Rais Samia na Watanzania naomba mpitie hapa ili Tanzania ipae kiuchumi

konda msafi

JF-Expert Member
Sep 5, 2018
1,666
8,582
Wakati nipo sekondari nilikuwa natamani niwe sehemu ya watunga sera za nchi au kuwa kiongozi serikalini, na hii ilisababishwa na jinsi nilivyokuwa naona mambo yanavyoendeshwa nchini. Niliona bila kuingia ndani ya siasa siwezi kubadirisha chochote, nitabaki kuwa mtazamaji tu, kama kuna mambo hayapo sawa na ninahitaji kuyabadirisha sina budi kuingia jikoni na hii ndoto nahisi siku moja itakuja kutimia. Mniombee.

Kwa sasa kila nikiiangalia nchi yangu naona inahitaji viongozi wenye maono na mikakati isiyoyumba ili kuipeleka Tanzania katika ulimwengu wa kwanza. Nchi za Ulaya na Amerika ya kaskazini hazijaamuka tu siku moja zikawa pale zilipo. Viongozi wake walikuwa na maono na mikakati isiyoyumba, na kila rais au kiongozi aliyekuwa anapata dhamana ya kuongoza alikuwa anatembea mle mle kwenye yale maono na mikakati iliyowekwa na watangulizi wake. Kama wao waliweza kuwa ulimwengu wa kwanza kwa nini sisi watanzania tushindwe ukizingatia sisi tuna rasimali za asili nyingi kuwazidi wao, tuna hali ya hewa nzuri, tuna ardhi inayomea kila aina ya mmea.

Natamani Tanzania iwe nchi ya kwanza Africa kufikia uchumi wa kwanza. Hili lipo ndani ya uwezo wetu watanzania, ni swala la kuamua tu na kujifunga mkanda.

Naomba tujadili kidogo nini kifanyike, hii ni nchi yetu, hatuna nchi nyingine zaidi yahii.

Binafsi vifuatavyo ni baadhi ya mambo ambayo yakifanyika Tanzania inakuwa ni miongoni mwa nchi za ulimwengu wa kwanza.

  • Lazima tupate katiba nzuri inayokwenda na wakati tulionao
Kwenye katiba kuanishwe malengo ya muda mrefu na ya muda mfupi. Moja ya malengo ya muda mfupi yanaweza kuwa mengi ila nitataja machache ambayo tunaweza kuanza nayo kama nchi,

  • Kuhakikisha serikali inakuja na sera za kuondoa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.
Hapa serikali inatakiwa kuja na mikakati ya kuchochea uwekezaji kutoka ndani na nje. Kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ili kutengeneza ajira. Serikali inaweza kutoa incentives kwa wawekezaji. Hii inaweza kuwa katika mfumo wa kupunguza kodi au kupunguza gharama za uagizaji wa mitambo ya viwandani, au serikali inaweza kutoa asilimia fulani ya kusaidia manunuzi ya mtambo wowote utakaonunuliwa na muwekezaji atakayekuwa tayari kujenga kiwanda fulani. Kwa mfano serikali inahitaji muwekezaji kwenye kiwanda cha mafuta ya kupikia au sukari kwa sababu kuna upungufu wa hizo bidhaa nchini. Serikali inaweza kutangaza kwamba muwekezaji mzawa atakayejenga kiwanda cha sukari au mafuta ya kupikia, serikali itachangia asilimia 25 ya gharama ya huo mtambo. Au serikali inaweza kutangaza kwamba kampuni yeyote itakayoweza kuajiri wafanyakazi kuanzia 20,000 haitalipa tozo ya Skill Development Levy (SDL). Hii ni mifano tu, watunga sera watatakiwa wewe wabunifu wa kubuni njia ambazo zitasaidia kuchochea ajira
  • Lengo jingine la muda mfupi linaweza kuwa hili; Hizi nafasi za uteuzi zenye mishahara mikubwa kama ukuu wa mikoa, ukuu wa wilaya, ukatibu mkuu, ukatibu tawala na zingine zote zinazoshabihiana na hizi zitumikiwe kwa miaka miwili tu ili kuwapisha wengine.
Sio mtu mmoja anakuwa kwenye hizo nafasi kwa muda mrefu. Wewe kama upo kwenye hizo nafasi na let’s say unapata mshahara wa milioni 4 kwa mwezi kwa muda wa miaka 2 utakuwa umetengeneza 96,000,000. 96,000,000 inakutosha sana kwenda kuanzisha biashara au uwekezaji na ukasaidia kutoa ajira kwa wengine. Kufikia uchumi wa duania ya kwanza sio lelemama hivyo uwajibikaji inabidi uanzie kwa viongozi wenyewe. Kwa hiyo kukiwa na utaratibu wa kuachiana madaraka na kwenda kuanzisha biashara baada ya kuachia madaraka kunakuwa na multiplier effect kwenye uchumi hususani kwenye kutengeneza ajira maana watanzania wengi wataajiriwa kwenye hizo nyadhifa na pia watanzania wengi wataajiriwa kwenye hizo ajira zitakazotengenezwa na hao viongozi walioachia madaraka baada ya miaka miwili.
  • Lengo jingine la muda mfupi ni hili, au linaweza kuwa la muda mrefu inategemea litadumu kwa muda gani;
kwa mfano kwa sasa bei ya sukari na mafuta ya kupikia yamepanda bei karibia 60% hii ilisababishwa na serikali kupiga marufuku uagizwaji wa hizi bidhaa kutoka nje ili kulinda viwanda vya ndani ilihali viwanda vya ndani havina uwezo wa kukidhi mahitaji ya ndani. Madhara yake ni bei ya sukari na mafuta imepanda bei na imeshindwa kushuka licha ya matamko ya viongozi kuwa bei ishuke, na hii bei inamuumiza mlaji wa mwisho. Kama hakuna muwekazaji, serikali inaweza kuanziasha kilimo cha alizeti na karanga na kujenga kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia. Serikali inaweza kuanzisha mashamba ya miwa na kujenga kiwanda cha sukari. Tanzania tuna ardhi yenye rutuba kila mkoa hivyo serikali ikiamua kutatua hii changamoto ya sukari na mafuta ya kupikia haishindwi. Natambua kiuchumi sio afya kwa serikali kujihusisha moja kwa moja kwenye biashara lakini kuna exceptional cases kama hizi, sidhani kama kutakuwa na madhara kama serikali itachukua jukumu la kuzalisha bidhaa ambayo private sector imeshindwa kuzalisha kwa kiwango kinachohitajika nchini. Nadhani huu uwekezaji kwenye hizi bidhaa ni wenye tija zaidi kwa watanzania kuliko uwekezaji wa kwenye ndege. Ndege wanapanda watanzania wachache wenye uwezo lakini sukari na mafuta ya kupikia yanatumiwa na watanzania wote, hivyo unaweza kuona manufaa kwa watanzania kama serikali itaamua kuwekeza kwenye bidhaa ambazo sector binafsi imeshindwa kukidhi mahitaji ya walaji. Pia kama serikali itawekeza kwenye hii miradi itasaidia kutengeneza ajira hivyo tatizo la ajira litazidi kupungua maana kwenye hayo mashamba ya miwa, karanga na alizeti watanzania wataajiriwa, kwenye hivyo viwanda vya sukari na mafuta pia watanzania wataajiriwa.
  • Malengo ya muda mrefu
Malengo ya muda mrefu yatakuwepo mengi kulingana na ubunifu wa watunga sera wetu watakaopewa hii dhamana, ila hapa nitataja machache ambayo yanaweza kuwemo kwenye hayo malengo

