Rais wa Russia Vladimir Putin apinga North Korea kuwekewa vikwazo vipya

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,929
military.jpg


Kiongozi wa Russia Vladimir Putin, akiwa anaongea kwenye mkutano wa 'Brics group' (Brazil, Russia, India, China and South Africa) uliofanyika Xiamen, China, amesema kuendelea kutaka kuiwekea vikwazo vipya North Korea ni sawa na kazi bure, pia amesema "North Korea watakula hata nyasi, kuliko kuachana na mpango wao wa nuclear."

Licha ya Putin kuishutumu North Korea, alisema kuwa vikwazo havitasaidia.

Marekani walisema siku ya Jumatatu kwamba wataweka mezani azimio jipya la UN juu ya vikwazo vigumu zaidi dhidi ya North Korea, kufuatia jaribio lao jipya la nuclear la jumapili.

Bwana Putin pia alisema kuwa hatua za kijeshi inaweza kuleta janga la dunia nzima.

Putin amesema kuwa mazungumzo ya diplomasia ndio njia pekee.

Kiongozi wa Ujerumani Angela Merkel, alikubaliana na mpango huo wa kuongeza vikwazo zaidi kwa North Korea siku ya Jumanne na kusema kwamba vikwazo hivyo vinahitajika mara moja ili kukabiliana na North Korea kuvunja mkataba na maazimio ya wazi ya kimataifa.
 
Rais wa Urusi bwana putini alitumia kura yake kupinga NK kuwekewa vikwazo akidai havitasaidia chochote kwa kuwa taifa hilo liko tayari hata kula nyasi lakini sio kuacha mpango wake wa nyuklia
Putini alisema hakuna njia nyingine zaidi ya mazungumzo na NK kwa kuwa vita dhidi ya korea kaskazini haitambakisha mtu salama

Wakati huo huo china nayo imetumia kura yake kupinga vikwazo dhidi ya NK kwa madai havijawahi kusaidia chochote
Huku wakisisitiza kujizuia kwa njia yoyote ya vita dhidi ya korea kaskazin

Wakati huo huo Marekani imesisitiza kuipa korea kusini mabomu makubwa zaidi ili kujikinga na korea kaskazini

Bbc Uingereza
 
Huyo ni zaidi ya mramba kichwa ngumu
Nyuklia na yeye yeye na nyuklia baasi
Wamemdekeza tu. Alitakiwa apigwe kabla ya Saddam.

Mara nyingine nafikiri General Douglas MacArthur alikuwa sahihi kutaka kuwamaliza hawa tangu vita vya pili vya dunia.

Angefanikiwa sasa hivi Korea ingekuwa moja na yote ingekuwa kama Korea Kusini.

Ila Truman akawa mwanadiplomasia.
 
Wamemdekeza tu. Alitakiwa apigwe kabla ya Saddam.

Mara nyingine nafikiri General Douglas MacArthur alikuwa sahihi kutaka kuwamaliza hawa tangu vita vya pili vya dunia.

Angefanikiwa sasa hivi Korea ingekuwa moja na yote ingekuwa kama Korea Kusini.

Ila Truman akawa mwanadiplomasia.
Kuhusu hizi korea 2 Mmarekani Urusi china wanahusika toka vita ya pili ya dunia
Mmarekani na korea ya kusini
Urusi na korea kaskazini
 
Wamemdekeza tu. Alitakiwa apigwe kabla ya Saddam.

Mara nyingine nafikiri General Douglas MacArthur alikuwa sahihi kutaka kuwamaliza hawa tangu vita vya pili vya dunia.

Angefanikiwa sasa hivi Korea ingekuwa moja na yote ingekuwa kama Korea Kusini.

Ila Truman akawa mwanadiplomasia.
Soviet na China wangekubali ?

Ndio maana walitenganishwa na baraza la usalama la umoja wa mataifa ,wakomunisti wakapewa NK na bepari wakamchukua south

Wazo lako lisingeweza kutekelezeka sababu wakomunisti walikuwa jino kwa jino na North na soviet ndiye walimuweka Kim II sul na soviet ambaye alikuwa trained soviet ,ndio maana mpaka Leo kimtindo Urusi anampa back up dogo lake
 
Huyu putin nae ni putout.... alisahau alipoambiwa akae pembeni watu wakaripue Syria? Asitushuhulishe mnafik namba 1 huyo.... yeye maneno tu.... vitendo sifuri... mikwala mingiii
 
Wewe Umemsikiliza kwa makini
Ameaza Kazi muda mrefu Kabla ujazaliwa
US huwezi kumpiga North Korea kirahisi Kama unavojua wewe


Sent using Jamii Forums mobile app
Putin ata km ameanza kaz kabla bibi yangu mzalia bibi aliemzaa bibi putin anabaki kuwa Coward tu.

Ni mnafiki.... nilitegemea putin atamdefend Syria dhidi ya uvamizi wa mabeberu wenzake lakini kamuacha mkono. Syria leo ipo chali kifo cha mende. Anaruhusu rafiki yake apigwe na mpinzani wake. Alitakiwa adefend na aoneshe msimamo wake. Yeye kutwa kutoa maneno tu. Kapewa kipaji cha matamko. Action hamna kitu. NK akivamiwa putin atatoa maneno tu na yeye na mchina wake. Communist nations zenyewe haziaminiani na hii ndio weakness yao.

USA anacheza kama pele, kwa silaha na tech alokuwa nayo jamaa ni rahisi kumvuruga NK. Kumbuka izo test za north korea zote zimekuwa detected, kwaio si kazi ngumu kwa USA kuzitungua kabla hazijafika ardhi yake. Lakini yeye hataki kuwa vitani peke ake akaingia hasara.

Kwanza anataka kufitunisha, ndio mana anamforce mchina kuweka vikwazo over Kim.
Pili anataka japa na Sk ndio waingie vitani dhidi ya North lkn na wao wajanja.

I will always congratulate kim for his bravery n belief but jamaa ni rahisi kwa usa kumvuruga
 
Back
Top Bottom