Rais wa Uruguay José Mujica, ndiye Rais anayeishi maisha duni kuliko wote duniani

Pamoja na misingi mizuri kama taifa, fisadi lazima atatengeneza njia ya kuiba. Unafikiri ni kwa nini awe huyu na sio mtangulizi wake? Huyu jamaa ana kitu cha ziada ambacho kinang`arishwa zaidi na ubora wa utamaduni wa taifa lao. Hata timu yao ya soka imeingiza msamiati ktk soka la kimataifa; kwa wanasoka, kinakitu huwa tunasema, timu imecheza kama Urugway.

Kwa hiyo jamaa wanapoona jamaa hana ac Uswisi na mshahara wake anagawa kwa maskini wanadhani jamaa ni lofa sana, hata nyumba anayosema anaishi, inamilikiwa na mkewe. Urugway inachanja mbuga kuelekea nchi ya maziwa na asali. Huku Bongo meneja mwadilifu tunamcheka sana mitaani, hapa ndipo ilipo tofauti.
 
Inamana rizone anaweza mzidi kwa cash? vp yeye hana malori? jakaya kashamtembelea au rais wetu ataki maskini.

Sijui kama wanaweza kulinganishwa hawa watu wawili. Kwa wenzetu kila kitu kiko wazi kabisa. Hatuko Urugway lakini kwa msaada wa network tumejua kuwa jamaa ana miliki nini, sasa huyu wa kwetu hata sijui anamiliki nini hata kama tuko mtaa mmoja !!!!!!
 
Pato lake halali ni zuri kiasi kwamba hahitaji kulimbikiza mimali, na amesema, akisha maliza muda wake wa uongozi anarudi kuchunga ng`ombe shambani kwake. Tatizo la wanadamu ni kwamba wengi hawajui wanataka nini. Kuku ngendu alikuwa na jumba kando ya ziwa Geneva la vyumba kibao, lakini aliishia kupigwa chepe Morocco kienyeji. Furaha ya kweli na uhuru wa kweli, na amani ya kweli ni bidhaa muhimu sana kwa maisha ya mtu mwenye akili timamu, huyu jamaa kafanikiwa sana kufikia hivi vitu vitatu.
Mimi binafsi nampongeza!!
 
Umesahau vitu vingi ktk hadithi yako hii, moja hujasema mkewe anafanya nini? Mkewe ni senetor ktk bunge/uongozi wa nchi hiyo, pili, huyu jamaa ana shamba kubwa la ng`ombe wa maziwa. Nchi hiyo ina-export bidhaa za maziwa nje. Tatu nchi ile ina wahamiaji wengi sana toka nje ya bara la America kusini. Na mwisho ni nchi yenye idadi ndogo sana ya watu, na wengi wanazalisha kwa njia ya kilimo kwa scale kubwa akiwemo Rais mwenyewe.

Kwa hiyo utaona kwamba hawa wahamiaji ( most Wadachi, japanese) wamekuwa na mchango mkubwa sana ktk mafanikio ya nchi ile. Na jioni wote wanaburudika na soka la vijana wao. Wenyewe wanasema ile ni Switzerland ya America Kusini.

hata rais wetu ni masikini sana zaidi ya huyo unayemsifia
 
hata rais wetu ni masikini sana zaidi ya huyo unayemsifia

Sijamsifia mtu, nimetoa kilicho ktk maandiko yaliyotolewa na bbc leo. Pili nimejazia maandiko ya mtoa mada mkuu, soma vizuri mchango wangu.
 
Umeambiwa Huyu Mujica anatoa 90% ya mshahara wake kwenda kusaidia wenye dhiki. Huwezi kuishi maisha haya ukaupata huo utajiri wa kutupwa wa huyo warren. Kwa upande mwingine, hakuna makuu kuliko kuwa na huo utajiri wa kutupwa wakati umezungukwa na watu wasiomudu hata mlo mmoja kutwa. Kwa lugha rahisi, ni ushetani.

huyo warren buffet ni tajiri wa tatu,ila kuna kipindi alikua namba moja.alitoa karibia robo ya utajiri wake kwa mfuko wa bill gate foundation ,unaohusika na utafiti wa chanjo za magonjwa kama malaria na HIV AIDS.
Anaishi nyumba ya kawaida,hana hata simu ya mkononi.ofisini kwake hakuna hata computer.
 
300089_10150318586135942_1905171732_n.jpg
 
Yericko rais wetu anasingiziwa tu wala sio tajiri coz anavijumba vya kawaida pale Msoga vimejengwa kwa msaada wa S.Patel (kama Nyerere alivyojengewa na JW). Kile kighorofa cha Regent any civil servant can build.

