Rais wa Burundi atapata Tsh biilioni 1.1 akistaafu Urais

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,005
9,872
Imesalia miezi minne kabla ya uchaguzi wa urais nchini Burundi, uchaguzi ambao rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amebainisha mara kadhaa kwamba hatawania.

Hayo yanajiri wakati Bunge la nchi hiyo limeidhinisha sheria inatakayompa rais Nkurunziza kitita cha faranga Burundi bilioni moja sawa na Dola laki 5 za Marekani atakapostaafu.

Hata hivyo upinzani umelalama na kusema fedha hizo ni nyingie mno.

Pia Bunge la Burundi limepitisha muswada wa sheria unaompa rais Pierre Nkurunziza cheo cha "Kiongozi Mkuu".
Sheria hiyo iliyotetewa bungeni na Waziri wa Sheria Aime Laurentine Kanyana, inaagiza pia Rais atakapostaafu kuchukuliwa kwa hadhi ya makamu wa rais kwa kipindi cha miaka 7.

Muswada huo wa sheria pia utamuwezesha kulipwa mshahara katika kipindi chote cha maisha yake, kupata marupurupu yote anayopewa makamu wa rais aliyeko mamlakani na atapewa nyumba ya kifahari, anayopewa kila rais wa Burundi aliyechaguliwa kidemokrasia.
 
'Dola laki 5 za Marekani'

Hizi pesa sio sawa na Tsh. Trillion 1 kama ulivyosema.

Pia anatengenezewa cheo cha Supreme Leader kama kile cha Ayattolah wa Iran yaani kunakua na Rais na kiongozi mkuu wa nchi,so technically Nkurunziza ataendelea kuendesha nchi.

dodge
 
Dola laki tano ni sawa na 1 bilion na points kwa hela za TZS.

Kwa vyeo alivyojiwekea hakuwa na haja ya kuachia urais kwa sababu ni kuingizia nchi gharama ambazo siyo za lazima.

Japo hujafafanua vizuri, ni utaratibu gani utatumika kupata kiongozi mkuu wa nchi? Ni kila Rais anapostaafu anakuwa kiongozi mkuu wa nchi na yule wa kwanza kustaafu pia?

Unakuwa kiongozi mkuu wa nchi huku pia utakuwa na cheo sawa na makamu wa rais maana yake nchi inakuwa na makamu wa rais wawili

Ayatollah = Vice President = Country Supreme Leader.

Then, President = ? is President>Supreme Leader?
 
Dola laki tano ni sawa na 1 bilion na points kwa hela za TZS

Kwa vyeo alivyojiwekea hakuwa na haja ya kuachia urais kwa sababu ni kuingizia nchi gharama ambazo siyo za lazima.

Japo hujafafanua vizuri, ni utaratibu gani utatumika kupata kiongozi mkuu wa nchi? Ni kila Rais anapostaafu anakuwa kiongozi mkuu wa nchi na yule wa kwanza kustaafu pia?

Unakuwa kiongozi mkuu wa nchi huku pia utakuwa na cheo sawa na makamu wa rais maana yake nchi inakuwa na makamu wa rais wawili

Ayatollah = Vice President = Country Supreme Leader

Then, President = ? is President>Supreme Leader?
'Ayatollah = Vice President = Country Supreme Leader

Then, President = ? is President>Supreme Leader?'

Daah it's complicated.

dodge
 
Dola laki tano ni sawa na 1 bilion na points kwa hela za TZS

Kwa vyeo alivyojiwekea hakuwa na haja ya kuachia urais kwa sababu ni kuingizia nchi gharama ambazo siyo za lazima.

Japo hujafafanua vizuri, ni utaratibu gani utatumika kupata kiongozi mkuu wa nchi? Ni kila Rais anapostaafu anakuwa kiongozi mkuu wa nchi na yule wa kwanza kustaafu pia?

Unakuwa kiongozi mkuu wa nchi huku pia utakuwa na cheo sawa na makamu wa rais maana yake nchi inakuwa na makamu wa rais wawili

Ayatollah = Vice President = Country Supreme Leader

Then, President = ? is President>Supreme Leader?
Vituko tupu mkuu, mwenyewe nilisikia hii habari DW jana sikuielewa.

