Rais Samia, wabunge 19 waliofukuzwa CHADEMA wanaiba kodi za masikini

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Feb 19, 2021
3,086
4,881
Hakika nichukue nafasi hii kukupongeza kwa hatua mbalimbali ulizochukua na unazochukua kurekebisha mambo ya nchi yetu.

Kubwa nililotaka kukushauri ni hili la wabunge 19 waliofukuzwa na Chadema kuendelea kuwa bungeni na kulipwa mishahara ambayo ni kodi za masikini wa nchi hii.

Rais Samia uliapa kuilinda na kuihifadhi katiba ya nchi na katiba inatamka wazi moja ya sifa ya mbunge kupoteza ubunge ni kufukuzwa na chama chake wabunge hao 19 wamefukuzwa na chama chao lakini mpaka leo wanalindwa na spika haijulikani ni kwa faida ya nani.

Kitendo cha kuwalipa mishahara wakati sio wabunge halali ni wizi na uhujumi uchumi. Ni imani yetu utalichukulia hatua hilo ili kuokoa kodi za wananchi.
 
Bunge ni mhimili, Samia kikatiba sidhani kama ana nguvu ya kuingilia Hilo, cha msingi shaur lipelekwe Mahakamani, mahakama itoe haki. Kama ana nguvu hyo Sawa
 
Na hao 19 ikitokea wametolewa ndio litakuwa bunge la CCM pure.
 
Bunge ni mhimili , Samia kikatiba sidhani kama ana nguvu ya kuingilia Hilo , cha msingi shaur lipelekwe Mahakamani , mahakama itoe haki....!! Kama ana nguvu hyo Sawa
Fedha inayoibiwa ni ya SERIKALI sio BUNGE na Serikali ni Yeye ndio Mkuu wa Huo Muhimili Bado ana Wajibu wa Kuhakikisha KODI za Wananchi Haziibiwi na Bado ana Wajibu wa Kuhakikisha Katiba Haichezewi
 
Kwani wangepelekwa na chadema wasingelipwa stahiki hizi wanazolipwa?

Je, huoni ni heri akina Mdee angalau wanaibua hoja za maana bungeni kuliko akina Zungu wanaopendekeza tuongezewe kodi kila siku?
 
Nchi hii inapitia kipindi kigumu sana, mama yenu hatoshi mnampaisha tu.
 
Kwani wangepelekwa na chadema wasingelipwa stahiki hizi wanazolipwa?

Je, huoni ni heri akina Mdee angalau wanaibua hoja za maana bungeni kuliko akina Zungu wanaopendekeza tuongezewe kodi kila siku?
Hawakufuata taratibu za chama. Watoke hadharani waseme nani aliwapeleka huko ili wananchi tujue na maamuzi yatolewe, kama ni msamaha au vinginevyo. Vyama vina taratibu za kuteua wanachama wao kwenda viti maalumu. Hawa walikiuka taratibu ndiyo maana wakafukuzwa.
 
Fedha inayoibiwa ni ya SERIKALI sio BUNGE na Serikali ni Yeye ndio Mkuu wa Huo Muhimili Bado ana Wajibu wa Kuhakikisha KODI za Wananchi Haziibiwi na Bado ana Wajibu wa Kuhakikisha Katiba Haichezewi
Fuata Katiba na Sio hela hata Spika analipwa hela ya Serikali
 
1624259487059.png

Gado amesha tamka, msipomsikiliza hayo ni matatizo yenu.
 
Bunge ni mhimili, Samia kikatiba sidhani kama ana nguvu ya kuingilia Hilo, cha msingi shaur lipelekwe Mahakamani, mahakama itoe haki. Kama ana nguvu hyo Sawa
Hawa wabunge 19 wanapaswa kurudisha pesa zote wanazolipwa
 
Jamani hao sio wabunge, ili uwe mbunge wa viti maalum lazima uwe mwanchama wa chama cha siasa hao ni Kovidi - 19 bunge linatakiwa lipigwe nyungu ili waondoke😂🐒🤸
 
Wale waliingia makubaliano na CCM na yakawa binded, kwa hiyo mama anasita kidogo kuwatimua bungeni sababu kwa kufanya hivyo anakuwa anakwenda kinyume na maamuzi ya chama chake, ni lazima aheshimu yaliyoamuliwa na mtangulizi wake.

Hapa ndipo ugumu ulipo, maslahi ya CCM kwanza.
 
Hakika nichukue nafasi hii kukupongeza kwa hatua mbalimbali ulizochukua na unazochukua kurekebisha mambo ya nchi yetu.

Kubwa nililotaka kukushauri ni hili la wabunge 19 waliofukuzwa na Chadema kuendelea kuwa bungeni na kulipwa mishahara ambayo ni kodi za masikini wa nchi hii.

Rais Samia uliapa kuilinda na kuihifadhi katiba ya nchi na katiba inatamka wazi moja ya sifa ya mbunge kupoteza ubunge ni kufukuzwa na chama chake wabunge hao 19 wamefukuzwa na chama chao lakini mpaka leo wanalindwa na spika haijulikani ni kwa faida ya nani.

Kitendo cha kuwalipa mishahara wakati sio wabunge halali ni wizi na uhujumi uchumi. Ni imani yetu utalichukulia hatua hilo ili kuokoa kodi za wananchi.
Walifukuzwa na naniii??? Acheni wivu zenu
 
Maisha yanakwenda kasi sana yaani ni kama jana tu kila alilosema Halima Mdee na Esther Matiku lilikuwa mjadala humu jukwaani lakini leo wanafananishwa na uviko19.

Hakika Kesho ni siri kubwa.
 
Wanapata heshima hii miaka minne,
Subiri baada ya hapo na ndugai atakuwa amestaafu kwa manufaa ya uviko 19
 
Hakika nichukue nafasi hii kukupongeza kwa hatua mbalimbali ulizochukua na unazochukua kurekebisha mambo ya nchi yetu.

Kubwa nililotaka kukushauri ni hili la wabunge 19 waliofukuzwa na Chadema kuendelea kuwa bungeni na kulipwa mishahara ambayo ni kodi za masikini wa nchi hii.

Rais Samia uliapa kuilinda na kuihifadhi katiba ya nchi na katiba inatamka wazi moja ya sifa ya mbunge kupoteza ubunge ni kufukuzwa na chama chake wabunge hao 19 wamefukuzwa na chama chao lakini mpaka leo wanalindwa na spika haijulikani ni kwa faida ya nani.

Kitendo cha kuwalipa mishahara wakati sio wabunge halali ni wizi na uhujumi uchumi. Ni imani yetu utalichukulia hatua hilo ili kuokoa kodi za wananchi.
Hang on. It is a matter of time. Mama, Speaker, and the "Covid-19 gang" are sitting on a time bomb. It will eventually erupt disastrously.
 
Back
Top Bottom