i. Elimu,
Hakuna nchi yeyote katika ulimwengu wa kwanza iliyoendelea kiuchumi bila kuweka mifumo mizuri ya elimu, na zaidi ya yote bila kuwekeza kwenye masomo ya sayansi na hesabu. Elimu bora ndio kila kitu kwenye maendeleo. Sasa hivi dunia ipo kwenye ulimwengu wa sayansi na tekinologia, bila elimu tutabaki kuwa wachuuzi tu, hatuwezi kumiliki na kuendesha viwanda vyetu. Kuna rafiki yangu ni raia wa Canada ila ana asili ya kieritrea, ana ndugu zake wa damu Ujerumani na nchi za Scandinavia. Nchi zote hizo amefika na kukaa kidogo. Aliniambia “Africa bila kuwekeza kwenye elimu tutabaki kuwa nyuma siku zote, Africa itapiga maendeleo makubwa ya kiuchumi kama itawekeza kwenye elimu hasa masomo ya sayansi na hesabu”. Alinitolea mfano nchi ya Sweden kama sikosei au the Netherlands ilikuwa masikini sana lakini serikali ilitunga sera na sheria kuhakikisha masomo ya sayansi na hesabu yanakuwa ya lazima, na kuhakikisha wanafunzi kutokea elementary school hadi chuo wanafundishwa vyema, wanapikika na kuiva kwenye hesabu na sayansi. Yalikuwa ni malengo ya muda mrefu lakini baada ya muda matunda yalionekana, na sasa kama mnavyoona hiyo nchi ipo ulimwengu wa kwanza. Anasema hiyo nchi walimu wanaongoza kwa kulipwa mishahara mikubwa. Kwa hiyo sisi watanzania kama tunataka kufika huko lazima tuwekeze kwenye elimu, hakuna short cut ya maendeleo, lazima tuwe na mipango ya muda mrefu ambayo tutakuwa na uhakika kuwa baada ya muda fulani tutakuwa level nyingine. Natambua tunaweza kuwa na changamoto ya kupata walimu wa hesabu na sayansi kukidhi mahitaji ya shule zetu lakini tukiamua hii changamoto tunaishinda. Kuishinda hii changamoto serikali inaweza kutangaza nafasi za kazi za ualimu wa hayo masomo duniani. Mtu yeyote kutoka nchi yeyote anayeyamudu hayo masomo aruhusiwe aje apate kazi, na viza yake isiwe na urasimu kuipata. Kuwe tu na screening ya uhakika ili isitumike kama uchochoro wa raia wa nchi zingine kuja kufanya yao Tanzania.

Nchi ya Korea ya kusini ina utaratibu wa watu kutoka mataifa ambayo English ni lugha ya nyumbani kuruhusiwa kwenda kufundisha kiingeeza huko. Ukiwa na passport ya hizo nchi unapata viza ya kwenda kufundisha kiingereza. Kwa nini Tanzania tusifanye hivyo.

Malengo ya nchi, rais akiingia madarakani lazima ayafuate.
  • Kwa sababu tumeamua kama nchi kufikia uchumi wa juu, itungwe sheria ya kumtaka kila rais anayeingia madarakani ayatekeleze malengo ya nchi. Rais hatakuwa na uwezo wa kuiendesha nchi anavyotaka yeye. Awe na job description kabisa kwamba watanzania wamejiwekea malengo haya hivyo ukiingia madarakani lazima uyatekeleze, ukienda kinyume na hayo malengo bunge linakutoa kwenye hicho kiti cha urais na makamu wa rais anachukua usukani au uchaguzi mwingine unafanyika. Katiba itaweka wazi kipi ni bora zaidi kati ya kufanya uchaguzi au makamu wa rais kushika madaraka.

  • Ili kuhakikisha hili linafanyika, inaweza kuundwa taasisi huru ambayo itakuwa inahakikisha rais anafuata katiba. Unajua sisi watanzania ni wapole sana. Tunaweza kuwa na katiba bora kabisa ambayo imeainisha mambo yote yanayotakiwa kutekelezwa na rais, na tukawa na taasisi amabayo jukumu lake ni kuhakikisha katiba haivunjwi. Lakini pamoja na kuwa na hivi vyote unaweza kukuta rais bado anavunja katiba na hiyo taasisi iliyoundwa kumuwajibisha rais haimfanyi chochote, na raia nao washatishwa kupigwa kipigo cha mbwa koko wamefyata hata kuandamana kushinikiza katiba ifuatwe hawawezi. Sasa nini kifanyike, labda inaweza kutungwa sheria inayotambua huu woga na udhaifu wa watanzania ikasema kwamba “Pale rais au kiongozi yeyote wa juu serikalini anapovunja sheria au anapoenda kinyume na mipango iliyaoanishwa kwenye katiba, raia yeyote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana haki ya kufungua kesi katika mahakama za kimataifa ili kushikikiza katiba ifuatwe na kumwajibisha rais au kiongozi aliyevunja katiba au aliyeenda kinyume cha malengo yaliyoainishwa kwenye katiba”

  • Kwa muktadha huu mahakama za kimataifa zitakuwa zimearifiwa kuhusu katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo zitakuwa na mamlaka yaku-prosecute kesi ya namna hii itakapoletwa mbele yake. Kuna watu wataanza kusema Konda msafi wewe sio mzalendo, rais wetu ashitakiwe nje tena? hapana mimi ni mzalendo, najaribu tu kuwa realistic. Haya ni mawazo tu ambayo yanaweza kufikiriwa kuingizwa kwenye katiba na sio lazima yaingizwe, huenda kukawa na mawazo bora zaidi ya haya ambayo yatasaidia kuhakikisha katiba inalindwa na malengo tuliyojiwekea kama nchi hayatelekezwi.

  • Rais kuachana na mambo ya uchama akiwa madarakani

    Kwa sababu tumeamua kupiga kazi kwa ajili ya nchi yetu. Uchaguzi ukiisha na rais akatangazwa katiba imzuie rais kushabikia hadharani mambo ya chama chake badala yake awatumikie wananchi. Mambo ya mipasho kuwananga wapinzani yasiwepo, kauli za kuwagawa wananchi kwa misingi ya chama zisiruhusiwe. Rais ni rais wa raia wote na sio rais wa chama kilichompa ticketi ya kuwania urais. Mambo ya chama atayaongea akiwa kwenye vikao vya chama chao lakini anapokuwa nje au kwenye ziara za kikazi hataruhusiwa kuongea mambo ya kichama. Atatakiwa awe na kazi ya kuhamasisha umoja, ushirikiano na uzalendo na kutekeleza malengo yaliyoainishwa kwenye katiba.

  • Sheria kandamizi
    Ili tufike tunakotaka, sheria kandamizi zote zifutwe. Sheria zina nafasi kubwa sana kwenye kuleta maendeleo. Sheria zote zinazokwamisha maendeleo zifutwe. Sheria zote kandamizi zifutwe. Mojawapo ya sheria kandamizi ambazo binafsi ningependa zifutwe ni hizi: sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii NSSF na PSSSF. Kumpangia mtu namna ya kutumia hela yake, hii sheria ni kandamizi. Fao la kujitoa lirudishwe. Mfanyakazi akiachishwa kazi au akiacha kwa hiari yake apewe hela yake ikamsaidie mambo yake. Haya mambo ya kumzuia kuchukua hela yake mpaka uzeeni hayafai. Apewe hela yake ili kama anataka kufanya biashara akafanye akatengeneze ajira. Sheria nyingine kandamizi ni hii ya kufungwa miaka 30 jela ukimpa ujauzito mwanafunzi. Hii sheria ukiachilia kuwa ni kandamizi pia inamnyima haki mtoto atakayezaliwa haki ya kulelewa na wazazi wake wote wawili. Unapomfunga baba wa mtoto huoni kama unakitesa kiumbe kisichokuwa na hatia? Baba ake mmemfunga, huyo mtoto atahudumiwa na nani? Mama mjamzito atahudumiwa na nani? Zaidi ya yote unapomfunga baba wa mtoto unapata faida gani? Sheria kandamizi zipo nyingi, hizi mbili ni mifano tu.