Rais JK sio mfanyabiashara, ni mkulima wa mahindi na mananasi.

Vibiashara vingi mnavyovisema ni vya mwanae ambaye nasikia ni mzuri sana wa kuandika proposal ndio maana anapata tender nyingi za serikali.
Hata ile kampuni yake ya uwakili RGK (share na binti wa Karume) inapata kazi serikalini kwa vile kampuni nyingi zimekuwa haziisaidii ipasavyo serikali yetu.

Nasikia wasaidizi wake ndio wanapenda pomps, ila yeye hana makuu. Ukiona kavaa suti ya gharama sana basi kuna uwezekano mkubwa kapewa tu hajanunua yeye..

Rais wetu sio tajiri...



uko serious!!!?????...............najizuia sana kukutukana hapa,kama kweliuko serious!!!

  • A%20S%20angry.gif

 
uko serious!!!?????...............najizuia sana kukutukana hapa,kama kweliuko serious!!!
Rubuye123 tukana tu ila ukikutana na BAN usinilaumu.
ILA Ukinitukana utakuwa unanionea tu...na ukiacha utakuwa umeniogopa.....hahahahahaa!!!!!!

Ila kwa vile jibu langu lilikuwa limeelekezwa kwa Yericko nadhan yeye amenielewa iwapo nilikuwa siriaz au la!!!!
 
Rubuye123 tukana tu ila ukikutana na BAN usinilaumu.
ILA Ukinitukana utakuwa unanionea tu...na ukiacha utakuwa umeniogopa.....hahahahahaa!!!!!!

Ila kwa vile jibu langu lilikuwa limeelekezwa kwa Yericko nadhan yeye amenielewa iwapo nilikuwa siriaz au la!!!!


eephhhewwww.....................nimesoma katikati ya mistari na nadhani nimeelewa!huwezi kumuelezea ''huyu jamaa'' kwa namna hii,usipigwe hata vibao aisee!

halafu kumbe nafanya makusudi kumbe unajua nitaogopa ban....poa tu bana!basi nimekuogopa....furahi sasa!!!
 
Rais Jose akishuka kwenye gari lake, kwenye nyumba yake ya kawaida. Wanaoonekana pembeni ni wasaidizi wake wa idara ya ulinzi (Picha kutoka Mtandao)

<tbody>
</tbody>





MARA zote nafasi ya kuongoza nchi, kuwa rais, ni mwanga wa maisha bora, chumo la uhakika wa kula, kulala, kunywa, kutibiwa, kukaa kwenye mahekalu, kuheshimiwa hata kama huna busara wala visheni, kuhukumu (ikiwamo kunyonga) hata kwa uonevu, na mambo mengine.


Elimu kwa watoto wa rais, hata wale anaowalea hutolewa bure, tena kwa shule wanazochagua ama watoto au baba au mama yao ambaye anakuwamadarakani wakati huo.


Kimsingi, mambo haya yooote ni bure kwa rais, mke (au wake zake, wakiwamo wale wa nyumba ndogo), watoto wake, ndugu na hata jamaa wa karibu.


Hivyo, unapokuwa rais unakuwa na nafasi ya kulelewa kama mtoto mchanga, wakati mwingine unachaguliwa hata nguo na hata viatu vya kuvaa, pia unachaguliwa hata hata mahali pa kwenda, watu unaoshirikiana nao na wale wa kushikana nao mikono kwa salamu.


Ni kutokana na hili, mtu anapokuwa rais, ujira wake, kwa maana ya mshahara, unakosa pa kwenda. Tambua kwamba katika nchi zetu za Afrika, nyingi zikiwa zinaogelea kwenye umasikini wa kutupwa, hata wazazi wa rais na wasaidizi wake wa karibu, wanalindwa, wanalishwa, wanatibiwa na kusafiri bure kokote wanakokwenda. Yawezekana hili haliko kisheria, lakini kujipendekeza na woga wa watendaji wengine chini ya rais wanalifanya lionekane limo kwenye vitabu vya sheria.


Nimefurahi sana baada ya kukutana na huyu Rais wa Uruguay, Jose Mujica, ambaye ana maisha na historia ya kiongozi pekee, mkuu wa nchi ambaye anapenda sana maisha ya kawaida kabisa, maisha ya kuwahurumia wengine na kujitahidi kuonesha kwa vitendo.


Rais huyo, huwezi kuamini ndiye kiongozi mwenye ufukara mkubwa zaidi ya watu anaowaongoza. Kwamba yeye ni miongoni mwa wananchi wanaioshi maisha ya kawaida, tena mara nyingi akishirikiana nao kwa shughuli za ujenzi wa taifa, ikiwamo ujenzi wa barabara, kulima mashamba ya mfano na zaidi sana kutibiwa nao. Huyu ni yule kiongozi anapougua anawahi kupanga mstari ili kuwahi kuona daktari, akichelewa anapanga mstari kusubiri zamu yake.


