Rais wa Ethiopia awasili Chato mkoani Geita. Rais Magufuli aahaidi kuwaachia wahamiaji haramu 1789 kutoka Ethiopia bila masharti

Sina uhakika kama Mwalimu (RIP) ali host Mwaliko wa kidola ndani ya Butiama, Sina uhakika vilevile kama Mzee Mwinyi alifanya dhifa ya kitaifa hapo kwake msasani ama Zanzibar - ama Mzee wetu Mkapa (RIP) naye kule Lupaso ama Lushoto, halikadhalika sina uhakika kama Jakaya alifanya mwaliko kama huu huko Msoga !!

Katiba ya nchi inasemaje kuhusu ugeni kama huu !! Je Chato ina Ikulu tayari ? Sipingi kuwapokea wageni hawa ila utatarabiu wa Katiba na Sheria zetu unasemaje tafadhali

..Chato International Airport ilikuwa upigaji tu.

..ila kipindi hiki jamaa yuko lockdown ya Covid-19 ndio uwanja umepata matumizi.
 
Ukizingatia kuwa kuna tetesi za Co...19 kuwako Tz huenda asitoke Chato tena.
Dont quote me ni mawazo tu.
 
Sina uhakika kama Mwalimu (RIP) ali host Mwaliko wa kidola ndani ya Butiama, Sina uhakika vilevile kama Mzee Mwinyi alifanya dhifa ya kitaifa hapo kwake msasani ama Zanzibar - ama Mzee wetu Mkapa (RIP) naye kule Lupaso ama Lushoto, halikadhalika sina uhakika kama Jakaya alifanya mwaliko kama huu huko Msoga !!

Katiba ya nchi inasemaje kuhusu ugeni kama huu !! Je Chato ina Ikulu tayari ? Sipingi kuwapokea wageni hawa ila utatarabiu wa Katiba na Sheria zetu unasemaje tafadhali
Gubu tu hamna hoja hapo
 
Lissu aliposema ule uwanja hauna activities zozote sasa mkuu anawalazimisha wageni wake watue angalau kule?
Tatizo ni akiondoka kama Mabutu je uwanja utatumika. Lakini kuna biashara ya samaki ndege zinaweza kubeba samaki
 
Karibuni Sana Bandugu zetu Wana Afrika.

Karibuni Tanzania,

Karibuni Chato.

Karibuni Sana Arumeru.
 
sawa, sasa tuambie rais katokomea wapi ndugu? maana dar hayupo, dom haonekani
Unataka aje nyumbani kwako ili ujue yupo? Chuki na wivu wa aina hii mbona hauwezi kukuacha salama ndg! Magu piga humohumo, tupo pamoja na tunakuelewa!
 
Back
Top Bottom