    Karibuni tujadiliane, ushauri na mapendekezo. Tanzania ni yetu sote. Kazi ieendelee.
Pia kwa kuongezea kama kutunga katiba mpya ni gharama basi zinaweza kutungwa sheria mpya zinazoendana na mipango yetu ya kufikia uchumi wa juu, na sheria kandamizi zikafutwa. Hatutakiwi kuwa na sheria kandamizi kwenye ulimwengu wa sasa uliojaa watu wastaarabu. Katiba ya Jaji Warioba inaweza kutumika ila kukatungwa sheria zingine ambazo specifically kwa ajili ya utekelezaji wa mipango ya nchi.
 
Hizo pesa za kuwapa watu wale Ili watuandikie Katiba, ni kupoteza pesa ya umma tu, Katiba haileti maendeleo, inahitajika na utashi wa kisiasa

Kenya Wana Katiba nzuri Afrika, mbona hakuna maendeleo, China, Russia, North Korea hakuna Katiba "nzuri"lakini nchi zimeendelea sana, sie tuna hitaji viwanda, sio vyerehani na upuuzi wa kusema kila mkoa una viwanda 100!!

Kama music industry ilivyofanikiwa, tufsnye na sekta zingine ziwe hivyo, mifano ya kuiga ipo Mingi, Dubai, Philippine, malaysia, Japan, Korea, china, hii nchi inakosa utashi wa kisiasa tu,

Watu wanapenda chama kuriko nchi.haya mavyeo ya kupeana hayawezi kutusaidia,kwanza inabidi yafutwe.
RC hana kazi yoyote zaidi ya kuwa nyapara tu,

Tanzania tuliwahi kuwa na viwanda vya radio, betri, sana za kilimo, pale kibaha tulikuwa tuna assembling plant ya scania miaka ya 90! sasa hv tunayo skilled labour kwanini hatuna viwanda vya magari, compyuta, Tunaishia kuagiza china!?

Serikali inabidi isaidie kuanzisha hivi viwanda sio serikali inaenda kuanzisha kiwanda Cha kusaga unga wa lishe!
 
Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na wenye nchi (Watanzania) ipo na tunayo. Wanasiasa kwa maslahi yao hawataki kuipitisha. Kwa kiburi hicho inatakiwa tuwapige chini au wakubaliane na matakwa yetu. Hakuna sababu ya kuanza upya ni kupoteza muda na ni matumizi mabaya ya rasilmali zetu tunazozihitaji kwa maendeleo yetu. Tupeni katiba yetu tuliyomuagiza Jaji Warioba ailete kwenu muipitishe. wanasiasa kumbukeni mliingia mjengoni kwa niaba yetu na si vinginevyo.
 
Hizo pesa za kuwapa watu wale Ili watuandikie Katiba,ni kupoteza pesa ya umma tu,Katiba haileti maendeleo,inahitajika na utashi wa kisiasa,
Kenya Wana Katiba nzuri Afrika,mbona hakuna maendeleo,China,Russia,North Korea hakuna Katiba "nzuri"lakini nchi zimeendelea sana,sie tuna hitaji viwanda,sio vyerehani na upuuzi wa kusema kila mkoa una viwanda 100!!
Kama music industry ilivyofanikiwa,tufsnye na sekta zingine ziwe hivyo,mifsno ya kuiga ipo Mingi,Dubai,Philippine,malaysia,Japan,Korea,china,hii nchi inakosa utashi wa kisiasa tu,
Watu wanapenda chama kuriko nchi.haya mavyeo ya kupeana hayawezi kutusaidia,kwanza inabidi yafutwe.
RC hana kazi yoyote zaidi ya kuwa nyapara tu,
Tanzania tuliwahi kuwa na viwanda vya radio,betri,sana za kilimo,pale kibaha tulikuwa tuna assembling plant ya scania miaka ya 90!sasa hv tunayo skilled labour kwanini hatuna viwanda vya magari,compyuta,Tunaishia kuagiza china!?
Serikali inabidi isaidie kuanzisha hivi viwanda sio serikali inaenda kuanzisha kiwanda Cha kusaga unga wa lishe!
Umeongea vizuri sana ndugu yangu mwarobaini wa matatizo yetu sio katiba mpya bali ni utashi wa kisiasa tukiweka uvyama pembeni na tukavaa roho ya kuitumikia Nchi kwa nguvu zako zote kwa kipindi kifupi tu tutakuwa tumeshapiga hatua ila tukindelea na hizi porojo za majukwaani tutakesha
 
Wakati nipo sekondari nilikuwa natamani niwe sehemu ya watunga sera za nchi au kuwa kiongozi serikalini, na hii ilisababishwa na jinsi nilivyokuwa naona mambo yanavyoendeshwa nchini. niliona bila kuingia ndani ya siasa siwezi kubadirisha chochote, nitabaki kuwa mtazamaji tu, kama kuna mambo hayapo sawa na ninahitaji kuyabadirisha sina budi kuingia jikoni na hii ndoto nahisi siku moja itakuja kutimia. Mniombee.

Kwa sasa kila nikiiangalia nchi yangu naona inahitaji viongozi wenye maono na mikakati isiyoyumba ili kuipeleka Tanzania katika ulimwengu wa kwanza. Nchi za Ulaya na Amerika ya kaskazini hazijaamuka tu siku moja zikawa pale zilipo. Viongozi wake walikuwa na maono na mikakati isiyoyumba, na kila rais au kiongozi aliyekuwa anapata dhamana ya kuongoza alikuwa anatembea mle mle kwenye yale maono na mikakati iliyowekwa na watangulizi wake. Kama wao waliweza kuwa ulimwengu wa kwanza kwa nini sisi watanzania tushindwe ukizingatia sisi tuna rasimali za asili nyingi kuwazidi wao, tuna hali ya hewa nzuri, tuna ardhi inayomea kila aina ya mmea.

Natamani Tanzania iwe nchi ya kwanza Africa kufikia uchumi wa kwanza. Hili lipo ndani ya uwezo wetu watanzania, ni swala la kuamua tu na kujifunga mkanda.

Naomba tujadili kidogo nini kifanyike, hii ni nchi yetu, hatuna nchi nyingine zaidi yahii.

Binafsi vifuatavyo ni baadhi ya mambo ambayo yakifanyika Tanzania inakuwa ni miongoni mwa nchi za ulimwengu wa kwanza.

  • Lazima tupate katiba nzuri inayokwenda na wakati tulionao
  • Kwenye katiba kuanishwe malengo ya muda mrefu na ya muda mfupi.

