Lee Swagger
JF-Expert Member
- Mar 30, 2018
- 1,064
- 1,807
TRUMP AIBANA KOO RWANDA - TANZANIA, UGANDA, KENYA ZAPONEA CHUPUCHUPU: Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwamba hatoziwekea vikwazo vya kibiashara nchi za Tanzania, Uganda, Kenya kama alivyofanya kwa Rwanda endapo nchi hizo zitaendelea na uamuzi wao wa kutopiga marufuku bidhaa za mitumba kutoka marekani.
Uamuzi huo wa Trump wa kuiwekea Rwanda ushuru wa nguo zake katika soko la Marekani umetokana na Rwanda kuweka vikwazo kwa nguo na viatu vya mitumba vinavyotoka Marekani.
Chini ya mkataba wa ushirikiano wa kibiashara baina ya Afrika na Marekani (AGOA) baadhi ya nchi za Afrika Rwanda ikiwemo ziliondolewa ushuru wa baadhi ya bidhaa zake zinazouzwa Marekani.
"Hata hivyo Marekani inaendelea kutoa faida za AGOA kwa mataifa ya Tanzania na Uganda kwa sababu nchi hizo zimechukua hatua ya kuondoa kodi ya nguo na viatu vya mitumba na kuamua kutopiga marufuku bidhaa hizo," alisema mwakilishi wa ofisi ya biashara ya Marekani.
"Ninaipongeza Tanzania na Uganda kwa kuchukua hatua za kupatia suluhu hofu za Marekani," alisema afisa wa masuala ya biashara katika ofisi ya rais nchini Marekani C. J. Mahoney katika taarifa yake.
Rais Trump amesema kuwa kupiga marufuku mitumba Rwanda imevunja makubaliano ya kibiashara na Marekani chini ya AGOA.
Uamuzi huo wa Trump wa kuiwekea Rwanda ushuru wa nguo zake katika soko la Marekani umetokana na Rwanda kuweka vikwazo kwa nguo na viatu vya mitumba vinavyotoka Marekani.
Chini ya mkataba wa ushirikiano wa kibiashara baina ya Afrika na Marekani (AGOA) baadhi ya nchi za Afrika Rwanda ikiwemo ziliondolewa ushuru wa baadhi ya bidhaa zake zinazouzwa Marekani.
"Hata hivyo Marekani inaendelea kutoa faida za AGOA kwa mataifa ya Tanzania na Uganda kwa sababu nchi hizo zimechukua hatua ya kuondoa kodi ya nguo na viatu vya mitumba na kuamua kutopiga marufuku bidhaa hizo," alisema mwakilishi wa ofisi ya biashara ya Marekani.
"Ninaipongeza Tanzania na Uganda kwa kuchukua hatua za kupatia suluhu hofu za Marekani," alisema afisa wa masuala ya biashara katika ofisi ya rais nchini Marekani C. J. Mahoney katika taarifa yake.
Rais Trump amesema kuwa kupiga marufuku mitumba Rwanda imevunja makubaliano ya kibiashara na Marekani chini ya AGOA.