Huyu mjinga anastaafu urais geresha tu, ila anaendelea kuongoza nchi maisha yake yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Afadhali huyo ametajwa hadharani, hawa wa hapa kwetu WANAJICHOTEA WATAKAVYO na kufanyia STAREHE tu.
 
Madikteta wa Afrika wameanza kumuiga Putin kuweka watu wa kuwashikia hiyo nafasi naona Kabila yeye kafanikiwa tayari tusubirie huyo Nkrunzinza na Museveni.
 
Afadhali huyo ametajwa hadharani, hawa wa hapa kwetu WANAJICHOTEA WATAKAVYO na kufanyia STAREHE tu.
Tanzania nchi ambayo rais anastafu huku akiwa anatabasamu tena akiwa hana hata mawazo ya kuongezewa wiki 2, Tanzania nchi ambayo ma rais wake wore hawajaikimbia nchi na wanashiriki kwenye shufhuli za kijamii kikamilifu, nchi ambayo hakuna raid aliyewahi kugoma kutoka madarakani.
 
Afadhali huyo ametajwa hadharani, hawa wa hapa kwetu WANAJICHOTEA WATAKAVYO na kufanyia STAREHE tu.
Tanzania nchi ambayo rais anastafu huku akiwa anatabasamu tena akiwa hana hata mawazo ya kuongezewa wiki 2, Tanzania nchi ambayo ma rais wake wore hawajaikimbia nchi na wanashiriki kwenye shufhuli za kijamii kikamilifu, nchi ambayo hakuna raid aliyewahi kugoma kutoka madarakani.
 
Afadhali huyo ametajwa hadharani, hawa wa hapa kwetu WANAJICHOTEA WATAKAVYO na kufanyia STAREHE tu.
Tanzania nchi ambayo rais anastafu huku akiwa anatabasamu tena akiwa hana hata mawazo ya kuongezewa wiki 2, Tanzania nchi ambayo ma rais wake wore hawajaikimbia nchi na wanashiriki kwenye shufhuli za kijamii kikamilifu, nchi ambayo hakuna raid aliyewahi kugoma kutoka madarakani
 
Rekebisha title ya habari yako. Dola laki tano haifiki kwenye trilioni 1.1, ni bilioni 1.1 kwa pesa ya kitanzania.
Ni kama Tsh. 1,150,000,000/= hivi. Nafikiri wameona kama ndio itamfanya aende basi ngoja apewe.

Ila anataka awe "The power behind the throne"..!! Ila hii mara nyingi inakuja ku-backfire sana. Tuliona hata hapa kwa Nyerere na Mwinyi, walibaki kushibana kinafiki sana.

Tuliona kule Cameroon kitendo alichofanyiwa rais wao wa kwanza Ahmadou Ahidjo mwaka 1982 na rais wa sasa anayeumwa Bw. Paul Biya.

Hata kule Malawi tuliona interaction ya Bakili Muluzi na Mbingu wa Mutharika (Rip)ilivyokuwa hadi wakashikana uchawi na baadaye Mutharika kumuita Muluzi hadharani kuwa "Mwizi".

Pia Zambia hadi Levi Mwanawasa (Rip) akamburuza Frederick Chiluba (Rip) mahakamani kwa madai ya ufisadi hadi kupelekea Chiluba kufariki ostensibly prematurely.

Kule Angola pia tunaona misukosuko anayopata Jose Eduardo dos Santos na familia yake hadi yeye kuvuliwa uwenyekiti wa chama cha MPLA.

Na hata hapa Tz, mahusiano ya rais wa sasa na watangulizi wake wawili, umejawa na unafiki mkubwa mno, rejea sera nyingi za Magufuli na tabia yake ya kuwaponda watangulizi wake kuwa hamna cha maana walichokifanya.

Hata mahusiano ya Joseph Kabila na rais wa sasa wa DRC Etienne Tshisekedi yanaenda yakigubikwa na ukakasi kila uchao. Hivyo Nkurrunziza should not take anything for granted.

Yeye Nkurunziza, akiondoka madarakani ajue ameondoka yale mambo ya kuvizia the second chance ni tamaa ambayo itamgharimu. Ajifunze kutokana na historia, although the dictators always learn the hard way.
.
 
Back
Top Bottom