  • Moja ya malengo ya muda mfupi yanaweza kuwa mengi ila nitataja machache ambayo tunaweza kuanza nayo kama nchi, i. kuhakikisha serikali inakuja na sera za kuondoa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana. Hapa serikali inatakiwa kuja na mikakati ya kuchochea uwekezaji kutoka ndani na nje. Kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ili kutengeneza ajira. Serikali inaweza kutoa incentives kwa wawekezaji. Hii inaweza kuwa katika mfumo wa kupunguza kodi au kupunguza gharama za uagizaji wa mitambo ya viwandani, au serikali inaweza kutoa asilimia flani ya kusaidia manunuzi ya mtambo wowote utakaonunuliwa na muwekezaji atakayekuwa tayari kujenga kiwanda flani. Kwa mfano serikali inahitaji muwekezaji kwenye kiwanda cha mafuta ya kupikia au sukari kwa sababu kuna upungufu wa hizo bidhaa nchini. Serikali inaweza kutangaza kwamba muwekezaji mzawa atakayejenga kiwanda cha sukari au mafuta ya kupikia, serikali itachangia asilimia 25 ya gharama ya huo mtambo. Au serikali inaweza kutangaza kwamba kampuni yeyote itakayoweza kuajiri wafanyakazi kuanzia 20,000 haitalipa tozo ya Skill Development Levy (SDL). Hii ni mifano tu, watunga sera watatakiwa wewe wabunifu wa kubuni njia ambazo zitasaidia kuchochea ajira

  • ii. Lengo jingine la muda mfupi linaweza kuwa hili; Hizi nafasi za uteuzi zenye mishahara mikubwa kama ukuu wa mikoa, ukuu wa wilaya, ukatibu mkuu, ukatibu tawala na zingine zote zinazoshabihiana na hizi zitumikiwe kwa miaka miwili tu ili kuwapisha wengine. Sio mtu mmoja anakuwa kwenye hizo nafasi kwa muda mrefu. Wewe kama upo kwenye hizo nafasi na let’s say unapata mshahara wa milioni 4 kwa mwezi kwa muda wa miaka 2 utakuwa umetengeneza 96,000,000. 96,000,000 inakutosha sana kwenda kuanzisha biashara au uwekezaji na ukasaidia kutoa ajira kwa wengine. Kufikia uchumi wa duania ya kwanza sio lelemama hivyo uwajibikaji inabidi uanzie kwa viongozi wenyewe. Kwa hiyo kukiwa na utaratibu wa kuachiana madaraka na kwenda kuanzisha biashara baada ya kuachia madaraka kunakuwa na multiplier effect kwenye uchumi hususani kwenye kutengeneza ajira maana watanzania wengi wataajiriwa kwenye hizo nyadhifa na pia watanzania wengi wataajiriwa kwenye hizo ajira zitakazotengenezwa na hao viongozi walioachia madaraka baada ya miaka miwili.

  • iii. Lengo jingine la muda mfupi ni hili, au linaweza kuwa la muda mrefu inategemea litadumu kwa muda gani; kwa mfano kwa sasa bei ya sukari na mafuta ya kupikia yamepanda bei karibia 60% hii ilisababishwa na serikali kupiga marufuku uagizwaji wa hizi bidhaa kutoka nje ili kulinda viwanda vya ndani ilihali viwanda vya ndani havina uwezo wa kukidhi mahitaji ya ndani. Madhara yake ni bei ya sukari na mafuta imepanda bei na imeshindwa kushuka licha ya matamko ya viongozi kuwa bei ishuke, na hii bei inamuumiza mlaji wa mwisho. Kama hakuna muwekazaji, serikali inaweza kuanziasha kilimo cha alizeti na karanga na kujenga kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia. Serikali inaweza kuanzisha mashamba ya miwa na kujenga kiwanda cha sukari. Tanzania tuna ardhi yenye rutuba kila mkoa hivyo serikali ikiamua kutatua hii changamoto ya sukari na mafuta ya kupikia haishindwi. Natambua kiuchumi sio afya kwa serikali kujihusisha moja kwa moja kwenye biashara lakini kuna exceptional cases kama hizi, sidhani kama kutakuwa na madhara kama serikali itachukua jukumu la kuzalisha bidhaa ambayo private sector imeshindwa kuzalisha kwa kiwango kinachohitajika nchini. Nadhani huu uwekezaji kwenye hizi bidhaa ni wenye tija zaidi kwa watanzania kuliko uwekezaji wa kwenye ndege. Ndege wanapanda watanzania wachache wenye uwezo lakini sukari na mafuta ya kupikia yanatumiwa na watanzania wote, hivyo unaweza kuona manufaa kwa watanzania kama serikali itaamua kuwekeza kwenye bidhaa ambazo sector binafsi imeshindwa kukidhi mahitaji ya walaji. Pia kama serikali itawekeza kwenye hii miradi itasaidia kutengeneza ajira hivyo tatizo la ajira litazidi kupungua maana kwenye hayo mashamba ya miwa, karanga na alizeti watanzania wataajiriwa, kwenye hivyo viwanda vya sukari na mafuta pia watanzania wataajiriwa.

  • Malengo ya muda mrefu

  • Malengo ya muda mrefu yatakuwepo mengi kulingana na ubunifu wa watunga sera wetu watakaopewa hii dhamana, ila hapa nitataja machache ambayo yanaweza kuwemo kwenye hayo malengo
  • i. Elimu,
  • Hakuna nchi yeyote katika ulimwengu wa kwanza iliyoendelea kiuchumi bila kuweka mifumo mizuri ya elimu, na zaidi ya yote bila kuwekeza kwenye masomo ya sayansi na hesabu. Elimu bora ndio kila kitu kwenye maendeleo. Sasa hivi dunia ipo kwenye ulimwengu wa sayansi na tekinologia, bila elimu tutabaki kuwa wachuuzi tu, hatuwezi kumiliki na kuendesha viwanda vyetu. Kuna rafiki yangu ni raia wa Canada ila ana asili ya kieritrea, ana ndugu zake wa damu Ujerumani na nchi za Scandinavia. Nchi zote hizo amefika na kukaa kidogo. Aliniambia “Africa bila kuwekeza kwenye elimu tutabaki kuwa nyuma siku zote, Africa itapiga maendeleo makubwa ya kiuchumi kama itawekeza kwenye elimu hasa masomo ya sayansi na hesabu”. Alinitolea mfano nchi ya Sweden kama sikosei au the Netherlands ilikuwa masikini sana lakini serikali ilitunga sera na sheria kuhakikisha masomo ya sayansi na hesabu yanakuwa ya lazima, na kuhakikisha wanafunzi kutokea elementary school hadi chuo wanafundishwa vyema, wanapikika na kuiva kwenye hesabu na sayansi. Yalikuwa ni malengo ya muda mrefu lakini baada ya muda matunda yalionekana, na sasa kama mnavyoona hiyo nchi ipo ulimwengu wa kwanza. Anasema hiyo nchi walimu wanaongoza kwa kulipwa mishahara mikubwa. Kwa hiyo sisi watanzania kama tunataka kufika huko lazima tuwekeze kwenye elimu, hakuna short cut ya maendeleo, lazima tuwe na mipango ya muda mrefu ambayo tutakuwa na uhakika kuwa baada ya muda flani tutakuwa level nyingine. Natambua tunaweza kuwa na changamoto ya kupata walimu wa hesabu na sayansi kukidhi mahitaji ya shule zetu lakini tukiamua hii changamoto tunaishinda. Kuishinda hii changamoto serikali inaweza kutangaza nafasi za kazi za ualimu wa hayo masomo duniani. Mtu yeyote kutoka nchi yeyote anayeyamudu hayo masomo aruhusiwe aje apate kazi, na viza yake isiwe na urasimu kuipata. Kuwe tu na screening ya uhakika ili isitumike kama uchochoro wa raia wa nchi zingine kuja kufanya yao Tanzania.

  • Nchi ya Korea ya kusini ina utaratibu wa watu kutoka mataifa ambayo English ni lugha ya nyumbani kuruhusiwa kwenda kufundisha kiingeeza huko. Ukiwa na passport ya hizo nchi unapata viza ya kwenda kufundisha kiingereza. Kwa nini Tanzania tusifanye hivyo.

  • Malengo ya nchi, rais akiingia madarakani lazima ayafuate.
  • Kwa sababu tumeamua kama nchi kufikia uchumi wa juu, itungwe sheria ya kumtaka kila rais anayeingia madarakani ayatekeleze malengo ya nchi. Rais hatakuwa na uwezo wa kuiendesha nchi anavyotaka yeye. Awe na job description kabisa kwamba watanzania wamejiwekea malengo haya hivyo ukiingia madarakani lazima uyatekeleze, ukienda kinyume na hayo malengo bunge linakutoa kwenye hicho kiti cha urais na makamu wa rais anachukua usukani au uchaguzi mwingine unafanyika. Katiba itaweka wazi kipi ni bora zaidi kati ya kufanya uchaguzi au makamu wa rais kushika madaraka.

