Rais wa Tanzania kukutana na Viongozi wa Vyama vya Siasa Ikulu ya Dar es salaam

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,609
218,032
Hii ndio Taarifa mpya iliyosambazwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa Nchini Tanzania .

Kwamba viongozi wa vyama vyote vya Siasa nchini Tanzania wanaombwa kufika Ikulu tarehe 03/01/2023 ili kuonana na kuongea na Rais Dkt Samia Suluhu , kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete , kuanzia saa 3 asubuhi .

Kila Chama cha siasa kimeombwa kufika na viongozi wanne wa Juu , Mwenyekiti , Makamu Mwenyekiti , Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu .

Nimeona Barua ya mwaliko huo kutoka ofisi ya Msajili kwenda kwa vyama vya siasa , bali Hakuna maelezo yoyote kuhusu ajenda zitakazojadiliwa , Lakini tunadhani kwamba Masuala ya Katiba Mpya , Tume Huru ya Uchaguzi , Mikutano ya hadhara na Maandamano vyaweza kuwa ajenda kuu .

Ngoja tusubiri .
 
Naamini mikutano ya hadhara ya siasa ndio inaenda kuruhusiwa rasmi, huo utakuwa uwanja mzuri wa kufanya hivyo, kile kikao cha Mbowe, Kinana, na Samia juzi ndio kitakuwa kilifikia maazimio hayo.

Lakini kama ikitokea ikawa kinyume na hapo, basi kitakachofanyika ni kupotezeana muda kwenye maridhiano, na mazungumzo yenyewe hayatakuwa na tija yoyote kwenye mustakabali wa siasa zetu, zaidi ya kuinufaisha CCM na serikali yake.
 
Okay, ngoja ifike ofisini tuone.

Rangi ya nguo? Barua haina maelekezo ya dressing code ama nitupie tu hata Kihadzabe?

Nausubiri kwa hamu huo mkutano.
 
Naamini mikutano ya hadhara ya siasa ndio inaenda kuruhusiwa rasmi, huo utakuwa uwanja mzuri wa kufanya hivyo, kile kikao cha Mbowe, Kinana, na Samia juzi ndio kitakuwa kilifikia maazimio hayo.

Lakini kama ikitokea ikawa kinyume na hapo, basi kitakachofanyika ni kupotezeana muda kwenye maridhiano, na mazungumzo yenyewe hayatakuwa na tija yoyote kwenye mustakabali wa siasa zetu, zaidi ya kuinufaisha CCM na serikali yake.
Ngoja tuone
 
Hii ndio Taarifa mpya iliyosambazwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa Nchini Tanzania .

Kwamba viongozi wa vyama vyote vya Siasa nchini Tanzania wanaombwa kufika Ikulu tarehe 03/01/2023 ili kuonana na kuongea na Rais Dkt Samia Suluhu , kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete , kuanzia saa 3 asubuhi .

Kila Chama cha siasa kimeombwa kufika na viongozi wanne wa Juu , Mwenyekiti , Makamu Mwenyekiti , Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu .

Nimeona Barua ya mwaliko huo kutoka ofisi ya Msajili kwenda kwa vyama vya siasa , bali Hakuna maelezo yoyote kuhusu ajenda zitakazojadiliwa , Lakini tunadhani kwamba Masuala ya Katiba Mpya , Tume Huru ya Uchaguzi , Mikutano ya hadhara na Maandamano vyaweza k
Makamu Mwenyekiti wa Chama atahudhuriaje sasa! Tuliwaambia Chadema na Makamu Mwenyekiti wao waache ujuaji hawasikii. Sasa wataenda pungufu kesho!! Wakizidiwa hoja huko wanaishia kususa!!
 
Ila SERIKALI hii sijasikia mtu SHUPAVU kutoka upinzani kapewa teuzi ....Kila mtu APAMBANE na kombe lake KIPINDI kile upinzani wengi walipewa teuzi
 
Back
Top Bottom