Hivi karibuni tumeshuhudia Rais wa Zanzibar akiapishwa na Jaji Mkuu kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri kama Katiba inavyosema, swali langu kwenu wasomi wa Sheria ni kuhusu uhalali wa kitendo hicho kisheria na kikatiba! Je hapo Katiba haijabakwa? mimi nadhani wajumbe wa Baraza la Mawaziri huapishwa na Mwenyekiti wao, sasa huyu atakuwa mjumbe gani ambaye hajaapa utii kwa bosi wake?