  • Ili kuhakikisha hili linafanyika, inaweza kuundwa taasisi huru ambayo itakuwa inahakikisha rais anafuata katiba. Unajua sisi watanzania ni wapole sana. Tunaweza kuwa na katiba bora kabisa ambayo imeainisha mambo yote yanayotakiwa kutekelezwa na rais, na tukawa na taasisi amabayo jukumu lake ni kuhakikisha katiba haivunjwi. Lakini pamoja na kuwa na hivi vyote unaweza kukuta rais bado anavunja katiba na hiyo taasisi iliyoundwa kumuwajibisha rais haimfanyi chochote, na raia nao washatishwa kupigwa kipigo cha mbwa koko wamefyata hata kuandamana kushinikiza katiba ifuatwe hawawezi. Sasa nini kifanyike, labda inaweza kutungwa sheria inayotambua huu woga na udhaifu wa watanzania ikasema kwamba “Pale rais au kiongozi yeyote wa juu serikalini anapovunja sheria au anapoenda kinyume na mipango iliyaoanishwa kwenye katiba, raia yeyote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana haki ya kufungua kesi katika mahakama za kimataifa ili kushikikiza katiba ifuatwe na kumwajibisha rais au kiongozi aliyevunja katiba au aliyeenda kinyume cha malengo yaliyoainishwa kwenye katiba”

  • Kwa muktadha huu mahakama za kimataifa zitakuwa zimearifiwa kuhusu katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo zitakuwa na mamlaka yaku-prosecute kesi ya namna hii itakapoletwa mbele yake. Kuna watu wataanza kusema Konda msafi wewe sio mzalendo, rais wetu ashitakiwe nje tena? hapana mimi ni mzalendo, najaribu tu kuwa realistic. Haya ni mawazo tu ambayo yanaweza kufikiriwa kuingizwa kwenye katiba na sio lazima yaingizwe, huenda kukawa na mawazo bora zaidi ya haya ambayo yatasaidia kuhakikisha katiba inalindwa na malengo tuliyojiwekea kama nchi hayatelekezwi.

  • Rais kuachana na mambo ya uchama akiwa madarakani
  • Kwa sababu tumeamua kupiga kazi kwa ajili ya nchi yetu. Uchaguzi ukiisha na rais akatangazwa katiba imzuie rais kushabikia hadharani mambo ya chama chake badala yake awatumikie wananchi. Mambo ya mipasho kuwananga wapinzani yasiwepo, kauli za kuwagawa wananchi kwa misingi ya chama zisiruhusiwe. Rais ni rais wa raia wote na sio rais wa chama kilichompa ticketi ya kuwania urais. Mambo ya chama atayaongea akiwa kwenye vikao vya chama chao lakini anapokuwa nje au kwenye ziara za kikazi hataruhusiwa kuongea mambo ya kichama. Atatakiwa awe na kazi ya kuhamasisha umoja, ushirikiano na uzalendo na kutekeleza malengo yaliyoainishwa kwenye katiba.

  • Sheria kandamizi
  • Ili tufike tunakotaka, sheria kandamizi zote zifutwe. Sheria zina nafasi kubwa sana kwenye kuleta maendeleo. Sheria zote zinazokwamisha maendeleo zifutwe. Sheria zote kandamizi zifutwe. Mojawapo ya sheria kandamizi ambazo binafsi ningependa zifutwe ni hizi: sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii NSSF na PSSSF. Kumpangia mtu namna ya kutumia hela yake, hii sheria ni kandamizi. Fao la kujitoa lirudishwe. Mfanyakazi akiachishwa kazi au akiacha kwa hiari yake apewe hela yake ikamsaidie mambo yake. Haya mambo ya kumzuia kuchukua hela yake mpaka uzeeni hayafai. Apewe hela yake ili kama anataka kufanya biashara akafanye akatengeneze ajira. Sheria nyingine kandamizi ni hii ya kufungwa miaka 30 jela ukimpa ujauzito mwanafunzi. Hii sheria ukiachilia kuwa ni kandamizi pia inamnyima haki mtoto atakayezaliwa haki ya kulelewa na wazazi wake wote wawili. Unapomfunga baba wa mtoto huoni kama unakitesa kiumbe kisichokuwa na hatia? Baba ake mmemfunga, huyo mtoto atahudumiwa na nani? Mama mjamzito atahudumiwa na nani? Zaidi ya yote unapomfunga baba wa mtoto unapata faida gani? Sheria kandamizi zipo nyingi, hizi mbili ni mifano tu.
  • Karibuni tujadiliane, ushauri na mapendekezo. Tanzania ni yetu sote. Kazi ieendelee.
unazunguka mbuyu dawa ni katiba mpya bila katibba mpya hakuna uchumi maana ccm ni walewale mchwa.
 
Hizo pesa za kuwapa watu wale Ili watuandikie Katiba,ni kupoteza pesa ya umma tu,Katiba haileti maendeleo,inahitajika na utashi wa kisiasa,
Kenya Wana Katiba nzuri Afrika,mbona hakuna maendeleo,China,Russia,North Korea hakuna Katiba "nzuri"lakini nchi zimeendelea sana,sie tuna hitaji viwanda,sio vyerehani na upuuzi wa kusema kila mkoa una viwanda 100!!
Kama music industry ilivyofanikiwa,tufsnye na sekta zingine ziwe hivyo,mifsno ya kuiga ipo Mingi,Dubai,Philippine,malaysia,Japan,Korea,china,hii nchi inakosa utashi wa kisiasa tu,
Watu wanapenda chama kuriko nchi.haya mavyeo ya kupeana hayawezi kutusaidia,kwanza inabidi yafutwe.
RC hana kazi yoyote zaidi ya kuwa nyapara tu,
Tanzania tuliwahi kuwa na viwanda vya radio,betri,sana za kilimo,pale kibaha tulikuwa tuna assembling plant ya scania miaka ya 90!sasa hv tunayo skilled labour kwanini hatuna viwanda vya magari,compyuta,Tunaishia kuagiza china!?
Serikali inabidi isaidie kuanzisha hivi viwanda sio serikali inaenda kuanzisha kiwanda Cha kusaga unga wa lishe!
Ni vizuri kuwa na katiba nzuri; lakini nadhani watu wanachanganya mambo na kudhani kwamba hiyo katiba ndiyo itakayosababisha nchi ipate maendeleo.

Sijui hii dhana wanaitoa wapi?

Umefanya vizuri sana kuweka mifano ya nchi kadhaa hizo hapo juu ambazo zimepiga hatua ya kujipatia maendeleo bila ya kuwa na katiba nzuri.

Ni vizuri pia kwamba umetoa mifano ya viwanda vilivyowahi kuanzishwa Tanzania. Laiti kama viwanda hivi vingefanikiwa tungekuwa tumepiga hatua kubwa sana wakati huu. Hapa haina maana kwamba viwanda havikufanikiwa kwa sabau hatukuwa na katiba nzuri.

Uongozi wa nchi yetu, hasa Rais, anatakiwa sasa kutuliza akili sana na kuweka mkazo katika kufanya mambo machache yaliyo ya muhimu sana ili tuweze kusonga mbele haraka.

Mtaji uliopo wa wananchi wetu, nguvu kazi yetu ndiyo nyenzo muhimu kabisa ya kwanza kutupeleka mbele. Ni lazima tutafute njia zilizo bora kuutumia ipasavyo mtaji huu kabla ya mengine yote. Maovu yanayofifisha nguvu za mtaji huu, kama rushwa na mengineyo ni lazima viongozi wetu wayatambue na kuyarekebisha.

