Rais, wananchi wanataka kujua Michango mashuleni imerudishwa? Tunaomba tamko la Serikali

mkamanga original

JF-Expert Member
Jan 21, 2015
614
597
Watoto wa madarasa ya awali na darasa la kwanza hawapokelewi mashuleni mpaka wazazi watoe michango.

Utafiti uliofanyika unaonyesha mzazi wa darasa la kwanza analazimika kuchangia kati ya tsh. 15,000 hadi tsh. 80,000. Wakati wale wa awali michango yao ni kati ya tsh. 20,000 hadi 100,000.

Mbaya zaidi michango yenyewe hawatoi hata risiti wanachofanya walimu kuandika jina tu kwenye daftari.

Serikali ilishatoa maelekezo na waraka wa uchangiaji lakini mwaka huu ni kama waziri mwenye mamlaka haoni kinachoendelea kwenye shule zake.

Mfano wa michango inayochangishwa ni ujenzi wa madarasa, chakula na madawati. Taasisi zake rais zifanye kazi, shule za serikali hazipaswi kuwakataa wanafunzi kisa umaskini wa mzazi.

Hii wizara ni bora angepewa Mh.Lukuvi kwa sababu anafuatilia mpaka kwenye grassroot lakini Jaffo na Ngalichako wamepoa mno ,hata hawajui kama wazazi wanakataliwa kupokelewa watoto wao kisa mchango.

Ningeweka baadhi ya risiti hapa za wazazi ambao nilibahatika kupata nakala ,lakini naona kila nikijaribu kuattach zinagoma, michango katika shule za msingi nimerudi kwa kasi
 
Sema wewe ndiyo unataka kujua wananchi gani waliokutuma uwasemee?

Michango hata ulaya watu wanatoa kwa maendeleo jinga wewe kama huna tulia siyo kuleta uchochezi humu.
 
Acha umbeya! Taja shule ndio tujadili hoja yako.

Pili michango ya chakula ni kwa AFYA YA MWANAO ANAYESHINDA TANGU ASUBUHI HADI JIONI BILA KUTIA KITU TUMBONI! Kama ni wa kike subiri vijana wamfanyie mazoezi sababu ya njaa! Kama ni wakiume malizia mwenyewe.

Kikubwa wanaosimamia hili ni kamati za shule zilizoundwa na wazazi na sio waalimu
 
Watoto wa madarasa ya awali na darasa la kwanza hawapokelewi mashuleni mpaka wazazi watoe michango...
Mkuu inaonesha una sababu zako nyuma ya pazia. Ikiwa Huna ushahidi unafanya uchochezi. Hiyo michango ni Kwa ajili ya nini na Nani walikubaliana, ni wazi wenyewe au walimu ndo wameibua wenyewe? Ni vema ukawa na maelezo yaliyojitosheleza
 
Tutajie hizo shule Ili na sisi wananchi tujue wapi tumekosa watendaji wanaweza kutekeleza maagizo ya serikali.
 
Hii wiki imekuwa ya vilio kila kona wazazi wa watoto wanaosoma shule za Kayumba wakilalamikia utitiri wa michango mashuleni.

Nikiwa Mwanachama wa CCM ningewataka Waziri wa Tamisemi Mh Jafo na Waziri wa elimu Prof Ndalichako waache kutegeana au kuviziana watoke hadharani wawaeleze wazazi kama michango imerudi mashuleni.

Tena mtoke haraka kabla ya suala ya Ijumaa kesho kutoa ufafanuzi.

Yanga oyeeee.

Maendeleo hayana vyama!
 
Back
Top Bottom