako uliwahi kuelewa kwa kina chanzo cha mgogoro ule. La pili elewa tangu mgogoro huu uanze hakukuwahi kutolewa kauli rasmin ya goverment na miongoni mwa watu wa mwanzo kulalama kuhusu tamko la goverment ni wana jf. Madai ya madaktar kwa ujmla wake ni madai chanya na serikali imeyakubali ni ieleweke kama mh rais alivyotueleza kuwa yale si madai ya madaktar peke yake haya ni madai ya watanzania kwa ujumla kupitia sekta tofauti na akaikumbusha serikali na viongozi kwa ujumla kila mtu kwa nafasi yake tubadilike na tujifunze kuchukua hatua mapema. Lengo na comment yangu ni tujifunze kutoa pongezi pale panapohitajika na tujifunze kukosoa pale panapokwenda kombo. Watanzania tufanye kazi tuwache kulalama hii tabia sijuwi imetoka wapi, tujaribu kuachia mihimili ya nchi kila moja kufanya kazi kwa taratibu zake wanasiasa tuwaache na siasa zao wanauchumi tuwaache watushauri na viongozi wa dini tuwaache watuelimishe tukiyatekeleza haya tutafika na hasa vijana safari bado refu siasa haitatusaidia kitu.
 
Ndugu watanzania wezangu hebu tujifunze kuelewa na kuthamini kile tunachokisikia ndugu mtoa mada kwanza yapaswa uelewe lengo la mkutano ule lengo la kwanza Mh Rais aliamua kutueleza uma wa watanzania chanzo cha mgogoro ule na hatua zilizowahi kuchukuliwa jee wewe kwa nafasi yako uliwahi kuelewa kwa kina chanzo cha mgogoro ule. La pili elewa tangu mgogoro huu uanze hakukuwahi kutolewa kauli rasmin ya goverment na miongoni mwa watu wa mwanzo kulalama kuhusu tamko la goverment ni wana jf. Madai ya madaktar kwa ujmla wake ni madai chanya na serikali imeyakubali ni ieleweke kama mh rais alivyotueleza kuwa yale si madai ya madaktar peke yake haya ni madai ya watanzania kwa ujumla kupitia sekta tofauti na akaikumbusha serikali na viongozi kwa ujumla kila mtu kwa nafaspi yake tubadilike na tujifunze kuchukua hatua mapema. Lengo na comment yangu ni tujifunze kutoa pongezi pale panapohitajika na tujifunze kukosoa pale panapokwenda kombo. Watanzania tufanye kazi tuwache kulalama hii tabia sijuwi imetoka wapi, tujaribu kuachia mihimili ya nchi kila moja kufanya kazi kwa taratibu zake wanasiasa tuwaache na siasa zao wanauchumi tuwaache watushauri na viongozi wa dini tuwaache watuelimishe tukiyatekeleza haya tutafika na hasa vijana safari bado refu siasa haitatusaidia kitu.

Politics is sensitive to be left to politicians
 
Back
Top Bottom