Rais Samia, wakumbuke watumishi wa umma katika teuzi za Ma-DED, Ma-DAS na wakuu wa Taasisi za Umma

Bara na pwani

New Member
Jan 2, 2014
2
9
MHESHIMIWA RAIS SASA NI MUDA WA KUWAKUMBUKA WATUMISHI WA UMMA KATIKA TEUZI ZA MA-DED, MA-DAS na Wakuu wa Taasisi za Umma

1. Tunatambua nguzo kuu mbili katika utendaji wa serikali. Ya kwanza ni ile ya watendaji katika shughuli za kisiasa ikiwemo Mawaziri, Manaibu Waziri, ma-RC, na ma-DC. Ya pili ni ile watendaji walio katika utumishi wa umma ambao ni Makatibu wakuu, Naibu Katibu wakuu, ma-RAS, ma-DED, ma-DAS na Wakuu wa Taasisi za Umma.

2. Mheshimiwa Rais teuzi za ma-DC zilizotoka hivi karibuni, zimekamilisha orodha ya kujaza nafasi za watendaji wa kisiasa serikalini. Tunakupongeza sana kwa kuzingatia uwiano wa makundi mbalimbali hasa vijana kama ulivyoahidi katika hotuba yako ulipozungumza na vijana kutokea Mwanza.

3. Watumishi wa umma nao huwa wanakua katika ngazi mbalimbali za utumishi wao serikalini. Wengine wao hujiunga na utumishi wa umma katika ngazi ya uofisa utumikia katika ya miaka 3 hadi 9 kutegemea na kujiunga kupitia utumishi au kupitia taasisi zingine za umma. Kisha hupanda kuingia daraja la ofisa mwandamizi na kutumikia hapo katika ya miaka 4 hadi 6. Ngazi ya mwisho ni ya ofisa mkuu ambayo ndio ya juu kabisa kabla ya watendaji hawa kupandishwa katika ngazi ya uongozi ndani ya wizara, taasisi au kuteuliwa katika nafasi za utumishi wa umma nje ya wizara au taasisi zao.

4. Mheshimiwa Rais, watendaji hawa huwa wamekomaa na kuiva pale wanapokuwa wamefika ngazi ya maafisa wakuu lakini katika awamu zilizopita wachache sana wamekuwa wakiteuliwa na hivyo kusababisha mlundikano wa maafisa hawa wenye uzoefu mkubwa katika utendaji popote pale watakapopelekwa.

5. Katika kipindi cha nyuma teuzi nyingi zinazowahusu watumishi wa umma zimekuwa zikipewa makada na wanasiasa waliowahi kushika nafasi za kisiasa, ile mheshimiwa hii ni kuwanyima motisha watendaji wako ukizingatia wengi walio katika kada hii wametumikia kwa muda usiopungua miaka 10, kwa kuwapandisha au kuwapa majukumu mengine inatoa nafasi kwa serikali kuajiri vijana kujaza nafasi katika utumishi wa umma.

6. Mheshimiwa naomba nitoe wito kwako katika nafasi za teuzi zijazo za ma-DAS, ma-DED na wakuu wa Taasisi za Umma uwakumbuke watendaji wako ambao wako tayari kuendelea kutumikia serikali yao na ikiwezekana uwe na kanzi data ya watumishi hawa wakuu kutoka sekta zote kwenye serikali yako ili mara zote uwe unaweza kuitumia pale unahitaji kuboresha maeneo ya kiutendaji katika serikali yako.
 
MHESHIMIWA RAIS SASA NI MUDA WA KUWAKUMBUKA WATUMISHI WA UMMA KATIKA TEUZI ZA MA-DED, MA-DAS na Wakuu wa Taasisi za Umma

1. Tunatambua nguzo kuu mbili katika utendaji wa serikali. Ya kwanza ni ile ya watendaji katika shughuli za kisiasa ikiwemo Mawaziri, Manaibu Waziri, ma-RC, na ma-DC. Ya pili ni ile watendaji walio katika utumishi wa umma ambao ni Makatibu wakuu, Naibu Katibu wakuu, ma-RAS, ma-DED, ma-DAS na Wakuu wa Taasisi za Umma.