Ni rais pekee ambaye ameamua kutoa mshahara wake kwa zaidi ya asilima 90 kugawana na watu masikini wa nchi yake, kwamba fedha hizo huingizwa katika vikundi mbalimbali vya maendeleo.
Baada ya kuingia madarakani, aligoma kuhamia Ikulu na anaendelea kuishi kwenye nyumba yake na mkewe, nje ya Ikulu, akiwa anapakana na wananchi wa kawaida ambao wengi ni wafanyabiashara wadogo na wakulima.


Akiwa amepangiwa na bunge kupokea (kwa fedha za Tanzania) shilingi milioni 15 kwa mwezi, hajawahi kupokea fedha hizo na ameiamuru Hazina kuzipeleka fedha hizo kwa wananchi masikini. Yeye hupokea shillingi milioni 1.6 tu, tena hizi akizitumia kwa ajili ya mafuta ya gari lake alilonunua na mkewe aina ya Mgongo wa Chura, yaani VW Beetle, hiyo hapo pichani.


“Niko mimi na mke wangu, wawili tu, gari kubwa la nini, sina haja nalo, sitaki kuwaibia wananchi, kunichagua tu kuwaongoza ni sifa pekee, tena kubwa inayokaribia utukufu wa kawaida, sasa zaidi ya hapo nini…


Nahitaji sana kuwatumikia wananchi wa Uruguay, siyo kuwanyonya wala kuwaibia au kuwa mwanya wa kuchuma na kujifurahisha mimi, mke wangu, watoto wangu na ndugu zangu, sioni haja hiyo na sitaki kuwa mnyonyaji kamwe,” anasema Rais Jose.


Rais Jose ndiye mkuu wan chi pekee duniani ambaye amekataa kuwa na akaunti benki, hana deni, hataki kuwa na bima ya aina yoyote na anasema anataka kufa akiwa na sifa ya utumishi uliotukuka.
“Nikiwa na akaunti benki, nikiwa na magari makubwa, nitakuwa nakaribisha ushawishi wa kuwa mwizi, kuwaibia wananchi wangu, sitaki chochote,” anaongeza.


Mujica, mke wa Rais Jose, tofauti ilivyo na wake za wakubwa wetu huku Afrika, hajipambi kwa dhahabu, almasi na wala harembeshwi na vito vya thamani, anasema maisha ya kawaida ndiyo sala yake na mumewe, full stop.


Rais Jose ambaye ana miaka 77, anaeleza kuwashangaa wakuu wenzake wan chi ambao wamegeuka kuwa wezi licha ya kulipwa fedha nyingi ikiwa ni mshahara, kula rushwa, kujilimbikizia kila aina ya mali, kwa jasho la waliowachagua na kuwapa madaraa makubwa.


Katika Tanzania, inaelezwa kuwa rais wake anapokea mshahara unaoonekana kwenye karatasi kuwa milioni 10, lakini marupurupu yake yanaweza kugota milioni 41/- kwa mwezi na kama ilivyo kawaida, anakula bure, analala bure, anatibiwa bure, watoto wake wanasoma bure shule anazopenda baba au mama, na marupurupu mengine yanayoonekana na yasiyoonekana.


Tujiulize, ni lini Tanzania itakuwa na kiongozi, walau atakayemkaribia Rais Jose wa Uruguay? Je, ni huyu ajaye baada ya Rais Jakaya Kikwete au huyo atakayemfuatia au yule mwingine?


Uhakika ni kwamba Watanzania, hawahitaji kuwa na rais mwenye umasikini wa kutupa na anayeishi kimasikini sana, lakini angalau basi atakuwa tayari kuonesha, tena hata tukimwangalia kwa macho makavu, tuone kabisa mboni zake zatueleza kuwa anawalilia wananchi wake, wengi wakishindwa kula mara mbili kwa siku.


Katika Tanzania, uchunguzi uliofanywa na Shirika la Care, umeonesha wananchi wengi nchini wanakula mara moja tu kwa siku, tena chakula ‘kisichoeleweka’.




Tafakari
 
Hiyo itabaki kuwa ndoto...watu wanaosema "Hata kama ni nyasi mtakula,lakini ndege ya Rais lazima inunuliwe", usitegemee kabisa kutumia mgongo wa kobe.
 
Hata akiishi kwa ufukara...atapimwa kwa maendeleo aliyowaletea wananchi wake. Sipingi tajiri au fukara kuongoza nchi...napinga dhaifu, fisadi, hasiye na vision kuongoza nchi!
 
Back
Top Bottom