Tukianzia hapo, hata huo uwekezaji utakuja na utakuwa wa nmanufaa sana kwa nchi yetu. Lakini kama tunaleta uwekezaji wa kudidimiza juhudi za wananchi wetu, hiyo haitatuondoa kwenye umaskini.
 
Hizo pesa za kuwapa watu wale Ili watuandikie Katiba,ni kupoteza pesa ya umma tu,Katiba haileti maendeleo,inahitajika na utashi wa kisiasa,
Kenya Wana Katiba nzuri Afrika,mbona hakuna maendeleo,China,Russia,North Korea hakuna Katiba "nzuri"lakini nchi zimeendelea sana,sie tuna hitaji viwanda,sio vyerehani na upuuzi wa kusema kila mkoa una viwanda 100!!
Kama music industry ilivyofanikiwa,tufsnye na sekta zingine ziwe hivyo,mifsno ya kuiga ipo Mingi,Dubai,Philippine,malaysia,Japan,Korea,china,hii nchi inakosa utashi wa kisiasa tu,
Watu wanapenda chama kuriko nchi.haya mavyeo ya kupeana hayawezi kutusaidia,kwanza inabidi yafutwe.
RC hana kazi yoyote zaidi ya kuwa nyapara tu,
Tanzania tuliwahi kuwa na viwanda vya radio,betri,sana za kilimo,pale kibaha tulikuwa tuna assembling plant ya scania miaka ya 90!sasa hv tunayo skilled labour kwanini hatuna viwanda vya magari,compyuta,Tunaishia kuagiza china!?
Serikali inabidi isaidie kuanzisha hivi viwanda sio serikali inaenda kuanzisha kiwanda Cha kusaga unga wa lishe!
Mawazo yako ni mazuri sana. Basi badala ya katiba zitungwe sheria zitakazosimamia hayo malengo mazuri uliyoyataja, na kuwekwe utaratibu ambao utahakikisha sheria zinafuatwa.
 
Ninakumbuka wakati wa ukoloni Tanga ulikua mji wa neema. Kulikua na ajira bandarini, railways, mashamba ya mikonge, ajira za majumbani nk.

Wahindi waliuza bidhaa kutoka Ulaya, Asia, hata Unguja. Watu walitoka Burundi, Mozambique nk kutafuta maisha Tanga.
Nyerere aliongeza viwanda, kulikua na kiwanda cha chuma, mbolea, sabuni, mafuta ya ngozi.

Kilichobadilika ni uongozi tu lakini Tanga bado ni ile ile. Wahindi wamepakimbia na Wazungu anaemaliza mkataba wake wa kazi aliondoka kimya kimya.
 
Ninakumbuka wakati wa ukoloni Tanga ulikua mji wa neema. Kulikua na ajira bandarini, railways, mashamba ya mikonge, ajira za majumbani nk.

Wahindi walikaa bidhaa kutoka Ulaya, Asia, hata Unguja. Watu walitoka Burundi, Mozambique nk kutafuta maisha Tanga.
Nyerere aliongeza viwanda, kulikua na kiwanda cha chuma, mbolea, sabuni, mafuta ya ngozi.

Kilichobadilika ni uongozi tu lakini Tanga bado ni ile ile. Wahindi wamepakimbia na Wazungu anaemaliza mkataba wake wa kazi aliondoka kimya kimya.
Unadhani nini kifanyike turudi tena huko? Unadhani nini kifanyike Tanzania tufike level za mataifa ya ulaya ya magharibi?
 
Wakati nipo sekondari nilikuwa natamani niwe sehemu ya watunga sera za nchi au kuwa kiongozi serikalini, na hii ilisababishwa na jinsi nilivyokuwa naona mambo yanavyoendeshwa nchini. niliona bila kuingia ndani ya siasa siwezi kubadirisha chochote, nitabaki kuwa mtazamaji tu, kama kuna mambo hayapo sawa na ninahitaji kuyabadirisha sina budi kuingia jikoni na hii ndoto nahisi siku moja itakuja kutimia. Mniombee.

Kwa sasa kila nikiiangalia nchi yangu naona inahitaji viongozi wenye maono na mikakati isiyoyumba ili kuipeleka Tanzania katika ulimwengu wa
Kila ninavyozidi kusoma naona jinsi ulivyojaribu kupinpoint our failures kama nchi so painful.otherwice nice paperwork
 
Kijana story yako nzima inaonesha kuna elements za kawivu wivu hivi.

Sasa hatuwezi kuchukua story kama hii tukampa Rais.

Vipi khumbu baada ya kifo chake ulienda kuhani familia?

Khumbu alikuwa na makalio ya kuning'inia hivi ( hahahaha)
 
Kijana story yako nzima inaonesha kuna elements za kawivu wivu hivi.

Sasa hatuwezi kuchukua story kama hii tukampa Rais.

Vipi khumbu baada ya kifo chake ulienda kuhani familia?

Khumbu alikuwa na makalio ya kuning'inia hivi ( hahahaha)
Mkuu hapa tunajadili mambo muhimu. Mambo ya Khumbu si pahala pake hapa.
 
Wakati nipo sekondari nilikuwa natamani niwe sehemu ya watunga sera za nchi au kuwa kiongozi serikalini, na hii ilisababishwa na jinsi nilivyokuwa naona mambo yanavyoendeshwa nchini. niliona bila kuingia ndani ya siasa siwezi kubadirisha chochote, nitabaki kuwa mtazamaji tu, kama kuna mambo hayapo sawa na ninahitaji kuyabadirisha sina budi kuingia jikoni na hii ndoto nahisi siku moja itakuja kutimia. Mniombee.

Kwa sasa kila nikiiangalia nchi yangu naona inahitaji viongozi wenye maono na mikakati isiyoyumba ili kuipeleka Tanzania katika ulimwengu wa kwanza. Nchi za Ulaya na Amerika ya kaskazini hazijaamuka tu siku moja zikawa pale zilipo. Viongozi wake walikuwa na maono na mikakati isiyoyumba, na kila rais au kiongozi aliyekuwa anapata dhamana ya kuongoza alikuwa anatembea mle mle kwenye yale maono na mikakati iliyowekwa na watangulizi wake. Kama wao waliweza kuwa ulimwengu wa kwanza kwa nini sisi watanzania tushindwe ukizingatia sisi tuna rasimali za asili nyingi kuwazidi wao, tuna hali ya hewa nzuri, tuna ardhi inayomea kila aina ya mmea.

Natamani Tanzania iwe nchi ya kwanza Africa kufikia uchumi wa kwanza. Hili lipo ndani ya uwezo wetu watanzania, ni swala la kuamua tu na kujifunga mkanda.

Naomba tujadili kidogo nini kifanyike, hii ni nchi yetu, hatuna nchi nyingine zaidi yahii.

Binafsi vifuatavyo ni baadhi ya mambo ambayo yakifanyika Tanzania inakuwa ni miongoni mwa nchi za ulimwengu wa kwanza.

  • Lazima tupate katiba nzuri inayokwenda na wakati tulionao
  • Kwenye katiba kuanishwe malengo ya muda mrefu na ya muda mfupi.

