Rais wetu, majeshi yetu, wanaelekea kujiondolea uhalali wa kuwatumikia wananchi wa Tanzania

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Nashangaa sana nguvu ya kijeshi ambayo Tanzania inataka kutumia dhidi ya wananchi wasio na silaha katika kuzima kile ambacho ukitafakari sana, ni suala dogo tu la watu kueleza hisia zao juu ya mambo ambayo yanawakera kuhusu haki zao.

Kwa nini Rais awe mkali kiasi hiki, kutishia watu hadi kuonyesha nguvu kubwa za kijeshi? Rais anaogopa nini hasa? Kuna ubaya gani kuacha watu waandamane wakaeleza hisia zao na ukawajibu kistaaarbu tu kwamba malalamiko yako utajaribu kadiri uwezavyo kuyatekeleza?

Nakubali kwamba wakati fulani maandamano ya wananchi hutumiwa na watu wachache katika kufanya uhalifu. Basi ingekuwa busara sana kutumia hao wanajeshi wanaofanya mazoezi kwa ajili ya kuona kuwa maandamano yanafanyika kwa amani pasipo wachache kutumia nafasi hiyo kufanya uhalifu.

Lakini kitendo cha kutishia wananchi wa Tanzania ambao siku zote unasema wewe ni kiongozi wao, na kuwaonyesha nguvu kubwa za kijeshi ili wasieleze malalamiko yao ni ukosefu mkubwa wa busara ya kiuongozi. Ukifanya hivyo siku zote utafanya tatizo liwe kubwa hata zaidi. Ndivyo ilivyokuwa Misri, na hatimaye huko Misri hayo majeshi na bunduki zao zilishindwa dhidi ya nguvu ya wananchi, kwa kuwa walichofanya ni kuwachochea wananchi kwa hasira hata zaidi.

Hainingii akilini kwamba tumefikia mahali ambapo Raisi wa Tanzania anabariki mpambano wa wanajeshi wa JWTZ wenye silaha dhidi ya raia wa Tanzania wasio na silaha! Hivi ukifikia hatua hiyo kweli bado unastahili kuitwa kiongozi wa wananchi, waliokuchagua na wasiokuchagua?

Kiongozi wa nchi yeyote duniani anayetumia majeshi yenye silaha dhidi ya umati wa wananchi wake wasio na silaha, ambao wanachotaka tu ni kujieleza madai yao kwa njia ya amani, basi anakuwa amejiondolea uhalali na ustahiki wa kuitwa kiongozi wa wananchi.

Na pia, kwa jeshi lolote duniani litakalobeba silaha dhidi ya wananchi wa nchi yao wenyewe wasio na silaha, kwa kuwa tu wananchi hao waliamua kueleza dukuduku zao za kimaisha kwa njia ya amani, basi wanajeshi wake wanapaswa wajiulize tena na tena iwapo kiapo chao kilikuwa ni kwa ajili ya kuwatumikia wananchi au viongozi wachache wanajiona mabwana dhidi ya wananchi wanaodai kuwa viongozi wao. Na hususa, siku Jeshi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ, wakichukua silaha dhidi ya Wananchi wa Tanzania wasio na silaha mikononi mwao, basi likome kuitwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania na litafute jina jingine ili wananchi wa Tanzania waelewe wazi kwamba jeshi hilo sio kwa ajili yao tena. Kulikuwa na sababu kwa nini jeshi hili tuliliita JWTZ, na sababu hizo bado ni za msingi.
 
Nakubali kwamba wakati fulani maandamano ya wananchi hutumiwa na watu wachache katika kufanya uhalifu. Basi ingekuwa busara sana kutumia hao wanajeshi wanaofanya mazoezi kwa ajili ya kuona kuwa maandamano yanafanyika kwa amani pasipo wachache kutumia nafasi hiyo kufanya uhalifu.
Mbona muoga?
Unajitisha bure wewe andamana hao wanajeshi watawalinda tu
 
Waandamanaji mmetaharuki na jwtz
Rais ana mamlaka yote kutumia vyombo vya dola kulinda amani
Mnapo hamasishana,mnadai mnataka kumtoa magufuli na shein madarakani,kwa akili zenu mnategemea serikali italala?
 
