Rais wa nchi kuiita pesa ya nchi yake pesa ya madafu, kiongozi kweli huyo?

Kinyungu

JF-Expert Member
Apr 6, 2008
17,369
33,011
Nimemsikiliza rais Jakaya Kikwete (JK) jana na hotuba yake ya kujibaraguza mbele ya Watanzania. Sikutegemea jipya kwenye story zake za jana na wale Wazee wa vijiwe vya CCM ila hili la yeye kama rais wa nchi kudharau sarafu ya nchi yake mwenyewe hadharani limenisikitisha sana.

Ni ajabu sana kwa rais wa nchi kwenda mbele ya vyombo vya habari kukiwa na halaiki ya watu na kuiita bila haya wala aibu sarafu ya nchi kwa jina la kebehi kuwa eti ni "hela ya madafu" halafu anaachwa tu hakuna kitakachompata. Hii ni fedheha na dharau ya hali ya juu kwa sisi ambao hela hiyo ya 'madafu' ndio mshahara wetu na fedha yetu ya kufanya biashara kila siku.

Tunajua mmeiba sana na tena mkishaiba chap chap mnazibadilisha kuwa dollar hivyo haya "madafu" hata yawe sawa na toilet paper (karatasi za kuchambia) kwenu sio issue. Itakuwa ajabu sana kama nikimsikia tena waziri wa fedha na uchumi akisisitiza wafanyabiashara hasa Wahindi ambao wanajua sana umuhimu wa dhamani ya fedha wasiuze bidhaa zao kwa dollar maana hela wanayoambiwa watumie hata mkuu wa nchi anaiona haina maana yoyote zaidi ya kuwaweza kununulia tunda la bei duni la aina ya madafu.

Rais anatakiwa aelewe kuwa kauli zake za namna hii tena anazozitoa hadharani zina madhara ya moja kwa moja kwa uchumi wetu na achunge sana kauli zake anapozungumza masuala muhimu ya nchi hadharani. Kama ni kutudharau kesha fanya hivo sana lakini atuache basi na hii sarafu yetu ambayo kila kukicha anafanya mbinu za kuishusha dhamani. Kudharau sarafu ya nchi hadharani tena mchana kweupe na mtoa dharau akiwa ndie rais wa nchi inatakiwa liwe kosa la uhujumu uchumi na JK anapaswa kushitakiwa kwa hili.

Tumekuvumilia kwa mengi JK lakini kwa kuifananisha sarafu yetu na madafu umevuka mipaka. Bora ungeiita hivyo ukiwa chumbani kwako au ukisha acha nafasi yako ya urais. Ni kwa sababu unaongoza nchi yenye mifumo mibovu ya sheria inayokulinda laiti ingelikuwa nchi nyingine kauli yako hiyo ingetosha wewe kujiuzulu ukachunge mbuzi wako kule Msoga.

Mwana JF hebu piga picha nini kitampata rais Baraka Obama wa Marekani kama siku atakwenda hadharani kukiwa na vyomba vya habari na kutamka maneno ya dhihaka kwa dollar kama alivyofanya rais Jakaya Kikwete jana pale ukumbi wa Diamond Jubilee. Jibu nadhani unalo mwenyewe mwana Jf.

Wasalaam,
Kinyungu.
 
Mkuu huyu jamaa mi huwa simuelewi, unakumbuka aliisha wahi toa picha akifanya mazoezi kavaa t-shirt ya Siemens? Hii pia ni aibu kwa mhe. Raisi wakati tuna tshirts nyingi tu za kitz na hata ikulu.... jamaa hajali, anatake mambo kirahisi tu na ndo maana shilling inashuka kwa kasi sana ukilinganisha na $....
 
Kwani hela ya ''madafu'' ina maana gani kwa sababu inawezekana tunalaumu kitu ambacho kinabeba uharisia wa maneno.

Kwani kusema hela ya ''madafu'' ina madhara gani ya moja kwa moja katika uchumi wa nchi?

Naomba unieleweshe kwa sababu sifahamu msingi wa hoja yako.
mkuu hiyo ni sawa na wewe uambiwe " acha mambo ya kiswahili" japo kiswahili ni lugha yetu ila walio wengi wanarusha ngumi.... jiulize...
 