  • Moja ya malengo ya muda mfupi yanaweza kuwa mengi ila nitataja machache ambayo tunaweza kuanza nayo kama nchi, i. kuhakikisha serikali inakuja na sera za kuondoa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana. Hapa serikali inatakiwa kuja na mikakati ya kuchochea uwekezaji kutoka ndani na nje. Kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ili kutengeneza ajira. Serikali inaweza kutoa incentives kwa wawekezaji. Hii inaweza kuwa katika mfumo wa kupunguza kodi au kupunguza gharama za uagizaji wa mitambo ya viwandani, au serikali inaweza kutoa asilimia flani ya kusaidia manunuzi ya mtambo wowote utakaonunuliwa na muwekezaji atakayekuwa tayari kujenga kiwanda flani. Kwa mfano serikali inahitaji muwekezaji kwenye kiwanda cha mafuta ya kupikia au sukari kwa sababu kuna upungufu wa hizo bidhaa nchini. Serikali inaweza kutangaza kwamba muwekezaji mzawa atakayejenga kiwanda cha sukari au mafuta ya kupikia, serikali itachangia asilimia 25 ya gharama ya huo mtambo. Au serikali inaweza kutangaza kwamba kampuni yeyote itakayoweza kuajiri wafanyakazi kuanzia 20,000 haitalipa tozo ya Skill Development Levy (SDL). Hii ni mifano tu, watunga sera watatakiwa wewe wabunifu wa kubuni njia ambazo zitasaidia kuchochea ajira

  • ii. Lengo jingine la muda mfupi linaweza kuwa hili; Hizi nafasi za uteuzi zenye mishahara mikubwa kama ukuu wa mikoa, ukuu wa wilaya, ukatibu mkuu, ukatibu tawala na zingine zote zinazoshabihiana na hizi zitumikiwe kwa miaka miwili tu ili kuwapisha wengine. Sio mtu mmoja anakuwa kwenye hizo nafasi kwa muda mrefu. Wewe kama upo kwenye hizo nafasi na let’s say unapata mshahara wa milioni 4 kwa mwezi kwa muda wa miaka 2 utakuwa umetengeneza 96,000,000. 96,000,000 inakutosha sana kwenda kuanzisha biashara au uwekezaji na ukasaidia kutoa ajira kwa wengine. Kufikia uchumi wa duania ya kwanza sio lelemama hivyo uwajibikaji inabidi uanzie kwa viongozi wenyewe. Kwa hiyo kukiwa na utaratibu wa kuachiana madaraka na kwenda kuanzisha biashara baada ya kuachia madaraka kunakuwa na multiplier effect kwenye uchumi hususani kwenye kutengeneza ajira maana watanzania wengi wataajiriwa kwenye hizo nyadhifa na pia watanzania wengi wataajiriwa kwenye hizo ajira zitakazotengenezwa na hao viongozi walioachia madaraka baada ya miaka miwili.

  • iii. Lengo jingine la muda mfupi ni hili, au linaweza kuwa la muda mrefu inategemea litadumu kwa muda gani; kwa mfano kwa sasa bei ya sukari na mafuta ya kupikia yamepanda bei karibia 60% hii ilisababishwa na serikali kupiga marufuku uagizwaji wa hizi bidhaa kutoka nje ili kulinda viwanda vya ndani ilihali viwanda vya ndani havina uwezo wa kukidhi mahitaji ya ndani. Madhara yake ni bei ya sukari na mafuta imepanda bei na imeshindwa kushuka licha ya matamko ya viongozi kuwa bei ishuke, na hii bei inamuumiza mlaji wa mwisho. Kama hakuna muwekazaji, serikali inaweza kuanziasha kilimo cha alizeti na karanga na kujenga kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia. Serikali inaweza kuanzisha mashamba ya miwa na kujenga kiwanda cha sukari. Tanzania tuna ardhi yenye rutuba kila mkoa hivyo serikali ikiamua kutatua hii changamoto ya sukari na mafuta ya kupikia haishindwi. Natambua kiuchumi sio afya kwa serikali kujihusisha moja kwa moja kwenye biashara lakini kuna exceptional cases kama hizi, sidhani kama kutakuwa na madhara kama serikali itachukua jukumu la kuzalisha bidhaa ambayo private sector imeshindwa kuzalisha kwa kiwango kinachohitajika nchini. Nadhani huu uwekezaji kwenye hizi bidhaa ni wenye tija zaidi kwa watanzania kuliko uwekezaji wa kwenye ndege. Ndege wanapanda watanzania wachache wenye uwezo lakini sukari na mafuta ya kupikia yanatumiwa na watanzania wote, hivyo unaweza kuona manufaa kwa watanzania kama serikali itaamua kuwekeza kwenye bidhaa ambazo sector binafsi imeshindwa kukidhi mahitaji ya walaji. Pia kama serikali itawekeza kwenye hii miradi itasaidia kutengeneza ajira hivyo tatizo la ajira litazidi kupungua maana kwenye hayo mashamba ya miwa, karanga na alizeti watanzania wataajiriwa, kwenye hivyo viwanda vya sukari na mafuta pia watanzania wataajiriwa.

  • Malengo ya muda mrefu

  • Malengo ya muda mrefu yatakuwepo mengi kulingana na ubunifu wa watunga sera wetu watakaopewa hii dhamana, ila hapa nitataja machache ambayo yanaweza kuwemo kwenye hayo malengo
  • i. Elimu,
  • Hakuna nchi yeyote katika ulimwengu wa kwanza iliyoendelea kiuchumi bila kuweka mifumo mizuri ya elimu, na zaidi ya yote bila kuwekeza kwenye masomo ya sayansi na hesabu. Elimu bora ndio kila kitu kwenye maendeleo. Sasa hivi dunia ipo kwenye ulimwengu wa sayansi na tekinologia, bila elimu tutabaki kuwa wachuuzi tu, hatuwezi kumiliki na kuendesha viwanda vyetu. Kuna rafiki yangu ni raia wa Canada ila ana asili ya kieritrea, ana ndugu zake wa damu Ujerumani na nchi za Scandinavia. Nchi zote hizo amefika na kukaa kidogo. Aliniambia “Africa bila kuwekeza kwenye elimu tutabaki kuwa nyuma siku zote, Africa itapiga maendeleo makubwa ya kiuchumi kama itawekeza kwenye elimu hasa masomo ya sayansi na hesabu”. Alinitolea mfano nchi ya Sweden kama sikosei au the Netherlands ilikuwa masikini sana lakini serikali ilitunga sera na sheria kuhakikisha masomo ya sayansi na hesabu yanakuwa ya lazima, na kuhakikisha wanafunzi kutokea elementary school hadi chuo wanafundishwa vyema, wanapikika na kuiva kwenye hesabu na sayansi. Yalikuwa ni malengo ya muda mrefu lakini baada ya muda matunda yalionekana, na sasa kama mnavyoona hiyo nchi ipo ulimwengu wa kwanza. Anasema hiyo nchi walimu wanaongoza kwa kulipwa mishahara mikubwa. Kwa hiyo sisi watanzania kama tunataka kufika huko lazima tuwekeze kwenye elimu, hakuna short cut ya maendeleo, lazima tuwe na mipango ya muda mrefu ambayo tutakuwa na uhakika kuwa baada ya muda flani tutakuwa level nyingine. Natambua tunaweza kuwa na changamoto ya kupata walimu wa hesabu na sayansi kukidhi mahitaji ya shule zetu lakini tukiamua hii changamoto tunaishinda. Kuishinda hii changamoto serikali inaweza kutangaza nafasi za kazi za ualimu wa hayo masomo duniani. Mtu yeyote kutoka nchi yeyote anayeyamudu hayo masomo aruhusiwe aje apate kazi, na viza yake isiwe na urasimu kuipata. Kuwe tu na screening ya uhakika ili isitumike kama uchochoro wa raia wa nchi zingine kuja kufanya yao Tanzania.

  • Nchi ya Korea ya kusini ina utaratibu wa watu kutoka mataifa ambayo English ni lugha ya nyumbani kuruhusiwa kwenda kufundisha kiingeeza huko. Ukiwa na passport ya hizo nchi unapata viza ya kwenda kufundisha kiingereza. Kwa nini Tanzania tusifanye hivyo.