2. Mheshimiwa Rais teuzi za ma-DC zilizotoka hivi karibuni, zimekamilisha orodha ya kujaza nafasi za watendaji wa kisiasa serikalini. Tunakupongeza sana kwa kuzingatia uwiano wa makundi mbalimbali hasa vijana kama ulivyoahidi katika hotuba yako ulipozungumza na vijana kutokea Mwanza.

3. Watumishi wa umma nao huwa wanakua katika ngazi mbalimbali za utumishi wao serikalini. Wengine wao hujiunga na utumishi wa umma katika ngazi ya uofisa utumikia katika ya miaka 3 hadi 9 kutegemea na kujiunga kupitia utumishi au kupitia taasisi zingine za umma. Kisha hupanda kuingia daraja la ofisa mwandamizi na kutumikia hapo katika ya miaka 4 hadi 6. Ngazi ya mwisho ni ya ofisa mkuu ambayo ndio ya juu kabisa kabla ya watendaji hawa kupandishwa katika ngazi ya uongozi ndani ya wizara, taasisi au kuteuliwa katika nafasi za utumishi wa umma nje ya wizara au taasisi zao.

4. Mheshimiwa Rais, watendaji hawa huwa wamekomaa na kuiva pale wanapokuwa wamefika ngazi ya maafisa wakuu lakini katika awamu zilizopita wachache sana wamekuwa wakiteuliwa na hivyo kusababisha mlundikano wa maafisa hawa wenye uzoefu mkubwa katika utendaji popote pale watakapopelekwa.

5. Katika kipindi cha nyuma teuzi nyingi zinazowahusu watumishi wa umma zimekuwa zikipewa makada na wanasiasa waliowahi kushika nafasi za kisiasa, ile mheshimiwa hii ni kuwanyima motisha watendaji wako ukizingatia wengi walio katika kada hii wametumikia kwa muda usiopungua miaka 10, kwa kuwapandisha au kuwapa majukumu mengine inatoa nafasi kwa serikali kuajiri vijana kujaza nafasi katika utumishi wa umma.

6. Mheshimiwa naomba nitoe wito kwako katika nafasi za teuzi zijazo za ma-DAS, ma-DED na wakuu wa Taasisi za Umma uwakumbuke watendaji wako ambao wako tayari kuendelea kutumikia serikali yao na ikiwezekana uwe na kanzi data ya watumishi hawa wakuu kutoka sekta zote kwenye serikali yako ili mara zote uwe unaweza kuitumia pale unahitaji kuboresha maeneo ya kiutendaji katika serikali yako.
Huu ni ushauri muajarabu kabisa kwa mheshimiwa mama yetu. Watumishi wa umma wakongwe ni hazina kwa nchi hivyo watasaidia sana wakiaminiwa.
 
Well spoken, Taifa letu limekuwa na nafisadi kutokana na viongozi wa kisiasa. Watumishi wa umma wamejifunza maadili katika Utumishi wa umma na kwa uzoefu mtu mwenye siha njema watakuwa wanajulikana na hivyo kupata fursa ya kutumikia nchi yao. Tukumbuke chama cha Mapinduzi ni chama cha wakulima na wafanyakazi, kwa hiyo serikali yake iwatumie watu hawa kwenye utawala kuliko wafanyabiashara (mabwenyenye). Naamni mama atauona na kufuatilia uzi huu na hatimae kuchukua mawazo ya wadau.
 
MHESHIMIWA RAIS SASA NI MUDA WA KUWAKUMBUKA WATUMISHI WA UMMA KATIKA TEUZI ZA MA-DED, MA-DAS na Wakuu wa Taasisi za Umma

1. Tunatambua nguzo kuu mbili katika utendaji wa serikali. Ya kwanza ni ile ya watendaji katika shughuli za kisiasa ikiwemo Mawaziri, Manaibu Waziri, ma-RC, na ma-DC. Ya pili ni ile watendaji walio katika utumishi wa umma ambao ni Makatibu wakuu, Naibu Katibu wakuu, ma-RAS, ma-DED, ma-DAS na Wakuu wa Taasisi za Umma.