Kikwete siku zote amedhihirisha udhaifu kiuongozi na kifikra. Haelewi kabisa nguvu ya nafasi ya uraisi. Hotuba zake ukizichambua utaona ni utumbo mtupu.
 
Kwani hela ya ''madafu'' ina maana gani kwa sababu inawezekana tunalaumu kitu ambacho kinabeba uharisia wa maneno.

Kwani kusema hela ya ''madafu'' ina madhara gani ya moja kwa moja katika uchumi wa nchi?

Naomba unieleweshe kwa sababu sifahamu msingi wa hoja yako.
Mkuu hapo ni kama wewe uambiwe "una degree ya chupi" - yani ni tusi na dharau inayoonyesha kwamba kisomo chako hakina thamani! Hivyo ndio kusema kwamba: "Pesa za madafu" maana yake ni pesa zisizo na thamani!
 
Mkuu huyu jamaa mi huwa simuelewi, unakumbuka aliisha wahi toa picha akifanya mazoezi kavaa t-shirt ya Siemens? Hii pia ni aibu kwa mhe. Raisi wakati tuna tshirts nyingi tu za kitz na hata ikulu.... jamaa hajali, anatake mambo kirahisi tu na ndo maana shilling inashuka kwa kasi sana ukilinganisha na $....

Sio ilikuwa "Bwin" ?....Maana ndio naikimbuka
 
Kwani hela ya ''madafu'' ina maana gani kwa sababu inawezekana tunalaumu kitu ambacho kinabeba uharisia wa maneno.

Kwani kusema hela ya ''madafu'' ina madhara gani ya moja kwa moja katika uchumi wa nchi?

Naomba unieleweshe kwa sababu sifahamu msingi wa hoja yako.

Kwa hiyo wewe huoni 'udhaifu' uliopo katika kutamka maneno kama hayo. Yeye ni kiongozi wa nchi mkuu, anatetea maslahi ya Tanzania duniani kote. Kuitaja sarafu ya nchi anayoongoza kwa miaka tisa na ushee kuwa ni madafu ni kujidhalilisha mwenyewe. Kama hulitambui hilo angalau fikiri kidogo.
 
Nimemsikiliza rais Jakaya Kikwete (JK) jana na hotuba yake ya kujibaraguza mbele ya Watanzania. Sikutegemea jipya kwenye story zake za jana na wale Wazee wa vijiwe vya CCM ila hili la yeye kama rais wa nchi kudharau sarafu ya nchi yake mwenyewe hadharani limenisikitisha sana.

Ni ajabu sana kwa rais wa nchi kwenda mbele ya vyombo vya habari kukiwa na halaiki ya watu na kuiita bila haya wala aibu sarafu ya nchi kwa jina la kebehi kuwa eti ni "hela ya madafu" halafu anaachwa tu hakuna kitakachompata. Hii ni fedheha na dharau ya hali ya juu kwa sisi ambao hela hiyo ya 'madafu' ndio mshahara wetu na fedha yetu ya kufanya biashara kila siku.

Tunajua mmeiba sana na tena mkishaiba chap chap mnazibadilisha kuwa dollar hivyo haya "madafu" hata yawe sawa na toilet paper (karatasi za kuchambia) kwenu sio issue. Itakuwa ajabu sana kama nikimsikia tena waziri wa fedha na uchumi akisisitiza wafanyabiashara hasa Wahindi ambao wanajua sana umuhimu wa dhamani ya fedha wasiuze bidhaa zao kwa dollar maana hela wanayoambiwa watumie hata mkuu wa nchi anaiona haina maana yoyote zaidi ya kuwaweza kununulia tunda la bei duni la aina ya madafu.

Rais anatakiwa aelewe kuwa kauli zake za namna hii tena anazozitoa hadharani zina madhara ya moja kwa moja kwa uchumi wetu na achunge sana kauli zake anapozungumza masuala muhimu ya nchi hadharani. Kama ni kutudharau kesha fanya hivo sana lakini atuache basi na hii sarafu yetu ambayo kila kukicha anafanya mbinu za kuishusha dhamani. Kudharau sarafu ya nchi hadharani tena mchana kweupe na mtoa dharau akiwa ndie rais wa nchi inatakiwa liwe kosa la uhujumu uchumi na JK anapaswa kushitakiwa kwa hili.

