Rais Samia wasaidie wananchi hawa wa Kigamboni kuna wakubwa ‘wanawapiga’ katika ardhi yao

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,457

Inadaiwa kuwa huu mchongo unawahusisha vigogo wa kwenye mamlaka za juu na ndiyo maana kuna danadana zinaendelea.

Taarifa za uhakika kutoka wa watu ambao wamekuwa sehemu ya waathirika wa mradi huo kwa ardhi yao kutaka kuuzwa kwa bei ya chini amedai kuwa wameshafanya vikao vingi lakini hakuna muafaka na hiyo ni kwa kuwa kuna michezo mingi michafu inaendelea nyuma ya pazia.

Inaelezwa kuna wakati walikaa kikao na viongozi wa juu tena baadhi yao ni watauliwa wa Rais Samia kuhusu mgogoro huo, wakapikwa mkwara kuwa hawatakiwi kurekodi kwa kifaa chochote mazungumzo hayo, iwe ni kwa simu au kamera ya kawaida.

Kuna wananchi zaidi ya 2000 katika madai hayo, kati yao wapo wachache ambao wameshapozwa na hivyo wamekubali kuuza kwa bei hiyo ya buku tatu kwa square mita, wakati wenzao wengi wanataka buku nane kwa square mita.

Baada ya kiongozi mmoja mkubwa kufika eneo hilo na kufanya kikao, wakaamua kuunda kamati ndogo ili kushughulika na suala hilo, lakini hao wachache nao wakapewa kazi ya kuwashawishi wenzao ili wakubali kwa kuwa kuna maslahi ya wakubwa.

Najua Serikali ya mama Samia ni sikivu na lazima itadili na hao vigogo wanaotaka kuwanyonya wananchi kwa maslahi yao binafsi ya wachache.
 
Subirini msaada wa serkali.Mtasubiri sana kwa waziri Mabula amabaye hata jimboni kwake matatizo yamemshinda pamoja na Riz wake hapo hamna msaada nchi imerudi kwa wenyewe. Kidogo Lukuvi alikuwa na uthubutu wa kushughulika na matatizo ya wananchi.
 
Hilo neno wakubwa linaweza kuvuruga utekelezaji wa hilo unalohitaji lifanyike. Tumia neno mbadala hapo! Yaani wataje kwa majina hao unaowaita wakubwa.
 
Ni kila mtu na urefu wa kamba yake....., Its law of the Jungle..., kukanyagana na mwenye nguvu mpishe..., nikiangalia mbele the future is Scary..., tunapandikiza mbegu zitakazokuja kuwatafuna Watanzania wa Kesho...
 
Na mbaya zaidi huu mwendo wa kusifu na Propaganda, mabaya yanayotokea hayapewi airtime..., ni Mwendo wa Uchawa, Kusifu na kufanya kampeni za Uchaguzi ujao...,

Tumewekeza kwenye kujisifia na kujipongeza na sio kutafuta matatizo na kuyatatua bali kuyafunika na kujifanya kwamba hayapo (yakipatikana ni kuyatetea na kutupia lawama wengine)
 
Hii migogoro ya ardhi inatakiwa imalizwe mahakamani. Siyo kumuomba rais aingilie kati. Tatizo hizi mahakama zetu ni hovyo hovyo. Taasisi za nchi hii zinatakiwa kubomolewa na kujengwa upya. Kama vile Marekani ilivyomtoa Saddam Hussein madarakani Iraq, ikabomoa taasisi zote na kuzijenga upya.
 
Kikao kilivunjika, lakini kwa bahati mbaya sana Mkuu wa Wilaya na wapambe wake wakasema MRADI upo watake ama wasitake. Kuhusu malipo wanasema watawapatia 3,000 kwa mita moja za mraba. na uthamini umeshaanza kwa ubabe.

Huo ni wizi wa mchana kabisa, kigamboni wapi utapata eneo kwa bei hiyo?
 
Zumaridi kamteua naibu waziri wa ardhi kimkakati ili amalizie kupora ardhi kunufaisha matajiri
 
Dah! Mh.Ngungulile ukowapi watu wako wanateseka nawewe ndio mtetezi wao .so sad.
 
View attachment 2141771
Inadaiwa kuwa huu mchongo unawahusisha vigogo wa kwenye mamlaka za juu na ndiyo maana kuna danadana zinaendelea.

Taarifa za uhakika kutoka wa watu ambao wamekuwa sehemu ya waathirika wa mradi huo kwa ardhi yao kutaka kuuzwa kwa bei ya chini amedai kuwa wameshafanya vikao vingi lakini hakuna muafaka na hiyo ni kwa kuwa kuna michezo mingi michafu inaendelea nyuma ya pazia.

Inaelezwa kuna wakati walikaa kikao na viongozi wa juu tena baadhi yao ni watauliwa wa Rais Samia kuhusu mgogoro huo, wakapikwa mkwara kuwa hawatakiwi kurekodi kwa kifaa chochote mazungumzo hayo, iwe ni kwa simu au kamera ya kawaida.

Kuna wananchi zaidi ya 2000 katika madai hayo, kati yao wapo wachache ambao wameshapozwa na hivyo wamekubali kuuza kwa bei hiyo ya buku tatu kwa square mita, wakati wenzao wengi wanataka buku nane kwa square mita.

Baada ya kiongozi mmoja mkubwa kufika eneo hilo na kufanya kikao, wakaamua kuunda kamati ndogo ili kushughulika na suala hilo, lakini hao wachache nao wakapewa kazi ya kuwashawishi wenzao ili wakubali kwa kuwa kuna maslahi ya wakubwa.

Najua Serikali ya mama Samia ni sikivu na lazima itadili na hao vigogo wanaotaka kuwanyonya wananchi kwa maslahi yao binafsi ya wachache.
Aisee kama ni kweli huu ni ukatili wa hali ya juu sana! na serikali za mitaa zipo, diwani na mbunge wote wapo.. Mkurugenzi mwenyewe akipima ardhi hauzi kwa bei hiyo iweje mkubaliane na wawekezaji fidia za kinyama na kinyonyaji hivyo? Wenye access na Mama Samia wamfikishie hii clip atume watu wake kujua ukweli
 
Back
Top Bottom