MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Kuna Mtu wako Mmoja wa karibu mno hasa kutoka Wizara uliyokuwa ukiiongoza huku Tanzania Bara kwa muda mrefu kanidokeza ya kwamba Role Models wako wakubwa Kiuongozi na ambao unawakubali sana ni aliyekuwa Rais wa Marekani Barrack Hussein Obama na Rais Mstaafu wa Tanzania kwa Awamu ya Nne Mzee Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.
Sikatai Mtu kuwa na Role Model au Role Models wake duniani kwani hata Mimi pia nilitamani kweli kweli kuwa kama Mchezaji wa Kifaransa japo ana Uraia wa nchi uliyowahi Kusoma pia ya Algeria Zinedine Zidane 'Zizzou' lakini nikajikuta sijafikia Malengo ya Kumuiga na kuwa kama Yeye hadi sasa nipo zangu tu hapa Kisiwani Pemba na Kazi yangu hii ya Kupara Samaki na Uvuvi pekee.
Mheshimiwa Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa takribani Mwezi sasa tokea uwe Rais huko nimeanza Kukuona ni Mtu unayependa sana Makamera na Kutupia Vitu vyako/ Mambo yako Mitandaoni. Na leo tena nimeona umetupia Picha uko ndani ya Ndege angani ukisoma Faili moja hivi kama vile alivyowahi kufanya Mzee Mwinyi na hata Rais Mstaafu wa Marekani Obama.
Ushauri wangu Kwako Mheshimiwa hebu punguza sana hizi mambo na fanya Kazi ngumu Kwanza ya Kuijenga vyema Zanzibar Isles, waunganishe vyema Wazanzibari na kazania mno masuala mazima ya Uchumi na Elimu zao na huko baadae Zanzibar yako ikikaa sawa sasa unaweza hata kuwa unatutupia Picha zako zingine ukiwa Dinning Room na Mkeo Bi. Mariam mnakula Kuku.
Na kuna Mtu Mmoja hivi wa juu yako Yeye mambo hizi huwa hapendi kwakuwa anataka awe Maarufu Yeye tu nchi nzima. Kuwa makini nae kabisa!
Sikatai Mtu kuwa na Role Model au Role Models wake duniani kwani hata Mimi pia nilitamani kweli kweli kuwa kama Mchezaji wa Kifaransa japo ana Uraia wa nchi uliyowahi Kusoma pia ya Algeria Zinedine Zidane 'Zizzou' lakini nikajikuta sijafikia Malengo ya Kumuiga na kuwa kama Yeye hadi sasa nipo zangu tu hapa Kisiwani Pemba na Kazi yangu hii ya Kupara Samaki na Uvuvi pekee.
Mheshimiwa Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa takribani Mwezi sasa tokea uwe Rais huko nimeanza Kukuona ni Mtu unayependa sana Makamera na Kutupia Vitu vyako/ Mambo yako Mitandaoni. Na leo tena nimeona umetupia Picha uko ndani ya Ndege angani ukisoma Faili moja hivi kama vile alivyowahi kufanya Mzee Mwinyi na hata Rais Mstaafu wa Marekani Obama.
Ushauri wangu Kwako Mheshimiwa hebu punguza sana hizi mambo na fanya Kazi ngumu Kwanza ya Kuijenga vyema Zanzibar Isles, waunganishe vyema Wazanzibari na kazania mno masuala mazima ya Uchumi na Elimu zao na huko baadae Zanzibar yako ikikaa sawa sasa unaweza hata kuwa unatutupia Picha zako zingine ukiwa Dinning Room na Mkeo Bi. Mariam mnakula Kuku.
Na kuna Mtu Mmoja hivi wa juu yako Yeye mambo hizi huwa hapendi kwakuwa anataka awe Maarufu Yeye tu nchi nzima. Kuwa makini nae kabisa!