Rais Samia utawezaje kujinasua na sifa bandia na kuharibu mafanikio ya watangulizi wako?

robinson crusoe

JF-Expert Member
Oct 22, 2020
740
1,214
Kuharibu sifa za watangulizi ni mtindo ulioanzishwa na Kikwete ndani ya chama kile kile cha CCM! Nauona ukiendelea kwa nguvu zote. Maofisini wizi umepamba moto.

Alipoingia Kikwete alimfanya Mkapa kama ni hovyo kabisa! Wafuasi wake wakaanza kumzomea barabarani. Hata sherehe za kitaifa akasusia nchi ikawa ni ya wana-Mtandao. Sifa zoote zikawa ni za Kikwete naye akaamini ni kiongozi bora. Waliokuwa wanamsifu wakafanya yao, nchi ikawa ni kwa sifa zote kwa rais.

Akaingia Magufuli. Wafuasi wake wakasema bora! Yako wapi? Kikwete kaa mbali umeharibu nchi. Mfumo wa nchi ukaundwa upya. Wanamtandao wakaona kama wanaonewa maana walishaaminishwa nchi ni yao kwa miaka 10. Mkapa akaibuka toka mafichoni kwa urafiki na JPM. Wananchi wakashangilia na wengine wakasononeka. Kikwete hakukata tama, akatembelea ikulu mara nyingi sana, hatimaye akagundua hana chake bora aendelee na biashara mitaani. Lakini biashara bila wizi wa kiserikali hailipi! Naamini tamaa ikarudi kwenye madaraka.

Ameingia Samia. Kikwete kaibuka kama ilivyokuwa kwa MKapa. Wafuasi wa Kikwete wakasema nafuu!! Teuzi zikaanza upya yeye akisema anafungua nchi. Walioachwa wakaokotwa tena bila kusafishwa. Waliokuwa kwa magufuli baadhi wakatoswa. Sifa zimehamia kwa Samia. MAMA! MAMA! Kila kona anaitwa MAMA.

Je, kweli anafanya kazi vizuri au ni mtindo ule ule wa kutukuzwa na kumfanya aliyepita hana maana ili waendelee ‘kuipiga’ nchi? Ndivyo tuonavyo! Tangu lini waliochafuka wakawa wasafi bila kusafishwa?
 
Tuliopo nje ya mfumo hatujui mengi yaliyokuwa yanaendelea au yanayoendelea sasa hivyo tunabaki na imani moja kumuamini mfanya maamuzi. Kama Samia anaona watangulizi wake hawakufanya vizuri naweza kusema yupo sahihi kwa sababu kwa nafasi yake anaelewa mengi yaliyojificha na yaliyofichwa
 
Magufuli hakusiwa?, Hukusikia serikali ya magufuli mpaka siku moja mzee Mkapa akalisemea kwa ukali. Hili tatizo lipo na usiongelee kwa kuangalia Samia au ulikua sayari ya Jupiter kipindi Cha awamu ya tano?. Huwa nafikiria kwa nini Samia anaandamwa hivi? Shida naamini ni jinsia.
 
Magufuli hakusiwa?, Hukusikia serikali ya magufuli mpaka siku moja mzee Mkapa akalisemea kwa ukali. Hili tatizo lipo na usiongelee kwa kuangalia Samia au ulikua sayari ya Jupiter kipindi Cha awamu ya tano?. Huwa nafikiria kwa nini Samia anaandamwa hivi? Shida naamini ni jinsia.
Serikali zetu hizi ni hovyo tu. Hata leo umsifie Samia, ukweli ni kwamba viongozi tulionao wote ni daraja la chini kuliko walioko dunia ya wanaojitambua.
 
Tuliopo nje ya mfumo hatujui mengi yaliyokuwa yanaendelea au yanayoendelea sasa hivyo tunabaki na imani moja kumuamini mfanya maamuzi. Kama Samia anaona watangulizi wake hawakufanya vizuri naweza kusema yupo sahihi kwa sababu kwa nafasi yake anaelewa mengi yaliyojificha na yaliyofichwa
Hakuna lolote, anafanya vizuri kupandisha vitu bei?
 