Tumekuvumilia kwa mengi JK lakini kwa kuifananisha sarafu yetu na madafu umevuka mipaka. Bora ungeiita hivyo ukiwa chumbani kwako au ukisha acha nafasi yako ya urais. Ni kwa sababu unaongoza nchi yenye mifumo mibovu ya sheria inayokulinda laiti ingelikuwa nchi nyingine kauli yako hiyo ingetosha wewe kujiuzulu ukachunge mbuzi wako kule Msoga.

Mwana JF hebu piga picha nini kitampata rais Baraka Obama wa Marekani kama siku atakwenda hadharani kukiwa na vyomba vya habari na kutamka maneno ya dhihaka kwa dollar kama alivyofanya rais Jakaya Kikwete jana pale ukumbi wa Diamond Jubilee. Jibu nadhani unalo mwenyewe mwana Jf.

Wasalaam,
Kinyungu.
Ni Kweli alichosema Rais wetu kuwa Pesa ya Tanzania ni Pesa ya Madafu mimi huwa ninaita Shilingi ya Tanzania ni Pesa ya machungwa sasa angalia machungwa na madafu ipi zaidi Mkuu Kinyungu Pesa ya Tanzania ingelikuwa na thamani mbona tungelikuwa tumekwisha kuendelea kimaendeleo.Lakini pesa yetu ya Machungwa haina thamani tutaendelea kivipi? Viongozi wetu wengi wao ni Mafisadi na Wala Rushwa tutaweza kweli kuwa na maendeleo? Rais ana haki kusema Pesa ya nchi yake ni pesa ya Madafu haina thamani ndani na nje ya nchi mimi pia nina muunga mkono Mheshimiwa Rais JK..
 
Rais kwa maneno yako inaonyesha ni jinsi gani usivyopenda nchi na watu wake huna hata chembe ya uzalendo kwa kejeli.
 
Hilo jina la madafu si jina la dharau sasa kwanini kama wewe ndio kila kila na ndio uliotuhalalishia hiyo kuwa fedha halali ya malipo leo hii uite ni madafu bado hapo sio tofauti yake na mtu anaejidharau mwenyewe..
 
Mimi sijaona tatizo lolote, kukosa hoja za msingi za kujadili mambo muhimu
tunakaa kushupalia neno 'pesa ya madafu'. Labda hili linaweza kuwa tatizo
kwa watu wa shamba na si mjini. Neno hilo halina athari yoyote iwe kisiasa
kiuchumi nk. Tutafute kukosoa hotuba yake katika mambo mengine
kujadili hili ni upuuzi zaidi.
 
Mkuu, lazima awe dharau maana zile wanazokwapua zipp kwa dollar.
Ndio zile kauli za akina Chenge- vijisenti
 
Mimi sijaona tatizo lolote, kukosa hoja za msingi za kujadili mambo muhimu
tunakaa kushupalia neno 'pesa ya madafu'. Labda hili linaweza kuwa tatizo
kwa watu wa shamba na si mjini. Neno hilo halina athari yoyote iwe kisiasa
kiuchumi nk. Tutafute kukosoa hotuba yake katika mambo mengine
kujadili hili ni upuuzi zaidi.
Wewe mwenzetu huoni.Tambua tu neno lililotamkwa na mkuu wa nchi lina maana kubwa. Inawezekana halikuwepo kwenye Andiko la Hotuba ila kalichomekea tu, lakini halikuwa neno zuri kutamkwa na mkuu wa nchi dhidi ya Fedha anayoisimamia!
 
Kwani hela ya ''madafu'' ina maana gani kwa sababu inawezekana tunalaumu kitu ambacho kinabeba uharisia wa maneno.

Kwani kusema hela ya ''madafu'' ina madhara gani ya moja kwa moja katika uchumi wa nchi?

Naomba unieleweshe kwa sababu sifahamu msingi wa hoja yako.

Mkuu wamekuibia password au ni wewe?
 
Mkuu mtoa mada hili jambo liliniuma sana nikalipost facebook straight ili liwalo na liwe. Wachangiaji wasioona tatizo ni washabiki ambao upeo wao wa masuala ya uchumi na fedha ni mdogo sana. Na hawajui thamani ya fedha inaakisi nini, pili hata Kikwete mwenyewe hajui kwanini hela yetu inashuka thamani kila uchwao. Kweli shule ni tatizo
 
Back
Top Bottom