#COVID19 Rais ulifanya makosa makubwa kuifanya chanjo kuwa hiari, ulipaswa kukubaliana na Mbowe kuwa chanjo lazima ili tuweze kupambana na Gwajima

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
52,187
42,011
Wasalaam wana jamvi.

Mimi ni mmoja wa watu ambao kusema kweli nilitamani kabisa swala la chanjo liwe kwa lazima kwa kila mtanzania na hili lilipaswa kuwekwa wazi kabisa na Mh Rais pale alipotangaza ujio wa chanjo hiyo kwani ingesaidia sana kupambana na watu wanaopinga chanjo hiyo.

Nakumbuka hivi karibuni Mh Mbowe aliweka wazi kabisa kuwa anataka serikali itoe chanjo kwa watanzania wote kwa lazima lakini alipata upinzani mkubwa kutoka kila upende na watu tukasahau kuwa kuna wamba watatumia huo mwanya wa chanjo ya hiari kuipinga chanjo na kuwatisha na kuwahamasisha wengine wasiende kupata chanjo kwani sio lazima. Kwa hiyo mtu akishawishiwa kutokwenda na asipo kwenda hakuna kosa kwani ni hiari Mtu akishawishiwa kwenda na akafanikiwa kwenda bado hakuna kosa lolote.

Madhara ya chanjo ya hiari ndiyo haya lazima watazuka watu kutoa maoni yao na watazuka watu kuwahamasisha watu kutochanjwa hivyo ni lazima tukubali kuwa watu wameamua kuutumia mwanya uliotengenezwa na mamlaka zenyewe hatupaswi kuwatisha bali nasisis tuwashawishi wengine wakachanjwe lazima kuna mmoja wetu atafanikiwa.

Kuwashambulia watu ambao tumewapa uhuru sisi wenyewe kwani ni sisi tuliosema kuwa chanjo ni hiari kwa hiyo kamwe hatupaswi kusema kuna watu wanapotosha bali tunatakiwa kutoa elimu juu ya chonjo na kuwashawishi watu wakachanjwe.

Ukweli ni kwamba watu walipaswa kupewa elimu kuhusu chanjo lakini kwakuwa serikali haikutoa elimu kuhusu chanjo basi tumetoa mwanya wa watu kufundishwa na watu ambao pengine tusingependa na hayo ndio madhara ya chanjo ya hiari.
 
Ndugu kachomwe hata chanjo za ulimi peleka na familia yako hakuna anaekuzuia ukachome hadi za jicho ni wewe tu.. maisha ni hiari ya mtu na ukumbuke hizi chanjo ni emergency tu hivyo hazina hakika so for your own risk.
 
Kuna watu wanaongea utadhani ni walevi na wapuuzi hv toka lini Chanjo likawa ni jambo la lazima? Nitajie chanjo ambayo ni lazima Duniani?

Sikia nendeni au pekeleni familia zenu wakachanjwe si kulazimisha watu Mbowe unaemsema yeye kasema kachanjwa je unaushahidi gani au kakuonyesha vaccination card yake? Mbona ndugu zake Kilimanjaro wanapukutika wawapelekee Chanjo kwa nini anataka Watu Watanzania wote?

Chama cha Democrsia lakini mambo yake utadhani chama cha kigaidi wajinga sana nyinyi kama mmekula fedha za mabeberu mtazitapika

Chanjo yenyewe kila swali ukiuliza jibu ni NO si upuuzi tu huu
 
Kuna watu wanaongea utadhani ni walevi hv toka lini Chanjo likawa ni jambo la lazima? Nitajie chanjo ambayo ni lazima Duniani?

Sikia nendeni au pekeleni familia zenu wakachanjwe si kulazimisha watu Mbowe unaemsema yeye kasema kachanjwa je unaushahidi gani au kakuonyesha vaccination card yake?

Chama cha democrsia lakini mambo yake utadhani chama cha kigaidi
Mkuu soma mantiki ya huu uzi sasa kama tunasema chanjo ni hiari sasa kwanini tuna hangaika na Gwajima?
 
Kheeeee😲😲

DUNIANI KOTE CHANJO NI HIYARI NA SI LAZIMA

Tanzania si KOREA YA KASKAZINI

#TuacheSiasaZaVyamaKatikaSualaLaChanjo
#TujiandaeKuchanjwa
#TumuungeMkonoMh.RaisKwaKujitokezaChanjoni
#KaziIendelee
 
Kwa hiyo mtu akishawishiwa kutokwenda na asipo kwenda hakuna kosa kwani ni hiari
Mtu akishawishiwa kwenda na akafanikiwa kwenda bado hakuna kosa lolote.
Kama unayajua haya tatizo liko wapi kiasi cha kuanzisha uzi huu!?
 
Tatizo lilianzia mbali kidogo, tulipojikongoja shida ya Covid-19 ilipoanza, baadae tukajiandaa kuchukua tahadhari na kutoa elimu kwa kipindi kifupi, tena tukaanza kukatisha tamaa waliokuwa tayari kuzingatia taratibu za kujikinga na kuwashawishi wasiwe na hofu, hivyo kazi yote tuliyoianza ikarudi sifuri.

Kwa Sasa tunachokiona ni matunda ya kile tulichokipanda kwa tunaowataka wakaipate chanjo. Hali iko hivi kwakuwa tuliwafundisha ,na kuaminishwa isivyo wengi wakisikia chanjo, kwanza wanatanguliza nia ya chanjo yeyewe.

Kulingana na alivyoaminishwa, ila ukweli ni kuwa wale wauelewa wa kawaida wakisikia habari ya chanjo ni mbio nyingi kiasi hata cha kuacha mguu mmoja nyuma. Hivyo ipo kazi ya kutoa elimu upya kuanzia sifuri.
 
Mkuu soma mantiki ya huu uzi sasa kama tunasema chanjo ni hiari sasa kwanini tuna hangaika na Ngwajima?
Wanaoangaika na Gwajima ni wajinga tu coz walitakiwa kujibu hoja alzotoa yeye ametoa hoja jibuni hoja why unadeal na mtu badala ya hoja?

Why Serikali na hayo makampuni hayataki kubeba mzigo endapo Chanjo ikitokea kuleta madhara? Hv inaingia akilini mtu utoe pesa kununua bidhaa ya kula then mtengenezaji akatae kuwajibika na usalama wa Afya yako?
 
Wa
Wasalaam wana jamvi....
Mimi ni mmoja wa watu ambao kusema kweli nilitamani kabisa swala la chanjo liwe kwa lazima kwa kila mtanzania na hili lilipaswa kuwekwa wazi kabisa na Mh Rais pale alipotangaza ujio wa chanjo hiyo kwani ingesaidia sana kupambana na watu wanaopinga chanjo hiyo...
Ukitaka lazima tengeneza yako na familia yako.

Sisi hapa tz tutachanja tunavyojisikia
 
Kwa kuzingatia "hali ya hewa", serikali isingeweza kusema chanjo ni lazima.

Pia, bwaba Gwajima alishaipinga chanjo mapema kabisa kabla hata haijaja. So nadhani hata serikali ingesema ni lazima bado angepinga tu.

Sidhani Kama serikali imemuundia jamaa hiyo loophole.
 
Itakua lazima tu hivi karibuni pale utakapo ambiwa huwezi ingia hospitali bila kadi inayo onesha ume chanjwa.
 
Hivi thread nyingine ni za kutafuta ban tu,,,,😂😂😂maana hii ni bait kabisa,watu waje watukane waripotiwe
 
Back
Top Bottom