Rais wa Ujerumani atetea kiti chake katika uchaguzi, anaendeleza muhula wa pili

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
57699665_303.jpg

Picha: Rais wa Ujerumani Frank -Walter Steimeier
Rais wa Ujerumani, Frank-Walter Steinmeier amechaguliwa tena kutumikia muhula wa pili wa miaka mitano.

Rais huyo maarufu amechaguliwa kwenye mkutano maalum wa wabunge 736 na wawakilishi wa majimbo 16 ya Ujerumani uliofanyika jana Jumapili mjini Berlin.

Mwanasiasa huyo mahiri mwenye umri wa miaka 66 wa Chama cha Social Democratic (SPD) aliungwa mkono na vyama vyote vitatu vinavyounda serikali ya mseto pamoja na chama cha upinzani cha wahafidhina cha Christian Democratic Union (CDU).

Steinmeier katika hotuba kwenye Bunge Maalum baada ya kukubali kuchaguliwa kwake, amesema wajibu wake ni kuwatumikia watu wote wa Ujerumani na amesisitiza kuwa haegemei upande wowote na linapokuja suala la demokrasia yeye wakati wote atasimama na wanaotetea demokrasia.

Wadhifa wa Rais nchini Ujerumani ni wa heshima tu. Wagombea wengine watatu waligombea ofisi hiyo ya juu zaidi nchini Ujerumani ingawa hawakuwa na nafasi kubwa ya kushinda.

PIA SOMA:
- Ujerumani kumchagua Rais wake kupitia Baraza la Wabunge
 
Back
Top Bottom