Waandamanaji mmetaharuki na jwtz
Rais ana mamlaka yote kutumia vyombo vya dola kulinda amani
Mnapo hamasishana,mnadai mnataka kumtoa magufuli na shein madarakani,kwa akili zenu mnategemea serikali italala?
Using'ang'ane kwenye kijidondoo kidogo tu.Umeuelewa uzi? Acha kuwa nanga wa kusoma.
 
Mbona muoga?
Unajitisha bure wewe andamana hao wanajeshi watawalinda tu
Ni kweli jamaa ameshaanza kugwaya. Tukiwauliza wanasema hakuna kiongozi yoyote wa chama aliyeitisha maandamano lakini muda wote wanalalamika kuona mazingira si rafiki kwa maandamano.
 
Siyo kila wakati wananchi wanapoandamana wana dhamira ya kubadilisha serikali bali wanatumia maandamano kama njia ya kupeleka ujumbe kwa viongozi wao(siyo watawala). Ndivyo ilivyotokea Marekani katika vuguvugu la kupinga ubaguzi. Viongozi kutolewa husababishwa na wananchi kutosikilizwa kama ilivyotokea Ethiopia na Tunisia. Majirani Kenya watu wanaandamana sana lakini serikali ipo imara.
 
Kutumia jeshi la wananchi jw kwenye masuala ya siasa nikushushia heshma jeshi letu.nibora wakatae maagizo ya kisiasa hata km yanatoka kwa nani hapo watajijengea heshima kubwa kwa jamii yetu

Acha tu watumike kwani viongozi wao hawajui mipaka na majukumu ya jeshi. Tukiwaona njiani basi ujue hapo ni kama tumetangaziwa state of emergency
 
Woga wangu ni kuwa wanajeshi wenye nia mbaya na utawala unapowatoa makambini ukidhani wanakuja kukusaidia kupambana na kaka zao na Dada zao, wajomba na baba wanaweza kutumia mwanya huo kukutoa madarakani.
Chunga sana matumizi ya majeshi! Hasa haya ambayo yameanza kulalamika kuhusu kuminywa kwa maslahi yao
 
Unadhani kwa nini aliwateua Mabeyo na Sirro
Ni kupata absolute loyalty kumlinda
Haijawahi kutokea nchi hii Rais kukabiliwa na kitisho cha kuondolewa madarakani kama kwa huyu Mhutu
 
Siyo kila wakati wananchi wanapoandamana wana dhamira ya kubadilisha serikali bali wanatumia maandamano kama njia ya kupeleka ujumbe kwa viongozi wao(siyo watawala). Ndivyo ilivyotokea Marekani katika vuguvugu la kupinga ubaguzi. Viongozi kutolewa husababishwa na wananchi kutosikilizwa kama ilivyotokea Ethiopia na Tunisia. Majirani Kenya watu wanaandamana sana lakini serikali ipo imara.
Kweli Mkuu. Hata kama maandamano hayatafanyika leo au kesho, tayari kuna vuguvugu la wananchi kuijia juu serikali. Mbaya zaidi naona kama viongozi wa dini wanaingia taratibu upande wa wananchi. Hakuna kitu kigumu kuzima kama mwamko unaoungwa mkono na viongozi wa dini.
 
Alianza kumuweka Mabeyo kwanza ili iwe rahisi kulitumia jeshi
Naanza kuwa na wasiwasi sana na Mabeyo. Mara nyingi sana anatoa kauli ambazo watangulizi wake huko nyuma hawakuwahi kuzitolea matamko hata siku moja. Na pia kuna wakati anaongea utafiiri yeye ndiye IGP. Labda kashikwa na ile fever ya I wish I kudu be IGP
 
Kutumia jeshi la wananchi jw kwenye masuala ya siasa nikushushia heshma jeshi letu.nibora wakatae maagizo ya kisiasa hata km yanatoka kwa nani hapo watajijengea heshima kubwa kwa jamii yetu
Kutumia silaha za JWTZ dhidi ya wananchi wako mwenyewe ni wendawazimu ambao hakuna mtu anayeweza kueleza. KUmbuka JWTZ wana wajibu wa kulinda kila raia wa nchi, awe raia mwema, mhalifu, awe wa upinzani, awe mpinga CCM nk. Silaha za JWTZ zilinunuliwa kwa ajili ya maadui wa nje, sio kutumika dhidi ya wananchi.
 
Back
Top Bottom