Rais wa Tanzania kufanya mahojiano na MSNBC-Andrea Mitchel

Nadhani atatumia lugha ya kiingereza...Umesikia wanasema 'He is a very special man'
Mimi naogopa kusikiliza kama ni kwa lugha ya Malkia maana lugha gongana kwa mkulu

Unaogopa kusikia " Atamanufacture teachers"!!!!!
 
wapendwa,

afadhali mie sikumsikiliza!!

mambo ya nchi yetu tanzania huwa yananipa kizunguzungu!!

ngoja niendelee kukoncentrate na kitabu changu!!

mbarikiwe sana ,

Glory to God!
 
JK amejitahidi kuelezea Umasikini wa Tanzania hasa vijiji. Msikilize kupitia link hii hapa chini

[video]http://video.msnbc.msn.com/nightly-news/47479032/#47478787[/video]
 
Anaona raha Kila siku Kuongelea Umasikini kama ni kitu cha kujivunia.
 
yaani huyu mzee jamani...yaani anajiona jabali kujisifia nchi masikini wakati ina kila kitu cha kuifanya iwe tajiri....daaaah
 
Mara 1000 ningeona rais anafanya jambo la maana kwa kuitisha mkutano wa kitaifa unaojumuisha watu mbalimbali wa matabaka mbalimbali na kujadili namna ya kuondoa umaskini. Ifike mahali sasa kama taifa tuwaambie viongozi wetu waache kutuabisha na kutafuta majawabu kwa wanyonyaji.

Watanzania ndio wanaokumbana na adha ya umaskini, lakini kwa hakika ni watanzania hawa hawa maskini ndio wenye majawabu juu ya namna ya kutokomeza umaskini. Tatizo tulilo nalo ni kasumba mbaya kwa viongozi wetu kujadili with the wrong people.

Hii campaign ya nutrition imeletwa na Marekani. It is not coming from us, na kwa mtu mwenye akili timamu Marekani wamebuni hii campaign kama njia mojawapo ya kupambana na influence ya China Africa. Wanajua watu wengi bado hawana chakula cha kutosha, na mchina yeye haongei mambo ya chakula, sasa wanacheza na akili za viongozi wetu. Na campaign inaongozwa na shirika lao USAID. kila anapokwenda Kikwete anakumbana na mkurugenzi wa USAID! Inakuwaje? Mbona hao USAID hawawagandi wakenya? Au Tanzania wana shida ya chakula kuliko Kenya?
 
Tanzania si kuna ardhi ya kutosha otherwise Somalia,Sudan na Kenya ndo wana njaa
 
Mara 1000 ningeona rais anafanya jambo la maana kwa kuitisha mkutano wa kitaifa unaojumuisha watu mbalimbali wa matabaka mbalimbali na kujadili namna ya kuondoa umaskini. Ifike mahali sasa kama taifa tuwaambie viongozi wetu waache kutuabisha na kutafuta majawabu kwa wanyonyaji.

Watanzania ndio wanaokumbana na adha ya umaskini, lakini kwa hakika ni watanzania hawa hawa maskini ndio wenye majawabu juu ya namna ya kutokomeza umaskini. Tatizo tulilo nalo ni kasumba mbaya kwa viongozi wetu kujadili with the wrong people.

Hii campaign ya nutrition imeletwa na Marekani. It is not coming from us, na kwa mtu mwenye akili timamu Marekani wamebuni hii campaign kama njia mojawapo ya kupambana na influence ya China Africa. Wanajua watu wengi bado hawana chakula cha kutosha, na mchina yeye haongei mambo ya chakula, sasa wanacheza na akili za viongozi wetu. Na campaign inaongozwa na shirika lao USAID. kila anapokwenda Kikwete anakumbana na mkurugenzi wa USAID! Inakuwaje? Mbona hao USAID hawawagandi wakenya? Au Tanzania wana shida ya chakula kuliko Kenya?

wewe ni malalamikaji tu,hebu jiulize wewe umefanya nini kuondoa umaskini wa watanzania zaid ya kubeza wanayofanya wengine.
 
Dunia inaangalia miaka 50 ijayo hali ya chakula itakuwaje? Maana population inaongezeka kwa kasi sana na uhitaji wa chakula unaongezeka hususan katika nchi za africa na Asia. Hivyo basi nchi zilizoendelea zinahitaji kujihakikishia usalama wa chakula kwa miaka ijayo wakati nasi tunahitaji angalau kujikwamua kutoka katika janga la njaa na umaskini.

Njia pekee ni kwa kushirikiana na mataifa mbalimbali kuinua kilimo katika nchi zetu za Afrika ili tujikwamue kwa sasa na tuwe na uhakika wa hiyo miaka 50 ijayo. UNIDO wameanza kuzunguka katika nchi zilizoendelea kwa teknolojia za kilimo ili zije afrika kwa mfano wameshaenda Israel, Marekani, Uk nk.

Hivyo basi JK ameongea vitu muhimu kuwa ili kutoka hapa tulipo katika sekta ya agriculture inabidi kufanya kazi bega kwa bega na wakulima. Wakulima wanahitaji inputs, teknolojia na soko la uhakika. Ameomba wawekezaji wa ndani na nje pamoja na serikali za nchi tajiri na maskini kushirikiana. Tunatakiwa tuwaalike hawa kwa malengo tajwa juu na kuwaondoa wakulima wetu kuitwa wakulima wadogowadogo ila tu tuanze kujadili juu ya mikataba mizuri iwapo wawekezaji watakuja kuwekeza katika sekta ya kilimo. Ninaamini itakuwa njia mojawapo ya kutupa ahueni ya maisha.

Big up JK ila hakikisha iwe kwa manufaa ya wa TZ wote na sio wachache.
 
Tatizo la viongozi wetu ni waoga sana linapokuja swala la hao weupe. Hata kama huna tatizo mweupe wa ulaya akituambia tuna tatizo huwa tunawakubalia. Hapo ndipo mwanzo wa matatizo kwa vile, ni kama mganga wa kienyeji, chochote akitakacho tunawapa ili mradi atuhakikishie kuwa atatuondolea tatizo letu ambazo sisi wenyewe hatulijui ila yeye.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
wewe ni malalamikaji tu,hebu jiulize wewe umefanya nini kuondoa umaskini wa watanzania zaid ya kubeza wanayofanya wengine.

Na kama hawezi kuondoa umaskini aliomba kazi ya urais kwa nini? Miaka sita sasa, maisha bora kwa kila mtanzania yako wapi?
 
Back
Top Bottom