2. Mheshimiwa Rais teuzi za ma-DC zilizotoka hivi karibuni, zimekamilisha orodha ya kujaza nafasi za watendaji wa kisiasa serikalini. Tunakupongeza sana kwa kuzingatia uwiano wa makundi mbalimbali hasa vijana kama ulivyoahidi katika hotuba yako ulipozungumza na vijana kutokea Mwanza.

3. Watumishi wa umma nao huwa wanakua katika ngazi mbalimbali za utumishi wao serikalini. Wengine wao hujiunga na utumishi wa umma katika ngazi ya uofisa utumikia katika ya miaka 3 hadi 9 kutegemea na kujiunga kupitia utumishi au kupitia taasisi zingine za umma. Kisha hupanda kuingia daraja la ofisa mwandamizi na kutumikia hapo katika ya miaka 4 hadi 6. Ngazi ya mwisho ni ya ofisa mkuu ambayo ndio ya juu kabisa kabla ya watendaji hawa kupandishwa katika ngazi ya uongozi ndani ya wizara, taasisi au kuteuliwa katika nafasi za utumishi wa umma nje ya wizara au taasisi zao.

4. Mheshimiwa Rais, watendaji hawa huwa wamekomaa na kuiva pale wanapokuwa wamefika ngazi ya maafisa wakuu lakini katika awamu zilizopita wachache sana wamekuwa wakiteuliwa na hivyo kusababisha mlundikano wa maafisa hawa wenye uzoefu mkubwa katika utendaji popote pale watakapopelekwa.

5. Katika kipindi cha nyuma teuzi nyingi zinazowahusu watumishi wa umma zimekuwa zikipewa makada na wanasiasa waliowahi kushika nafasi za kisiasa, ile mheshimiwa hii ni kuwanyima motisha watendaji wako ukizingatia wengi walio katika kada hii wametumikia kwa muda usiopungua miaka 10, kwa kuwapandisha au kuwapa majukumu mengine inatoa nafasi kwa serikali kuajiri vijana kujaza nafasi katika utumishi wa umma.

6. Mheshimiwa naomba nitoe wito kwako katika nafasi za teuzi zijazo za ma-DAS, ma-DED na wakuu wa Taasisi za Umma uwakumbuke watendaji wako ambao wako tayari kuendelea kutumikia serikali yao na ikiwezekana uwe na kanzi data ya watumishi hawa wakuu kutoka sekta zote kwenye serikali yako ili mara zote uwe unaweza kuitumia pale unahitaji kuboresha maeneo ya kiutendaji katika serikali yako.
Ushauri wako ni mzuri sana.

Naomba Mh. Rais pia azingatie suala Ia kuwahamisha baadhi ya watumishi wa umma hasa wakuu wa Idara za Halmashauri pamoja na Ma-DAS kutoka kituo kimoja kwenda kituo kingine ili kuleta tija na utendaji mzuri wa kazi katika utumishi wa Umma.

Mfano:-
Unamkuta Mkuu wa Idara au DAS kakaa kituo kimoja zaidi ya miaka 10 na kuendelea.
Hapo unategemea tija gani tofauti na kufanya kazi kwa mazoea, kupika majungu kila siku na kujiona miungu watu???


KAZI IENDELEE KWA UBORA STAHIKI.

Nawasilisha!
 
Teuzi zimekua za machawa, mahawara za watu Fulani Fulani, kujuana , ukada wa wazazi, kuhujumu wapinzani, sehemu ya kupeana ulaji n.k.

Nafasi ya Uwaziri, Ukurugenzi, UDC, uRC ni nafasi za heshima sana lakini Cha ajabu Kwa Sasa wanapewa watu wa ajabu ajabu kuzishika. DC anamwakilisha Rais kwenye Wilaya halafu anapewa mtu ambaye Hana uwezo na uzoefu wowote zaidi ya kuwa Chawa .

Tuna feli sana Kwa kweli . Ndio maana watu wanatamani nafasi hizo zifutwe Kwa kuwa hazitolewi Kwa sifa zilizoko wazi.
Siku hizi mpaka Wakurugenzi wanateuliwa watu wasiofaa . Mkurugenzi anapaswa kuwa mtumishi wa serikali ambaye ni siour ,mwenye uwezo ,uzoefu na mwadilifu
 
Back
Top Bottom