  • Malengo ya nchi, rais akiingia madarakani lazima ayafuate.
  • Kwa sababu tumeamua kama nchi kufikia uchumi wa juu, itungwe sheria ya kumtaka kila rais anayeingia madarakani ayatekeleze malengo ya nchi. Rais hatakuwa na uwezo wa kuiendesha nchi anavyotaka yeye. Awe na job description kabisa kwamba watanzania wamejiwekea malengo haya hivyo ukiingia madarakani lazima uyatekeleze, ukienda kinyume na hayo malengo bunge linakutoa kwenye hicho kiti cha urais na makamu wa rais anachukua usukani au uchaguzi mwingine unafanyika. Katiba itaweka wazi kipi ni bora zaidi kati ya kufanya uchaguzi au makamu wa rais kushika madaraka.

  • Ili kuhakikisha hili linafanyika, inaweza kuundwa taasisi huru ambayo itakuwa inahakikisha rais anafuata katiba. Unajua sisi watanzania ni wapole sana. Tunaweza kuwa na katiba bora kabisa ambayo imeainisha mambo yote yanayotakiwa kutekelezwa na rais, na tukawa na taasisi amabayo jukumu lake ni kuhakikisha katiba haivunjwi. Lakini pamoja na kuwa na hivi vyote unaweza kukuta rais bado anavunja katiba na hiyo taasisi iliyoundwa kumuwajibisha rais haimfanyi chochote, na raia nao washatishwa kupigwa kipigo cha mbwa koko wamefyata hata kuandamana kushinikiza katiba ifuatwe hawawezi. Sasa nini kifanyike, labda inaweza kutungwa sheria inayotambua huu woga na udhaifu wa watanzania ikasema kwamba “Pale rais au kiongozi yeyote wa juu serikalini anapovunja sheria au anapoenda kinyume na mipango iliyaoanishwa kwenye katiba, raia yeyote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana haki ya kufungua kesi katika mahakama za kimataifa ili kushikikiza katiba ifuatwe na kumwajibisha rais au kiongozi aliyevunja katiba au aliyeenda kinyume cha malengo yaliyoainishwa kwenye katiba”

  • Kwa muktadha huu mahakama za kimataifa zitakuwa zimearifiwa kuhusu katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo zitakuwa na mamlaka yaku-prosecute kesi ya namna hii itakapoletwa mbele yake. Kuna watu wataanza kusema Konda msafi wewe sio mzalendo, rais wetu ashitakiwe nje tena? hapana mimi ni mzalendo, najaribu tu kuwa realistic. Haya ni mawazo tu ambayo yanaweza kufikiriwa kuingizwa kwenye katiba na sio lazima yaingizwe, huenda kukawa na mawazo bora zaidi ya haya ambayo yatasaidia kuhakikisha katiba inalindwa na malengo tuliyojiwekea kama nchi hayatelekezwi.

  • Rais kuachana na mambo ya uchama akiwa madarakani
  • Kwa sababu tumeamua kupiga kazi kwa ajili ya nchi yetu. Uchaguzi ukiisha na rais akatangazwa katiba imzuie rais kushabikia hadharani mambo ya chama chake badala yake awatumikie wananchi. Mambo ya mipasho kuwananga wapinzani yasiwepo, kauli za kuwagawa wananchi kwa misingi ya chama zisiruhusiwe. Rais ni rais wa raia wote na sio rais wa chama kilichompa ticketi ya kuwania urais. Mambo ya chama atayaongea akiwa kwenye vikao vya chama chao lakini anapokuwa nje au kwenye ziara za kikazi hataruhusiwa kuongea mambo ya kichama. Atatakiwa awe na kazi ya kuhamasisha umoja, ushirikiano na uzalendo na kutekeleza malengo yaliyoainishwa kwenye katiba.

  • Sheria kandamizi
  • Ili tufike tunakotaka, sheria kandamizi zote zifutwe. Sheria zina nafasi kubwa sana kwenye kuleta maendeleo. Sheria zote zinazokwamisha maendeleo zifutwe. Sheria zote kandamizi zifutwe. Mojawapo ya sheria kandamizi ambazo binafsi ningependa zifutwe ni hizi: sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii NSSF na PSSSF. Kumpangia mtu namna ya kutumia hela yake, hii sheria ni kandamizi. Fao la kujitoa lirudishwe. Mfanyakazi akiachishwa kazi au akiacha kwa hiari yake apewe hela yake ikamsaidie mambo yake. Haya mambo ya kumzuia kuchukua hela yake mpaka uzeeni hayafai. Apewe hela yake ili kama anataka kufanya biashara akafanye akatengeneze ajira. Sheria nyingine kandamizi ni hii ya kufungwa miaka 30 jela ukimpa ujauzito mwanafunzi. Hii sheria ukiachilia kuwa ni kandamizi pia inamnyima haki mtoto atakayezaliwa haki ya kulelewa na wazazi wake wote wawili. Unapomfunga baba wa mtoto huoni kama unakitesa kiumbe kisichokuwa na hatia? Baba ake mmemfunga, huyo mtoto atahudumiwa na nani? Mama mjamzito atahudumiwa na nani? Zaidi ya yote unapomfunga baba wa mtoto unapata faida gani? Sheria kandamizi zipo nyingi, hizi mbili ni mifano tu.
  • Karibuni tujadiliane, ushauri na mapendekezo. Tanzania ni yetu sote. Kazi ieende
konda msafi
Nakupongeza sana kwa huu Uzi ulioenda shule.

Hakika kama mawazo yako yatachukuliwa "seriously" na watawala wetu, nchi yetu itapaa kimaendeleo
 
unazunguka mbuyu dawa ni katiba mpya bila katibba mpya hakuna uchumi maana ccm ni walewale mchwa.
Nashangaa katiba mpya ,katiba mpya hivi nchi zenye katiba nzuri zinatofauti ganj na sisi ,katiba mpya ni wimbo wa wanasiasi maaana nao wataanza nakumbuka Kwenye sitting allowance , lakini katiba mpya its cannot garantee you food on the table my dear work hard
 
Kondo msafi
Nakupongeza sana kwa huu Uzi ulioenda shule.

Hakika kama mawaz yako yatachukuliwa "seriously" na watawala wetu, nchi yetu itapaa kimaendeleo
Asante sana mkuu. Tanzania ni yetu sote hivyo tuna wajibu wa kuisaidia ili iwe sehemu bora ya kuishi. Wajukuu zetu watakapozaliwa wasije wakaanza kukimbilia Ulaya na Marekani kwa sababu wamekuta Tanzania sio sehemu bora ya kuishi.
 
Nashangaa katiba mpya ,katiba mpya hivi nchi zenye katiba nzuri zinatofauti ganj na sisi ,katiba mpya ni wimbo wa wanasiasi maaana nao wataanza nakumbuka Kwenye sitting allowance , lakini katiba mpya its cannot garantee you food on the table my dear work hard
Basi hata kama sio katiba mpya zitungwe sheria zinazoendana na wakati uliopo, na sheria kandamizi zifutwe.
 
Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na wenye nchi (Watanzania) ipo na tunayo. Wanasiasa kwa maslahi yao hawataki kuipitisha. Kwa kiburi hicho inatakiwa tuwapige chini au wakubaliane na matakwa yetu. Hakuna sababu ya kuanza upya ni kupoteza muda na ni matumizi mabaya ya rasilmali zetu tunazozihitaji kwa maendeleo yetu. Tupeni katiba yetu tuliyomuagiza Jaji Warioba ailete kwenu muipitishe. wanasiasa kumbukeni mliingia mjengoni kwa niaba yetu na si vinginevyo.
Una hoja nzuri sana mkuu. Hebu pendekeza mbinu tutakayotumia ili katiba ya Warioba ipitishwe.
 
Back
Top Bottom