Hao wote wamekaa miaka zaidi ya 25 ila hakuna ata mmoja aliyeweza kumaliza tatizo ata la madawati kwenye shule zetu.

Viongozi wa chini wameshajua professional au udhoefu hauna mchongo wewe kua msifiaji utaishi kwa neema na kuogopwa
 
Hao wote wamekaa miaka zaidi ya 25 ila hakuna ata mmoja aliyeweza kumaliza tatizo ata la madawati kwenye shule zetu.

Viongozi wa chini wameshajua professional au udhoefu hauna mchongo wewe kua msifiaji utaishi kwa neema na kuogopwa
Kwa miaka 10 yote ya kikwete wanafunzi walikaa chini, mavumbini! Shule za kata za Lowasa hazikuangaliwa kabisa! Magufuli akatikisa angalau madawati yakapatikana. Naye alipoanza miradi inayoitwa mikubwa, mambo yako chini na huyu aliyekuja hana hata mpango zaidi ya kuteua watu wa NGO waongoze serikali!

Viongozi wa kiafrika akili ni hovyo tu! Halafu unakuta limtu linataja Kikwete! Kikwete!, Magufuli! Magufuli! sasa tena Samia! Samia! kila wakati.
 
Magufuli hakusiwa?, Hukusikia serikali ya magufuli mpaka siku moja mzee Mkapa akalisemea kwa ukali. Hili tatizo lipo na usiongelee kwa kuangalia Samia au ulikua sayari ya Jupiter kipindi Cha awamu ya tano?. Huwa nafikiria kwa nini Samia anaandamwa hivi? Shida naamini ni jinsia.
Mwandishi kachambua vizuri tu isipokuwa wewe ndo unaingia kishabiki. Mkielezwa mnakimbilia jinsia. Tanzania tumekuwa na viongozi wengi wa kike mbona hawajasemwa hivyo kama ni jinsia. Mbona alikuwa makamu wa Rais, hakusemwa, na ni ngazi ya juu ya uongozi. Huo ujinsia au uanamke umeanza leo? Watu wanaangalia utendaji si jinsia!

Tumekuwa na maspika wa kike mbona hatujawahi sikia kulaumiwa na kuwepo utetezi wa jinsia. Tumekuwa na Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dr. Asha Rose Migiro mbona hatukusikia ujinsia au kulaumiwa! Tumekuwa na kina Bibi Titi mbona hatukusikia ujinsia, tumekuwa na Balozi Getrude Mongela wote hawa walikuwa na nafasi kubwa, bali walionekana ni moja ya viongozi mahiri.

Tuache kukimbilia kwenye kichaka cha jinsia kuficha madhaifu. Ni uwazi kuwa serikali ya awamu ya nne ndo iliyoanzisha haya mambo. Nakumbuka siku moja kwa mdomo wa Mkapa mwenyewe tukiwa sehemu fulani, alionesha jinsi alivyotengwa na kuonekana hafai wakati wa awamu ya nne.

Kuna wakati wale wazee wa Nyerere foundation, walibezwa, waliangaika sana kupata eneo la kujenga jengo lao. Walipigwa vita na hawakupata msaada toka serikali ya awamu ya nne. Mpaka alipoingia Magufuli ndo wakawezeshwa na hatimae kukamilisha jengo husika. Kisa kuna mtu alitaka yeye awe yeye chuki za kukataliwa na Nyerere wakati ule zilimkaa moyoni.
 
Magufuli hakusiwa?, Hukusikia serikali ya magufuli mpaka siku moja mzee Mkapa akalisemea kwa ukali. Hili tatizo lipo na usiongelee kwa kuangalia Samia au ulikua sayari ya Jupiter kipindi Cha awamu ya tano?. Huwa nafikiria kwa nini Samia anaandamwa hivi? Shida naamini ni jinsia.
Mkapa alikemea tabia ya sifa kwenda kwa JPM akataka ziende kwa CCM wote wakiwa ni watumishi wa serikali ya chama tawala.
 
Back
Top Bottom